Thursday, December 31, 2015

NAIBU WAZIRI WA HABARI,UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO, ANNASTAZIA WAMBURA ATEMBELEA TCRA LEO JIJINI DAR.

Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura akipewa maelekezo na Naibu Mkurugenzi wa maswala ya utangazaji wa Televisheni wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Frederick Ntobi mara baada ya kutembelea chumba cha maswala ya mawasiliano hasa ya Televisheni  leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Mkurugenzi wa maswala ya Posta wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Haruni Lemanya akizungumza na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Annastazia Wambura pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) leo jijini Dar es Salaa mara baada ya Naibu waziri kutembelea katika ofisi ya Maswala ya Posta katika Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

Wednesday, December 30, 2015

SALAMU ZA MWAKA ZA RAIS WA TFF KWA WADAU WA MPIRA WA MIGUU TANZANIA


Ndugu zangu, Kwa niaba ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania kupitia kwenu wanahabari ninaomba nitoe salam za mwaka za Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF.

Ligi Kuu ya Zanzibar KVZ na JKU Mchezo uliofanyika Uwanja wa Amaan Timu ya JKU Imeshinda 2--0

Wachezaji wa Timu ya JKU wakisalimiana na Wachezaji wa Timu ya KVZ kabla ya kuaza mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya JKU imeshinda 2--0.
Mchezo uliochezwa jioni mabao ya JKU yamefungwa katika kipindi cha kwanza na katika dakika ya 8 mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande ameipatia bao timu yake katika dakika ya nane ya mchezo huo kipindi cha kwanza na Bao la ushindi la JKU limepatikana katika kipindi hicho cha kwanza katika dakika ya 35 ya mchezo huo lililofungwa na mshambuliaji wake Nassor  Mattar.
Kocha Mkuu wa Timu ya KVZ King akifuatilia mchezo huo wakati timu yake ikiwa nyuma kwa mabao 2--0 
Beki wa timu ya KVZ Juma Abdalla, akijiandaa kumzuiya mshambuliaji wa Timu ya JKU mwenye mpira Nassorv Mattar, wakati wa mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 
Mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande(kulia) akimpita beki wa Timu ya KVZ Emill Wiliam  

Mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande, akimiliki mpira huku beki wa timu ya KVZ Emill William akijiandaa kumzuiya.  
Mshambuliaji wa Timu ya JKU Mohammed Abdalla akimpiga chenga golikipa wa timu ya KVZ Yakub Bakari. hatimai mpira huo na kutoka nje ya uwanja. 

Mshambuliaji wa Timu ya KVZ Masoud Abdalla mwenye jezi ya kijani akimpita mchezaji wa timu ya JKU  Mbarouk Chande. 
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot
Zanzinews.com.

SPIKA WA BUNGE, JOB NDUGAI AMEREJEA LEO KUTOKA INDIA

 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akilakiwa na Naibu Spika wa Bunge Mhe. Tulia Ackson mara baada ya kuwasili katika uwanja Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere jijini Dar es salaam akitokea Nchini India alikokuwa kwa ajili ya matibabu.

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo ampongeza Mbwana Samatta kwa kujiunga na klabu ya Genk ya Ubelgiji

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye(kushoto) akiongea na Mchezaji wa Timu ya TP Mazembe Mbwana Samatta(kulia) leo jijini Dar es salaam.Mbwana amemtembelea waziri Nape ofisini kwake na kuomba baraka za wizara katika kinyanganyiro cha kugombea uchezaji bora wa afrika anayechezea ligi za ndani na pia kumpa habari njema za yeye kutegemea kujiunga na timu ya Ubelgiji ya Genk.
Waziri wa Habari,Utamaduni,sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye(katikati)akiongea na waandishi wa Habari na kuwaomba watanzania kumwombea Mbwana Samatta ili ashinde katika kinyanganyiro cha kugombea uchezaji bora wa afrika anayechezea ligi za ndani kwani ni jambo la Taifa zima.Mhe Nape pia alimhakikishia kuwa Serikali ipo nyuma yake na ipo katika mkakati wa kuifanya michezo kuwa Shughuli Rasmi kwani itawafaidisha wanamichezo na Serikali kwa kupata kodi. 
Mchezaji wa TP Mazembe Mbwana Samatta(wa kwanza kushoto)akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) sababu za yeye kumtembelea Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo katika ofisi ya Wizara hiyo.Mbwana alisema kuwa amemtembelea waziri uyo kwa ajili ya kumfahamisha kuwa yumo katika kinyanganyiro cha kugombea uchezaji bora wa afrika anayechezea ligi za ndani na hivyo kuomba baraka za Wizara.Pia kumpongeza Mhe. Nape kwa kuchaguliwa kuwa waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo.Mbwana anategemea kujiunga na klabu ya Mpira ya Genk ya Ubelgiji kwa mkataba wa miaka minne.
Picha na Daudi Manongi-WHUSM.

JK,WAZIRI LWENGE WAKAGUA MITAMBO YA MAJI WAMI,CHALINZE

Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete (katikati), akizungumza na Waziri wa Maji, Gerson Lwenge wakielekea kukagua mitambo ya kusafisha na kusafirisha maji Wami, katika Halmashauri ya Mji wa Chalinze, mkoani Pwani leo.

RAIS MAGUFULI ATANGAZA MAKATIBU WAKUU NA MANAIBU KATIBU WAKUU WAPYA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

GUL1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitangaza Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, na kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue wakisikiliza kwa makini.

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFUNGUA MAFUNZO YA AWALI KWA WATUMISHI WA IDARA YA WAKIMBIZI, LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Washiriki wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani), wakati alipofungua mafunzo hayo katika ukumbi wa mikutano wizarani hapo,jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa  Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa, akizungumza na washiriki wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi(hawapo pichani),kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Utawala na Usimamizi wa Idara ya Wakimbizi, Deusdedit Masusu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akizungumza  na washiriki  wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi(hawapo pichani),wakati alipofungua mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wapya, katika ukumbi wa mikutano wizarani hapo,jijini Dar es Salaam.Kulia ni  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Numbilya Mpolo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(watatu kutoka kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, muda mfupi baada ya kufungua mafunzo hayo katika ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam wanne kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa  Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa na wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Numbilya Mpolo .(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,MOHA)

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil akizungumza  na washiriki  wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi wakati alipofungua mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wapya, katika ukumbi wa mikutano wa wizara, jijini Dar es Salaam.Kulia ni  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Numbilya Mpolo, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa  Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa .


Bresking Newzz--Mitandao ya Tigo,Smart,Airtel,Halotel,Na Zantel wapigwa kitanzi na TCRA,waamuriwa kulipa Faini Ya mamilioni,chanzo hiki hapa


HATUA ZA KISHERIA NA KIUDHIBITI KWA MAKAMPUNI YA SIMU YALIYOSHINDWA KULINDA WATEJA WAKE KITEKNOLOJIA NA KISHERIA KUHAKIKISHA USALAMA WA MAWASILIANO YAO

Tamko la ACT – WAZALENDO kuhusiana na utaratibu wa kutunza na kuzalisha taka:


Chama cha ACT – WAZALENDO kinafuatilia kwa karibu hatua zinazochukuliwa na serikali katika maeneo mbalimbali kama njia ya kuleta suluhu ya kudumu katika suala zima la utunzaji mazingira na hasa suala la usafi na utunzaji,usimamizi na uzalishaji wa taka ili kuimarisha mfumo wa taka kisera na kisheria.



Tuesday, December 29, 2015

Ligi Kuu ya Zanzibar Mafunzo na KMKM Timu Hizo Zimetoka Sare ya Bao 1--1

 Mshambuliaji wa timu ya Mafunzo akijiandaa kupiga mpira huku beki wa timu ya KMKM akiwa tayari kumzuiya wakati wa mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar timu hizo zimetoka sare ya bao 1--1.
 Beki wa Timu ya Mafunzo akiondoa mpira golini kwao, 
 Mshambuliajhi wa Timu ya KMKM na Beki wa Timu ya Mafunzo wakiwania mpira.

NAIBU WAZIRI MH. ANASTAZIA WAMBURA ATEMBELEA IDARA YA HABARI MAELEZO

it1
Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura katikati akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Assah Mwambene wa kwanza kulia ya jinsi ya kutunza picha za matukio mbalimbali wakati alipofanya ziara Idarani hapo leo, kushoto ni Afisa Habari Mkuu Anna Itenda.(picha na Benjamini Sawe-WHSUM).

MAGHEMBE AKABIDHIWA RASMI OFISI LEO NA ALIYEKUWA WAZIRI WA WIZARA HIYO LAZARO NYALANDU

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto) akikabidhiwa taarifa ya makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Lazaro Nyalandu (wa pili kulia) leo tarehe 29 Desemba 2015 ofisini kwake Mpingo House. Wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Adelhelm Meru (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Ndugu Selestine Gesimba (kulia).

VIONGOZI WAPYA WA TAHLISO WAAPISHWA RASMI,WAUNGANA NA KASI YA MAGUFULI

Mwenyikiti mpya wa shirikisho la wanafunzi wa elimu ya juu nchini Tanzania TAHLISO Ndugu STANSLAUS PETER akila kiapo kulitumikia shirikisho hilo mbele ya mwanasheria HAMZA JABIRI leo Jijini Dar es salaam kuanza kazi rasmi ya kuwatumikia wanafunzi wa elimu ya juu nchini Tanzania
 Na Exaud Mtei (msaka habari) wa Habari24 blog

Uongozi mpya wa shirikisho la elimu ya vyuo vikuu nchini Tanzania TAHLISO umesema kuwa upo tayari kumuunga mkono Rais wa Tanzania Dr John pombe magufuli kwa kasi aliyoanza nayo na kuhakikisha kuwa elimu ya Tanzania hasa elimu ya vyuo vikuu inakuwa ya ubora unaofaa na inaheshimika nchini Tanzania.
Makamu Mwenyekiti  mpya wa TAHLISO  Ndugu JUMA ALLY OMARI akila kiapo leo jijini Dar es salaam
Akizungumza na wanahabari mapema leo jijini Dar es salaam katika hafla fupi ya kuwasimika viongozi wa shirikisho hilo wapya mwenyekiti mpya wa TAHLISO Tanzania Bw STANSLAUS PETER amesema kuwa kwa miaka mingi elimu ya juu nchini Tanzania imekuwa haina ubora unaotakiwa ikiwa ni pamoja na mitaala mibovu,ukosefu wa mokopo kwa wanafunzi wengi jambo linalowakatisha tamaa wengi kusoma,ambapo amesema uongozi wake umeona kasi nzuri ya serikali ya awamu ya tano na wapo tayari kushirikiana na serikali kutatua changamoto za wanafunzi nchini.
Naibu katibu mkuu wa TAHLISO KHAMIS ELLY akiapa leo Jijini Dar es salaam
Mwenyekiti huyo amesema kuwa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa mwaka huu umeonyesha kuwa serikali ya Magufuli inawajali wanafunzi kwani asilimia kubwa ya wanafunzi walipata mikopo na wengine wanaendelea kupata mikopo huku akiwataka wanafunzi kutulia kwani neema kwao inakuja kutokana na kasi ya uongozi huo mpya pamoja na ule wa serikali ya awamu ya tano.
Katibu mkuu Mtendaji mpya wa Shirikisho hilo SAGOLE WAMBURA akiapa leo

Viongozi wa TAHLISO wameapishwa leo rasmi Jijini Dar es salaam baada ya uchaguzi wa Kidemocrasia uliofanyika tarehe 23 mwezi huu na wataiongoza Taasisi hiyo kwa mwaka mmoja kwa mujibu wa katiba yao.

Afya ya Uti wa Mgongo ni Afya ya Mgongo - Dk. Yash Gulati, Apollo Hospital





Dr Yash Gulati, Senior Spine and Joint Replacement Surgeon at Apollo Hospitals; Delhi

Tigo Pesa Yatowa Elimu kwa Mawakala Wao Zenj

Mkurugenzi  wa Tigo Pesa Tito Magesho akizungumza na mawakala wa Tigo Pesa walioko Zanzibar wakati wa mkutano wa kuwakutanisha mawakala wa Zanzibar jinsi ya  kuendesha huduma hiyo kwa wateja wao mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa skuli ya sekondari ya ben bella Zanzibar
Mawakala wa Tigo Pesa Zanzibar wakipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Maofisa wa Tigo Pesa baada ya mkutano wao wa kutowa elimu ya uliofanyika katika viwanja vya Skuli ya BenBella Zenj.
Msimamizi wa Tigo Pesa Kanada ya Zanzibar Mubaraka akibadilishama mawazo na Mkurugenzi  wa Tigo Pesa Tito Magesho, baada ya mkutano wao na Mawakala wa Tigo Pesa Zanzibar uliofanyika katika viwanja vya Skuli ya Sekondari Ben Bella Zanzibar. 

Mkurugenzi  wa Tigo Pesa Tito Magesho akizungumza na mawakala wa Tigo Pesa walioko Zanzibar wakati wa mkutano wa kuwakutanisha mawakala wa Zanzibar jinsi ya  kuendesha huduma hiyo kwa wateja wao mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa skuli ya sekondari ya ben bella Zanzibar
Mkurugenzi  wa Tigo Pesa Tito Magesho akizungumza na 
mawakala wa Tigo Pesa walioko Zanzibar wakati wa mkutano wa kuwakutanisha mawakala wa Zanzibar jinsi ya  kuendesha huduma hiyo kwa wateja wao mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa skuli ya sekondari ya ben bella Zanzibar
Afisa wa Tigo Pesa Kanda ya Zanzibar Mbaraka akizungumza na Mawakala wa Tigo Pesa Zanzibar wakati wa mkutano na Mawakala hao uliofanyika katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari ya Ben Bella Zanzibar 
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot 
Zanzonews.com.

Monday, December 28, 2015

Kuhusu Ajali ya Msafara wa waziri Muhongo Leo soma hapa

mug1
Msafara wa Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo umepata ajali baada ya magari mawili kuacha njia katika Kijiji cha Kagorogoro Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera.

Hata hivyo Afisa habari wa wizara hiyo Bi. Asteria Muhozya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema katika ajali hiyo hakuna majeruhi na walifanikiwa kubadilisha matairi yaliyokuwa yamepasuka kutokana na msukosuko wa kuacha njia  na kuendelea na safari,  Msafara huo ulikuwa unatoka mpaka wa Murongo karibu na nchi jirani ya Uganda.

WAZIRI WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII PROF. JUMANNE MAGHEMBE AWASILI MAKAO MAKUU YA WIZARA HIYO MPINGO HOUSE MARA BAADA YA KUAPISHWA IKULU LEO

Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (mbele kulia) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Selestine Gesimba wakati wa mapokezi yake leo tarehe 28 Desemba 2015 katika ofisi yake mpya Mpingo House mara baada ya kuapishwa Ikulu mapema asubuhi ya leo. Nyuma yake kulia ni naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Eng. Ramo Makani na anaeongoza utambulisho katikati yao ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Adelhelm Meru.

RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI IKULU LEO

2
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akimuapisha Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mh. Profesa Makame Mbarawa Ikulu, ambapo amewapisha mawaziri watano kujaza nafasi za mawaziri zilizokuwa wazi katika wizara kadhaa za serikali ya awamu ya tano, Hafla ya kuwaapisha mawaziri hao imefanyika leo asubuhi.

TIGO YAFIKIA WAFUASI MILIONI MOJA KATIKA MTANDAO WA FACEBOOK



Kampuni ya Tigo Tanzania hivi karibuni imetanga za kufikisha wafuasi milioni moja katika mtandao wao wa Facebook. Katika ukarasa wake wa Facebook, www.facebook.com/TigoTanzania kampuni ilifikisha mfuasi wa milioni  moja Jumapili Desemba 27 mwaka huu hapa Tanzania.

Kutokana na ongezeko la matumizi ya mtandao wa kijamii wa Facebook hapan chini, Facebook imekuwa mstari wa mbele  katika matumizi kutoka na uzinduzi wa Facebook katika lugha ya Kiswahili uliofanyika mwaka wa 2014 kwa ushirikiano wa Tigo Tanzania na Facebook, ambapo wateja wanaweza kutumia Facebook kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza kupitia simu zao za mkononi bila malipo yoyote ya ziada.

 Ukurasa wa Facebook wa Tigo uliundwa Juni 2011 na umekuwa jukwaa madhubuti wa kurambaza na wateja wake wapendwa ambapo wanajifunza kuhusu huduma na bidhaa mpya za kampuni.

Hivi karibuni, Tigo Tanzania imejishindia tuzo mbili katika Tuzo za Uongozi Bora (Tanzania Leadership Awards) ambayo inatambua mashirika na watu binafsi katika uongozi. Tuzo hizo ni ya Ubora wa bidhaa (The Hall of Fame in Brand Excellence), na Matumizi Bora ya Mitandao ya Kijamii Katika Mauzo( Best use of Social Media in Marketing).

Tigo Tanzania inaongoza katika soko la mawasiliano na imekuwa mstari wambele katika mitandao ya kijamii ambapo wateja wamekuwa wakiuliza maswali na kujibiwa haraka. Hii imeufanya mtandao kuaminika sana na wateja na kutumika kama mwendelezo wa huduma kwa wateja.
Kuhusu Facebook Mkurugenzi wa Tigo Bwana Diego Gutierrez anasema. “Jukwaa letu la Facebook na Twitter (Tigo TZ) limekuwa kitendea kazi muhimu ambacho kinatumika kujifunza kutoka  kwa wateja wetu na jamii kwa jumla ambao wanakitumia.
Tunajivunia kwa kuweza kuyafikia mafanikio haya, na tunawashukuru wateja wetu kwa kuwa naimani nasi.

Tigo, imedhamiria kubadilisha mtindo wa maisha wakidijitali kwa kuwa letea wateja wetu ubunifu wa teknolojia maridha wa. Hivi karibuni, tumezindua teknolojia ya 4G LTE hapa Tanzania ambayo ni intaneti iliyona kasi kuliko zote pamoja na ofa ya aina ya simu yaTechno Y3 Smartphone inayotumia lugha ya Kiswahili.

Waraghabishi wakoleza kasi ya mabadiliko wilayani Kishapu

Watendaji wa Kituo cha Maendeleo cha Jamii ya Uchunga wilayani Kishapu  wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi mbele ya jengo la kituo hicho likiwa limekamilika kutokana na michango yao ya fedha na nguvu kazi. 

KAMPUNI YA TIGO YATOA MISAADA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA MUGEZA MSETO MANISPAA YA BUKOBA

Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akikabidhi misaada
mbalimbali Mwenyekiti wa kamati ya shule ya kulelea watoto Yatima cha Mugeza
Mseto Manispaa ya Bukoba Bi. Evelyne Mwijage juzi. Kampuni ya Tigo ilitoa
misaada kwenye kituo hicho
Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akikabidhi misaada
mbalimbali Mwenyekiti wa kamati ya shule ya kulelea watoto Yatima cha Mugeza
Mseto Manispaa ya Bukoba Bi. Evelyne Mwijage juzi. Kampuni ya Tigo ilitoa
misaada kwenye kituo hicho
Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akiongea na
wanahabari,viongozi  na watoto wa kituo
cha kulelea watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba.
Meneja wa Mauzo Mkoa wa Kagera, Sadoki Phares akiongea na wanahabari,
viongozi na  watoto wa kituo cha kulelea
watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba.
Meneja wa
Huduma kwa Wateja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Beatrice Kinabo(kushoto) na Meneja wa
Duka la Tigo Bukuba, Lilian Mwise (aliyebeba mtoto).
 
Watoto wa Kituo cha kulelea watoto cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba
wakifuatilia kwa makini.
Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akitembea na watoto wa
kituo cha Mugeza mara baada ya kukabidhi misaada.
A
Watoto wa Kituo
cha kulelea watoto cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba wakifuatilia kwa makini.