Wednesday, October 21, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO, KATIKA KITUO CHA KUTUNZIA KUMBUKUMBU CHA TAIFA (NATIONAL INTERNET DATA CENTRE) KIJITOMYAMA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuzindua Jengo jipya la Mradi wa Kituo cha Kutunzia kumbukumbu Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi iliyofanyika leo Kijitonyama, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib, akipata maelezo kuhusu utendaji kazi wa mitambo ya kutunzia kumbukumbu, kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Bidhaa za Shirika la Simu Tanzania, TTCL, Issaya Ernest, wakati Dkt Bilal, alipotembelea kituo hicho cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, leo Okt 21, 2015.
 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa, kwa pamoja wakifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, leo Okt 21, 2015.
   
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa (kushoto) na Mwakilishi wa Ofisi ya Uchumi na Biashara ya Serikali ya China, nchini Tanzania, Lin Zhiyong,  kwa pamoja wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, leo Okt 21, 2015.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Simu Tanzania TTCL, wakati alipotembelea kituo hicho cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, leo Okt 21, 2015. Kushoto ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa (kulia) ni Afisa Mtendaji wa TTCL, Dkt. Kamugisha Kazaura.

 Mrisho Mpoto na wasanii wa bendi yake ya Mjomba, wakitoa burudani.
 Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa, akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Makamu wa Rais, kuhutubia.
 Sehemu ya wafanyakazi wa Shirika la Simu Tanzania, wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati alipokuwa akizungumza nao baada ya kutembelea mitambo hiyo, Kijitonyama.  
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa hafl ya uzinduzi wa Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, jijini Dar es Salaam leo Okt 21, 2015.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akibofya kitufye kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo Okt 21, 2015.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Afisa Mtendaji wa TTCL, Dkt. Kamugisha Kazaura, wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo Okt 21, 2015.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa hafla ya uzinduzi huo baada ya kuzindua rasmi leo Okt. 21, 2015 Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.
Picha na OMR

No comments: