Thursday, November 19, 2015

JUKATA WATAKA KAZI TU SASA IWE KATIBA TU,WAMTAKA RAIS MAGUFULI KUANZA NA KATIBA MPYA

Mwenyekiti wa Jukwaa la katiba nchini Tanzania JUKATA akizungumza na wanahabari kuhusu maswala kadhaa kuhusu katiba mpya Tanzania ambapo wamemshauri Rais wa Tanzania DR MAGUFULI kuhakikisha kuwa mchakato wa katiba mpya unaanza upya ili uweze kutoa nafasi ya ya kupata nafasi ya kupata katiba iliyotokana na maoni ya wananchi.
Na Exaud Msaka Habari
Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA wamemtaka Rais mpya wa Tanzania Mh DR JOHN POMBE MAGUFULI  kuhakikisha kuwa kasi yake na kauli mbiu yake ya HAPA KAZI TU ianzie katika mchakato wa kupata katiba mpya ambapo wamemtaka kuhakikisha kuwa anaanza upya mchakato wa kupata katiba mpya na kupata katiba ambayo imepatikana kutokana na maoni wananchi wa Tanzania.

Akizungumza na wanahabri mapema leo jijini Dar es salaam mwenyekiti wa Jukwaa la katiba nchini Tanzania JUKATA DEUC KIBAMBA amesema kuwa ili Rais mpya aweze kukamilisha adhma yeka  na ya watanzania wengi ya kuleta mabadiliko na mageuzi katika mfumo wa kiuongozi wa Tanzania ni lazima ahakikishe kuwa mchakato wa katiba mpya ambayo ndiyo pekee inayoweza kubadilisha mfumo wa Tanzania.

Amesema kuwa mpango alioanza nao Mh MAGUFULI  wa  kufanya ziara za kushtukiza pekee haitoshi kuleta mabadiliko ya kiutendaji nchini Tanzania bali mabadiliko ya kweli yatatokana na utendaji uliobadilika wa mfumo mzima wa serikali ambao utaletwa na katiba inayojali maoni ya wananchi.
Bwana DEUS KIBAMBA amesema JUKATA wanamtaka Rais wa Tanzanaia DR MAGUFULI baada ya kuzindua bunge na kupata mawaziri wake ahakikishe kuwa kwanza analitangazia Taifa Rasmi namna ya kurejea mchakato wa kupata katiba mpya,serikali ipeleke bungeni miswada ya mabadiliko ya serikali zinazosimamia mchakato wa katiba,kurejea makubaliano ya Dodoma ambayo yalitaka pia kupanua wigo wa wadau wahusika katika mchakato wa kupata katiba ikiwemo pia nyama vya wafanyakazi,ambapo amesema kuwa kama rais atafanya hayo anaweza kushinda mtihani wa serikali yake kuaminika na watanzania walio wengi.


Katika hatua nyingine jukwaa la katiba nchini Tanzania JUKATA wamemtaka Rais wa Tanzania DR MAGUFULI aweze kuongoza jitihada za kuinusuru Zanzibar kutumbukia kwenye mkwamo au machafuko ya kisiasa hali ya sintofahamu iliyojitokeza baada ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kutambua kuwa hatua ya umoja wa serikali ya kitaifa iliyokuwa imeshafikiwa na wanzanzibar inapaswa kulindwa na kuheshimiwa.


Bwana KIBAMBA amesema kuwa kwa mujibu wa waangalizi wa JUKATA waliokuwa wakiangalia uchaguzi wa Zanzibar wameonyesha kuwa uchaguzi huo wa zanzibar ulifanyika na kumalizika kwa amani na hakukuwa na dosari kubwa zilizokuwa zinaweza kuwafanya uchaguzi huo kuahirishwa hivyo wameshangazwa sana hatua ya mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar Kufuta uchaguzi huo.

No comments: