Hatimaye chama cha
Democrasia na maendeleo CHADEMA Pamoja na umoja wa katiba ya wananchi UKAWA
wameandika barua kwenda kwa Katibu Mkuu wa umoja wa mataifa Ba Ki-moon,Barua
ambayo pia imeenda katika mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ya
ICC,pamoja na jumuiya za kimataifa,barua
imnayowasilisha malalamiko ya vyama hivyo juu ya kile walichoita kauli
za vitisho na rafu zinazifanywa na serikali juu ya vyama hivyo kuelekea
uchaguzi mkuu wa wiki ijayo.
Akizumgumza na
wanahabari mapema leo mwanasheria wa chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA
JOHN MALLYA amesema kuwa wameamua kuandika barua hiyo kutokana na kile walichoita
ni kauli za vitisho zilivyotolewa na Rais wa Tanzania JAKAYA KIKWETE juu ya
wananchi jambo ambalo amesema wametaka kutoa taarifa katika taasisi hizo na
kuhoji kama ni sahihi kwa Rais kutoa kauli kama hizo.
Amesema kuwa maamuzi ya
kuandika barua kwa taasisi hizo yamekuja kutokana na uwazi kuwa kwa mujibu wa
sheria za Tanzania huwezi kumshataki Rais kutokana na kinga aliyonayo hivyo
wameona ni muhimu kufikisha swala hilo kwa jumuiya za kimataifa ili waendelee
kuitambua hali halisi inayoendelea na kama wanaweza kutoa maelekezo kwa Rais
kuacha kuwatisha wananchi kipindi hiki cha uchaguzi.
Kauli ambazo
zinalalamikiwa na Umoja huo ni kauli aliyoitoa Rais Kikwete juu ya swala la
wananchi kukaa meter mia mbili kulinda kura ambapo aliagiza vyombo vya dola
kuwashiughulikia wote ambao watafanya hivyo huku vyama hivyo vya upinzani
wakisisitiza kuwa swala hilo lipo kisheria na kuendelea kuwahamasisha wananchi
na wanachama wao kulinda kura baada ya kumaliza kupiga kura zao.
Barua hiyo iliyopelekwa
asubuhi ya leo ambayo imesainiwa na
makamu mweyekiti wa CHADEMA Profesa ABDALA SAFARI imepekekwa pia nakala zake
common wealth London,African Union,pamoja na mahakama ya kimataifa ya makosa ya
jinai ya uholanzi ICC.
No comments:
Post a Comment