Wednesday, November 18, 2015

Tigo yatoa zaidi ya Sh 200 milioni kudhamini Kilimanjaro Marathon msimu wa 2016.

   Meneja Mawasiliano ya Umma wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, John Wanyancha akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika hafla ya kuzindua msimu mpya wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2016, ambapo Tigo wametoa zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya mbio hizo.  Hafla hiyo imefanyika leo asubuhi jijini Dar es Salaam.

Wadhamini wa mbio za Marathon msimu wa 2016 wakiwa katika picha ya pamoja.

Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi msaidizi wa Michezo tokaWizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Alex Nkenyenge akizungumza na wageni waalikwa pamoja na wanahabari. Kushoto kwake ni Meneja Mawasiliano ya Umma wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, John Wanyancha.

Wadhamini wa mbio za marathon msimu wa 2016, wakilipua baruti za makaratasi kuashiria kuzinduliwa kwa udhamini huo jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

  Wana habari wakiwa katika uchukuaji wa tukio hilo ili kuipasha jamii.

Wadau wa masuala ya riadha pamoja na wana habari mabalimbali wakifuatilia kwa karibu uzinduzi wa msimu wa mbio za marathoni za Kilimanjaro msimu wa 2016.

No comments: