Monday, May 16, 2016

HOTUBA YA LEMA YAZUA HOFU BUNGENI,WASITISHA HADI JIONI

DOM1 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria na Katiba, Mhe. Najma Giga wakielekea Bungeni kwa ajili ya vikao vya asubuhi vya Bunge hilo leo 16 Mei, 2016 mjini Dodoma..   

Hotuba ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ya Msemaji Mkuu wa Wizara ya Mambo Ndani ya Nchi, Godbless Lema imezuiliwa kusomwa.

Imezuiliwa kusomwa mpaka kwanza kamati ya Kanuni ya Bunge iipitie hotuba hiyo kabla ya kusomwa bungeni ili kuangalia kama hotuba hiyo imekiuka kanuni za Bunge.---------
DOM2 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kulia) pamoja na Mbunge wa Viti Maalul CCM, Mhe. Halima Bulembo wakielekea Bungeni kwa jili ya vikao vya asubuhi vya Bunge hilo leo 16 Mei, 2016 mjini Dodoma.
DOM3 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Mhe. Profesa Joyce Ndalichako (kulia) pamoja na Naibu Waziri, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Mhandisi Edwin Amandus Ngonyani wakielekea Bungeni kwa ajili ya vikao vya asubuhi vya Bunge hilo leo 16 Mei, 2016 mjini Dodoma.
DOM4 
Baadhi ya Viongozi wa Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji na Zimamoto wakiingia ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya vikao vya bunge hususan kusikiliza Bajeti ya Wizara ya Mambo y Ndani ya Nchi 16 Mei, 2016 mjini Dodoma.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO, DODOMA.

No comments: