Thursday, January 14, 2016

VODACOM MZUNGUKO WA 14


Baada ya kusimama kwa wiki mbili kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania mzunguko wa kumi na nne (14) unatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo 8 kuchezwa katika viwanja mbalimbali, huku timu 16 zikichuana kusaka pointi 3 muhimu.


Jumamosi uwanja wa Karume jijini Dar es salaam, Maafande wa JKT Ruvu watawakaribisha Maafande wa Mgambo Shooting, Toto Africans watawakaribisha Tanzania Prisosns uwanja wa CCM Kirumba, huku Stand United wakicheza dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa Kamabarage mjini Shinyanga.
Uwanja wa Tafa jijini Dar es salaam, Simba SC watawakaribisha wakata miwa wa Mtibwa Sugar saa 10 jioni, Mbeya City watakua wenyeji wa Mwadui FC uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Coastal Union dhidi ya Majimaji uwanja wa Mkwakwani, huku mchezo kati ya Azam FC dhidi ya African Sports ukianza saa 1 usiku.
Jumapili ligi hiyo itaendelea kwa mchezo mmoja uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, ambapo Young African watawakaribisha Ndanda FC kutoka Mtwara.


No comments: