Wednesday, May 11, 2016

CCM NA CHADEMA WAENDELEA KUNGANGANIANA KESI YA UBUNGE JIMBO LA NDANDA

 Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa ubunge jimbo la Ndanda wilaya ya Masasi,Mariam Kasembe (CCM)dhidi ya Mbunge wa jimbo hilo, Cecil Mwambe (Chadema) imeendelea  kusikulizwa leo baada ya kuahirishwa jana na Jaji  Winfrida Kosoro ambapo pia leo imepigwa tarehe hadi ijumaa ya wiki hii ambapo ndiyo mahakama itaamua kama mshtakiwa atakuwa na kesi ya kujibu.

...Kesi hiyo iliendelea kusikilizwa hapo jana na upande wa mdaiwa kutoa ushahidi baada ya mleta maombi kupeleka mashahidi wiki iliyopita ambapo wakili wa mjibu maombi, Tundu Lissu aliieleza mahakama kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa mpeleka maombi unapaswa kuangaliwa kwa makini kwasababu hakuna ushahidi wowote wa nyaraka.

 Pichani ni wananchi wa jimbo la ndanda wakiwa mahakama ya wilaya masasi kusikiliza kesi ya kupinga matkeo iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo MARIAM KASEMBE wa CCM  dhidi ya mbunge wa jimbo hilo CECIL MWAMBE wa CHADEMA 

No comments: