Msemaji wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA Bwana TUMAIN MAKENE |
Umoja wa katiba ya
wananchi UKAWA umetangaza kusimamisha kwa kampeni zake kwa nchi nzima kwa siku
ya kesho kwa ajili ya kumuaga na maziko ya aliyekuwa mwenyekitri mwenza wa
umoja huo na mwenyekiti wa chama cha NLD Dk EMMANUEL MAKAID ambaye anataraji
kuzikwa kesho jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na msemaji wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA Bwana
TUMAIN MAKENE amesema kuwa Team zote za kampeni za umoja huo kesho
zitalazimika kusimamisha kampeni na kurejea Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa mwenyekiti huyo aliyekuwa na mchango mkubwa katika
umoja huo.
Mwenyekiti wa chama cha NLD Dk. Emmanuel Makaidi enzi za uhai wake |
Kwa mujibu wa taarifa
hiyo mwili wa Marehemu MAKAID utaagwa katika viwanja vya karimjee na baadae
kuzikwa katika makaburi ya sinza Jijini Dar es salaam ambapo viongozi wakubwa
wa vyama hivyo watashiriki akiwemo pia Mgombea urais wa Umoja huo Mh Edward
Lowasa na viongozi wengine kutoka serikalini na Taasisi mbalimbali
No comments:
Post a Comment