Wednesday, January 13, 2016

Mbunge NASSARI aingia sokoni china mwenyewe kutafuta vitanda vya wananchi wake

Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ,Joshua Nassari akiwa katika moja ya karakana ya kutengeneza vifaa tiba katika mji wa Guangzhou nchini China.
Mheshimiwa Nassari akifanya mazungumzo na wahusika wa karakana hiyo kuona namna ya kuapata vifaa hivyo kwa ajili ya kusidia katika Hosptali ya wilaya ya Arumeru na vituo vya afya.
Mh Nassari akiwa amelala kwenye moja ya vitanda vya wagonjwa alivyokuta katika karakana hiyo.
Mh ,Nassari akipita katika karakana hiyo . 
Mh Nassari akifanya mazungumzo na wahusika wa karakana hiyo ambako anatarajia kutumia fedha za mkopo wa gari la Ubunge kwa ajili ya kununua vitanda 200 ,viti vya magaurudumu pamoja na kabati ndogo za kuhifadhia dawa pamoja na vifaa vidogo vya matibabu.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kskazini.

No comments: