Mkurugenzi wa Uchaguzi Wa CHADEMA Bwana REGNALD MUNISI akizungumza na wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam |
Na Exaud Msaka Habari
Chama cha Democrasia na
maendeleo CHADEMA kwa kupitia umoja wa katiba UKAWA wametangaza kuwa kwa mujibu
wa utafiti uliofanywa na vyama hivyo nchi nzima wamejihakikishia ushindi wa
asilimia 61% katika uchaguyzi mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani unaotaraji kufanyika
jumapili ya wiki hii nchini Tanzania.
Akizungumza na
wanahabari mapoema leo mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho Bwana REGINALD
MUNISI ametanabaisha kuwa kila chama cha siasa kina utaratibu wake wa kuangalia
ni jinsi gani kinakubalika na ushindi aina gani kinaweza kupata katika ucgauzi
ambapo amesema wao wamekuwa wakitumia mfumo wa kawaida wa Pool ambazo ni Tafiti
wanazofanya mikoa yote Tanzania ili kupioma wana nafasi gani katika uchaguzi
mkuu wa mwaka huu.
Amesema kuwa kuwa
mujibu wa Utafiti waliofanya mwishoni mwa wiki jana(wikiend iliyopita) na
kuwahusisha watanzania zaidi ya elfu 30,Umeonyesha kuwa umoja wa katiba ya
wananchi kupitia mgombea wao wa Urais Edward Lowasa ana nafasi ya kushinda kiti
hicho kwa asilimia 61% ya kura zote ambazo zitapigwa nchini Tanzania.huku
akisema kuwa wana imani ndani ya siku zilizobaki hakiwezi kubadilika kitu
kikubwa katika takwimu hizo.
Bwana Munisi amesema
kuwa chama hicho pamoja na umoja wa katiba ya wananchi sasa umejiridhisha wazi
kuwa wanakwenda kushinda kwa kishindo katika uchaguzi wa mwaka huu hivyo
wapenzi na watanzania kutokuwa na hofu ya aina yoyote kuhusu amani ya Tanzania.
Katika hatua nyingine
vyama hivyo vimeitaka serikali iliyoppo madarakani kuwapa wananchi wa Tanzania kuamua
hatma ya nchi yao kupitia sanduku la kura na kupitia katiba ya Tanzania kwani
kumeanza kuonekana aina ya vitisho ambavyo amesema kwa namna moja ama nyingine
vinaweza kuwafanya watanzania kuwa na hofu juu ya uchaguzi huo.
Amesema kuwa ni wazi
kumekuwa na vihoja vingi,na maneno mengi ambayo yamekuwa yakisemwa na wapinzani
wao yakiwa na lengo la kuwaaminisha watu kuwa wapinzani hawana uwezo wa
kushinda ambapo amesema kuwa kupindi kama hiki ni lazima maswala hayo
yajitokeza ambapo amesema sio kikwazo katika ushindi wa uchaguzi wa mwaka huu.
Aidha umoja huo
wametangaza rasmi kuwa kampeni za mgombea Urais wa chama hicho Edward Lowasa
zitafungwa siku ya tarehe 24 katika viwanja vya jangwani Jijini Dar es salaam
ambapo mipango ya shughuli hiyo inaendelea na itakapokamilika itawekwa wazi
No comments:
Post a Comment