Wednesday, April 6, 2016

MARAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI WA TANZANIA NA PAUL KAGAME WA RWANDA WAZINDUA RASMI DARAJA LA LUSUMO

lsm01
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Dk. John Pombe Magufuli ameanza rasmi ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Rwanda ambapo amepokelewa na mwenyeji wake Rais Mh. Paul Kagame wa Rwanda kwenye mpaka wa Rusumo ambapo viongozi hao wote kwa pamoja wamefanya tukio la Kuzindua daraja la Lusumo linalounganisha nchi za Rwanda na Tanzania na pia wamezindua kituo cha Forodha kilichopo upande wa Rwanda katika mpaka huo, kama wanavyoonekana wakikata Utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa daraja la Lusumo watatu kulia katika picha ni Mwakilishi wa benki ya ADBDkt. Tonia Kandiero,  kutoka kulia ni  Balozi wa Japan nchini Tanzania Masaharu Yoshiba na Waziri wa Ujenzi Tanzania Mh. Profesa Makame Mbarawa
lsm1
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Dk. John Pombe Magufuli  na mwenyeji wake Rais Mh. Paul Kagame wa Rwanda pamoja na viongozi wengine walioshiriki katika uzinduzi huo wakipiga makofi mara baada ya kulizindua rasmi, watatu kulia katika picha ni mwakilishi wa benki ya ADB Dkt. Tonia Kandiero,  kutoka kulia ni  Balozi wa Japan nchini Tanzania Masaharu Yoshiba na Waziri wa Ujenzi Tanzania Mh. Profesa Makame Mbarawa
lsm2
Daraja la Lusumo linalounganisha nchi za Tanzania na Rwanda linavyoonekana mara baada ya kuzinduliwa na marais hao leo.
lsm3
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Dk. John Pombe Magufuli  na mwenyeji wake Rais Mh. Paul Kagame wa Rwanda pamoja na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa kiuo cha Forodha katika mpaka wa Rwanda na Tanzania uliopo Lusumo katika picha kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mh. Agustine Mahiga na Mwakilishiwa benki ya ADB Dkt. Tonia Kandiero pamoja na balozi wa  Japan na viongozi mbalimbali waliohudhuria katika uzinduzi huo.
kagm
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Dk. John Pombe Magufuli  na mwenyeji wake  Rais Mh. Paul Kagame wa Rwanda pamoja na wake zao Mama Janet Magufuli na Mama Jeannette Kagame mabalozi, Mawaziri  wa nchi hizi mbili pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa kituo cha Forodha kilichopo Lusumo  mpakani mwa Tanzania na Rwanda
lsm4Jiwe lenye kibao linaloelezea uzinduzi huo na lenye majina ya viongozi wa nchi hizo mbili za Rwanda na Tanzania.

No comments: