Saturday, December 12, 2015

MHE. ANJELA KAIRUKI AANZA KAZI RASMI OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA

ang2
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb) akiweka saini katika kitabu cha wageni baada ya kuwasili rasmi katika ofisi yake leo Jumamosi.
ang3
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora Bw. Tixon Nzunda (aliyesimama) akimkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (wa kwanza kutoka kulia) kuongea na watendaji wa ofisi yake baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

ang4
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb) (kulia) akizungumza na watendaji wa Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora mara baada kufika ofisini kwake kuanza kazi leo Jumamosi.
anj1
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb) (wa pili kutoka kushoto) akiwasili ofisini na kulakiwa na watendaji wa ofisi yake mara baada ya kuapishwa. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Bw. Tixon Nzunda.
…………………………………………………………………………….
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (MB) ameanza kazi rasmi Leo Jumamosi Desemba 12/2015 mara baada ya kuapishwa Ikulu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  John Pombe Magufuli.
Mhe. Kairuki akiongea na watendaji wa Wizara yake alielekeza masuala ya kiutumishi ikiwamo  kusimamia nidhamu ya kazi ni jambo la msingi  hivyo kutumia daftari la mahudhurio  peke yake haitoshi.
“Tutumie Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kubaini Watumishi wanaoiba muda wa kazi wa Serikali” Mhe. Kairuki alisisitiza na kusema kazi lazima zitekelezwe  kwa kiwango cha juu.
Mhe. Waziri Kairuki alisema suala la kufanya kazi kwa kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali ni muhimu kwa kuwaelekeza watendaji wa Wizara yake kushirikiana na Wakala ya Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kubaini taarifa za watumishi wanaofariki ili wafutwe katika orodha ya malipo.
Mhe. Waziri Kairuki alisema ushirikiano katika kazi ni jambo la msingi ili kushauriana katika kutatua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa masuala mbalimbali ya kiutumishi na kuondoa malalamiko.
Awali, Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Bw. Tixon Nzunda akimkaribisha Mh. Waziri Kairuki kuongea na watendaji wa Wizara alisema waajiri wote nchini walishaelekezwa kufanya kazi ya kusafisha takwimu zisizohitaji katika Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara Serikalini (HCMIS).
Bw. Nzunda alisema Watumishi wote wenye takwimu chafu (takwimu zisizohitajika) katika mfumo wa HCMIS watafutwa baada ya kukamilika kwa zoezi hilo ifikapo mwisho wa mwezi Desemba 2015 na endapo kutakua na mwajiri atakayekua na takwimu chafu atawajibika kwa kushindwa kutekeleza agizo hilo.

No comments: