Thursday, January 14, 2016

STARTIMES RAUNDI YA 11 KUENDELEA WIKIENDI


Ligi Daraja la Kwanza (StarTimes League) inaendelea wikiendi hii kwa michezo 12 kuchezwa katika viwanja mbalimbali, huku timu 3 za juu kutoka katika kila kundi zikipata nafasi ya kupanda Ligi Kuu msimu ujao moja moja.


Kundi A, Jumamosi Mji Mkuu watawakabili Africa Lyon uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, KMC dhidi ya Kiluvya uwanja wa Mabatini Mlandizi, Polisi Dodoma watacheza dhidi ya Friends Rangers uwanja wa  Mgambo Mpwapwa, huku Jumapili Polisi Dar wakiwakaribisha Ashanti uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.
Kundi B, Njombe Mji watakua wenyeji wa Kimondo uwanja wa Amani Njombe, Lipuli FC dhidi ya Kurugenzi uwanja wa Wambi – Mafinga, uwanaj wa Majimaji mjini Songea JKT Mlale watakua wenyeji wa Polisi Morogoro, huku Jumapili kukichezwa mchezo mmoja Ruvu Shooting dhidi ya Burkinafaso uwanja wa Mabatini, Mlandizi.
Kundi C, Rhino Rangers watawakaribisha JKT Kanembwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora, Panone FC dhidi ya Geita Gold uwanja wa Ushirika mjini Moshi, uwanja wa Karume Musoma, wenyeji Polisi Mara watacheza dhidi ya Polisi Tabora, huku siku ya Jumapili Mbao FC wakiwakaribisha JKT Oljoro uwanja wa CCM Kirumba.

No comments: