Thursday, February 11, 2016

Elimu bure yaweka Record,Idadi ya wanafunzi walioandikishwa darasa la kwanza Dar iko hapa.Mkuu wa mkoa aomba msaada wa wananchi kuchagngia madawati

 Mkuu wa mkoa wa Dar es samaa SAID MECK SADIC amewataka waanchi na wadau mbalimbali kuungfa mkono hatua iliyochukuliwa na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na DR JOHN POMBE MAGUFULI katika kusimamia maendeleo ya elimu na kuhakikisha inatekeleza ipasavyo wanafunzi wapate elimu.

Ameyasema hayo leo Jijini Dar es aalaam wakati wa mkutano na wakazi pamoja na wazazi wanafunzi walioandikishwa kwa ajili ya Darassa la kwanza katika shule ya msingi maji matitu ambayo zaidi ya wananfuzi 8276 wameandikishwa kwa mkoa wa Dar es salaam kujiunga na darasa la kwanza mwaka huu.
Akizngungumza na wananchu hao mkuu huyo wa mkoa wa Dar es salaamamesema kuwa sera ya Rais ya elimu bure imepokelewa kwa uzito kubwa na wananchi wameandikisha watoto wao kwa wingi na kuvuka makadirio kwa zaidi ya asilimia iliyokusudiwa hivyo jamii inatakiwa kuunga mkono jitihada hizo  kwa kuchangia madawati kwa ajili ya kuleta uboreshaji zaidi katika elimu hiyo.


Aidha amesema kuwa serikali kupitia mkoa amnaoungoza imepanga kuelekeza zaidi ya Billion 4 katika elimu baada ya kupunguza fedha katika matumizi yasoyo ya lazima ikiwa ni njia ya serikali ya kubana matumizi.

Naye mstahiki meya wa manispaa ya Temeke ABDALA CHAUREMBO akizungumza katika mkutano huo ameahidi kuwa halmashauri yake imedhamiria kuanza utekelezaji wa agizo kwa ujenzi wa shule mpya na kuongeza madarasa pamoja na kutatua changamoto mbalimbali za kielemu katika eneo lake,
Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa wa Temeke SOPHIA MJEMA amepongeza sera ya Rais ya elimu bure kwa kuwa amepanga kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapata elimu bora na yenye Tija kwa jamii 

No comments: