Tuesday, November 10, 2015

JESHI LA POLISI LAANZA KUTOA ELIMU KWA ABIRIA NA MADEREVA ILI KUKABILIANA NA AJALI KATIKA KIPINDI CHA MWISHO WA MWAKA

Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, PC Asha Adam, akiwasisitiza abiria kufunga mikanda  iliyopo kwenye viti walivyoketi muda wote wa safari muda mfupi kabla ya magari  kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi ya abiria Ubungo, jijini Dar es Salaam, kama hatua ya kudhibiti majeraha na vifo vitokanavyo na ajali za barabarani, kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka,

Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Inspekta Ibrahim Omary Samwi(kushoto), na PC Elisante Bura(kulia), wakikagua moja ya magari yanayofanya safari zake mikoani, kutekeleza mkakati wa Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka.Zoezi hili limefanyika  muda mfupi kabla ya magari  kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo,jijini Dar es Salaam kuelekea mikoa mbalimbali ya Tanzania .

Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Inspekta Ibrahim Omary Swami(aliyeko chini ya uvungu wa gari), akikagua moja ya magari yanayojiandaa kuelekea mikoani, zoezi ambalo limefanyika muda mfupi kabla ya magari kuanza kuondoka katika kituo Kikuu cha Mabasi, Ubungo jijini Dar es Salaam.aliyenyoosha kidole juu ni PC Elisante Bura. Hatua hii ya Jeshi la Polisi nchini  linalenga kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka,.
Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Sajenti Jackson Mafuru (kulia), na PC Elisante Bura(kushoto), wakikagua moja ya magari yanayofanya safari zake mikoani. zoezi hili ambalo limefanyika  muda mfupi kabla ya magari  kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo,jijini Dar es Salaam, ni moja ya hatua ya Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka,.


Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Koplo Abdallah Bwasi akikagua moja ya magari  yanayofanya safari zake nje ya mkoa wa Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya magari  kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo,jijini Dar es Salaam.Hatua hii ya Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani imekuja kwa lengo la kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka.(Picha zote na Abubakari Akida, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

  Imeandaliwa na Kitengo Cha Mawasiliano ya  Serikali- Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mkuu wa Kitengo cha Elimu kwa Umma, Makao Makuu ya Trafiki, Dar es Salaam, ASP Abel Swai akitoa elimu ya usalama barabarani kwa abiria, muda mfupi kabla ya kuanza safari za mikoani katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo, jijini Dar es Salaam, elimu ambayo inalenga kudhibiti ajali za barabarani kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka,

No comments: