Na Exaud Mtei
Mtandao wa asasi za
kuangalia chaguzi nchini Tanzania TACCEO kwa kushirikiana na kituo cha sheria
na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC leo wamezindua rasmi report yao ya
uangalizi wa uchauzi wa mwaka 2015 uliofanyika nchini Tanzania huku report hiyo
ikieleza baadhi ya mambo mbalimbali ambayo yalikuwa kama Changmoto katika uchaguzi
huo.
Baada ya kuzinduliwa Rasmi wakionyesha Report Juu |
Report hiyo ambayo
imeelezea changamoto na mafanikio ya uchaguzi mkuu uliomalizika mwaka jana
imeelezea mambo yote kuanzia katika mchakato wa uadikishaji wa daftari la
kudumu la wapiga kura hadi kufikia hatua ya kupiga kura na mchakato wa utangazwaji
wa matokeo ya uchaguzi ambao ulimazika kwa Rais JOHN POME MAGUFULI kuchaguliwa
kuwa Rais mpya wa Tazania.
Afisa na mwanasheria kutoka katika mtandao huo wakili HAMIS MKINDI akielezea mambo kadhaa yaliyomo ndani ya Report hiyo leo Jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi huo |
Akifafanua kuhusu
report hiyo jijini Dar es salaam afisa kutoka katika mtandao huo wakili HAMIS
MKINDI amesema kuwa kumekuwa na changamoto kadhaa ambazo zimeanishwa katika report
hiyo ambazo serikali,tume ya uchaguzi,na wadau wote wanapaswa kuzisoma ili
kuzifanyia kazi kwa ajili ya maadalizi ya uchaguzi mkuu ujao.
Msajili wa vyama vya siasa akikabidhiwa copy yake na mwenyekiti wa TACCEO Bi Martia Kabisama |
Akizitaja baadhi ya
changamoto hizo amesema ni pamoja na kukosekana kwa elimu ya uraia kwa mpiga
kura kwa kiasi cha kutosha kwa katika maeneo mengi ya nchi ,ukosefu wa
rasilimali kwa tume ya uchaguzi jambo ambalo liliathiri kwa kiwango kikubwa
ufanisi wa tume hiyo,baadhi ya vyama kushindwa kushiriki kampeni za uchaguzi
kwa ukosefu wa fedha,pamoja na vyama hivyo kukosa nafasi katika vyombo vya
habari kama iliyokuwa inapatikana kwa vyama viwili vilivyokuwa vinasigana
vikali.
Wawakilishi kutoka katika vyama kadhaa vya siasa walioshiriki katika tukio hilo |
Ameongeza kuwa katika
report hiyo ambayo imeandaliwa na TACCEO kwa kushirikiana na LHRC ambao
walikuwa na waangalizi wasiopungua 2100 nchi nzima imeelezea pia maswala kadhaa
ambayo yalijitokeza kwa mara ya kwanza katika uchaguzi huo likiwemo la
ushindani mkubwa uliokuwepo baina ya vyama viwili vya CCM na muungano wa vyama vinne
vya upinzani vya UKAWA,ambao umeelezewa kuwa ni ushindani ambao haukuwahi kuonekana
tangu kuanza kwa democrasia nchini Tanzania.
Matukio mengine ambayo
yametajwa katika Report hiyo ambayo ni nadra kutokea nchini ni pamoja na aina
ya kampeni ambazo zilikuwa zikifanyika na vyama viwili vikuu vilivyokuwa
vinachuana vikali pamoja na hamasa kubwa iliyokuwa kwa wananchi juu ya uchaguzi
huo.
Akizungumza katika
haflka hiyo mgeni rasmi msajili wa vyama vya siaa nchini Tanzania Jaji Fransis
Mutungi Amesema kuwa pamoja na changamoto zilizotajwa na waangalizi hao lakini
pia yapo mambo mazuri yaliyofanywa na serikali hivyo wataitumia Rreport hiyo
kushugulikia changamoto hizo ili kuboresha kuelekea uchaugzu ujao.
Katika hafla hiyo
imehudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka vyama vya siasa
nchini,wadau wa maendeleo kutoa nchi Tofauti duniani pamoja na wangalizi wa
uchaguzi huo mkuu kutoka TACCEO.
No comments:
Post a Comment