Tuesday, March 15, 2016

TAWLA YAWAKUTANISHA WADAU KUJADILI MATATIZO YA UZAZI NCHINI TANZANIA

Mkurugenzi wa miradi kutoka ndani ya chama hicho   Bi NASUKI KISAMBU akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es salaam na kuwakutanisha wadau mbalimbali kujadili kwa pamoja juu ya maswala ya vufi vitokanavyo na uzazi pamoja na changamoto zake

Na Exaud Mtei(Msaka Habari)
 Chama cha wanawake wanasheria nchini Tanzania TAWLA kimeendesha majadiliano maalum jijini Dar es salaam pamoja na wadau mbalimbali kuhusu maswala ya vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi na changamoto mbalimbali zinazowakuta wanawake wakati wa uzanzi nchini Tanzania.

Mkutano huo ambao umeendeshwa Jijini Dar es salaam umewahusisha wadau mbalimbali wa maswala ya kijamii wakiwemo madaktari na wataalam wa maswala ya uzazi,viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani na wengine wa mitaa,wanasheria mbalimbali pamoja na wanahabari ambapo lengo likiwa ni kupanua uelewa zaidi juu ya afya ya uazazi na jinsi gani ya kupunguza Tatizo la vifo vya wanawake wakati wa uzazi nchini Tanzania.

Akizungumza na wadau huo wakati akifungua mkutano huo mkurugenzi wa miradi kutoka ndani ya chama hicho   Bi NASUKI KISAMBU amesema kuwa chama cha wanawake wanasheria TAWLA kinaendesha mradi maalum kwa ajili ya maswla ya matatizo ya uzazni nchini Tanzania mradi ambao unafadhiliwa na shirika la kimataifa la OXFARM kwa lengo la kusaidia kupunguza vifo nitokanavyo na uzanzi nchini Tanzania.

Amesema kuwa vifo vingi vyauzanzi wa wanawake nchini Tanzania vinatokana na na utoaji mimba usio salama ambao unapelekea kupoteza watanzania wengi kutokana na Tatizo hilo,huku wakiwataka wadau mbalimbali kuliona tatizo hilo kuwa na kubwa sana na waweze kupambana nalo kwani Linawagharimu watanzania walio wengi.



Ameongeza kuwa pia lengo na mkutano huo ni kujadili kwa pamoja haki za wanawake duniani huku wakiangalia pia sheria mbalimbali zinazowapa haki wanawake hasa katika swala la utoaji mimba na uzazi kama sheria ya nyongeza ya haki za wanawake ya MAPUTO PROTOCAL na sheria ya tanzania zinavyozungumza juu ya maswala hayo na utekelezaji wa hizo sheria.

No comments: