Friday, November 20, 2015

VIDEO--Waangalizi wa TACCEO waliodakwa na Polisi kipindi cha uchaguzi Hatimaye Waanza kutoa Report zao,Hii ni ya kwanza kutoka kwao leo


Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa kuangalia chaguzi nchini Tanzania TACCEO Bw IZRAEL ILUNDE akizungumza na wanahabari wakati wakiwasilisha Report yao ya awali tangu kumalizika kwa uchaguzi wa Tanzania wakiwa kama waangalizi wa Ndani waliokuwa wakufwatilia uchaguzi huo
 Selikali imeaswa kushughulikia kesi za uchaguzi kwa wakati ili kuepusha wananchi kukosa haki yao ya msingi ya uwakilishi bungeni kwa wakati huo ambao watakuwa hawana uwakilishi ndani ya chombo hicho cha wananchi.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mwenyekiti wa (TACCEO)  BW ISRAEL ILUNDE wakati alipokuwa akitoa Ripoti ya awali ya  uchaguzi wa mwaka huu uliofanyika octaber 25 mwaka huu.report ambayo imekluja huku kukiwa bado kuna sintiofahamu ya vifaa kadhaa vya waangalizi hao vikiwa bado vimeshikiliwa na jeshi la polisi kwa kile kilichoitwa kukiuka sheria mbalimbali za uangalizi wa uchaguzi wa ndani.
Mmoja wa Waratibu wa mtandao huo HAMIS MKINDI akifafanua jambo katika Mkutano huo


 Bwana Ilunde ameeleza kuwa uangalizi wao umebaini kutotekeleza majukumu kwa wakati kulikokuwa kunafanywa na tume ya Taifa ya uchaguzi akitolea mfano kitendo cha kuchelewesha vifaa vya kupigia kura katika maeneo mbalimbali na baadhi ya maeneo kushindwa kufanya uchaguzi kutokana na kukosekana kwa vifaa kwa wakati jambo ambalo wamesema kuwa lilitokea katika maeneo kadhaa hapa nchini.

Aidha Ilunde alisema kwa miaka mingi kunakuwaga na ucheleweshaji wa kesi za uchaguzi jambo linalopelekeaga wananchi wa eneo husika kukosa uwakilishi na hatimaye jimbo lao kutofanya maendeleo
Kaimu Mkurugenzi wa LHRC ambao ndio waratibu wa TACCEO akizungumza katika mkutano huo
Kwa upande wake Mratibu wa mtandao huo Bw HAMIS MKINDI amesema kuwa tume ya taifa ya uchaguzi lazima iwe inachukulia changamoto zinazojitokeza kwenye uchaguzi husika kama somo kwa uchaguzi mwingne kwani zipi changamoto nyingi ambazo zilijitokeza.


Sambamba na hilo BW MKINDI amevishauri vyombo vya dola kusimamia haki ili Taifa liweze kuongozwa kwa misingi ya uwazi,haki na uadilifu
Wanahabari wakipata habari
Aidha wakizungumzia kizungumkuti kilichochojitokeza visiwani zanzibar, waangalizi hao wametangaza kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na haki lakini wanashangazwa na tume ya uchaguzi ZEC kushindwa kumtanga mshindi mpaka sasa.

Kaimu mkutugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC ambao ndio waratibu wa mtandao huo wa TACCEO Bi EMELDA LULU URIO alisema waangalizi wao wote walionyesha kuwa uchaguzi wa Zanzibar haukuwa na dosari yoyote hivyo ni matarajio yao ZEC itamtangza mshindi na siyo zoezi la kurudia kupiga kura.

No comments: