Sunday, October 25, 2015

KITUO CHA SEGEREA MAGEREZA HALI NI SHWARI WENGI WAJITOKEZA KUPIGA KURA

 Wakazi wa Segerea wakiwa katika foleni kwaajili ya kuendelea na zoezi la kupiga kura katika kituo cha Magereza Segerea muda huu huku hali ya usalama ikiwa shwari kabisa
 Foleni ikiwa bado ndefu huku mwamko ukiwa mkubwa kwa rika zote kuanzia vijana na wakina mama na baba zoezi linaendelea vizuri mpaka sasa
 Blogger Josephat Lukaza akiwa katika  foleni ya kupiga kura katika kituo changu cha Magereza segerea kwaajili ya kupiga kura kumchagua kiongozi atakayenifaa
Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog
 Wakazi wa Segerea ambao wamejiandikisha katika kituo cha Segerea Magereza wakiwa wamejitokeza kwa wingi muda huu katika kituo hiko kwaajili ya kushiriki zoezi la kupiga kura kuwachagua viongozi mbalimbali kuanzia Rais, wabunge na Madiwani. Hali ni shwari hakuna vurugu wala viashiria vyovyote vile vya vurugu japokuwa kuna changamoto za hapa na pale ambapo mkazi mmoja ameambiwa na msimamizi wa uchaguzi kuwa hawezi kupiga kura kutokana na namba ya Kitambulisho chake cha kupigia Kura kutofautiana tarakimu moja tu na Namba ya kitambulisho iliyoandikwa katika karatasi la majina ya kuhakiki. Mkazi huyo ambaye hakupenda jina lake litajwe amesema kuwa anasubiri Mkuu wa kituo cha Uchaguzi Segerea Magereza kuweza kuongea nae na Kutatua swala hilo endapo ataruhusiwa basi atapiga kura na asiporuhusiwa basi hatopiga kura
Wakazi wa Segerea wakiwa kwenye foleni kusubiri kupiga kura
Baadhi ya wakazi wa segerea wakiwa katika foleni tayari kwa kupiga kura.

No comments: