Tuesday, May 17, 2016

MAENEO YA JIJI LA DAR ES SALAAM NA BAGAMOYO KUKOSA MAJI KWA SAA 10

 
TAARIFA
KWA UMMA
   17/5/2016
KUZIMWA
KWA MTAMBO WA RUVU CHINI
Shirika
la Maji Safi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO),
linawatangazia  wakazi wa jiji la
Dar-es-salaam  pamoja na  Mji wa Bagamoyo kuwa Mtambo wa kuzalisha Maji
wa Ruvu Chini utazimwa kwa wastani wa Saa 10 kuanzia saa 5 asubuhi Jumanne,
Tarehe 17/05/2016.
Sababu za kuzimwa kwa
Mtambo wa Ruvu Chini ni kuzuia uvujaji uliotokea mtamboni kwenye bomba la inchi
72.
Kuzimwa
kwa mtambo wa Ruvu Chini kutasababisha maeneo yafuatayo katika Jiji la Dar es
salaam kukosa Maji:
MJI WA BAGAMOYO
VIJIJI VYA ZINGA, KEREGE NA MAPINGA, BUNJU, BOKO, TEGETA, KUNDUCHI, SALASALA,
JANGWANI, MBEZI BEACH NA KAWE.
Maeneo Mengine ni : 
MLALAKUWA, MWENGE,
MIKOCHENI, MSASANI, SINZA, KIJITONYAMA, KINONDONI, OYSTERBAY, MAGOMENI, UPANGA,
KARIAKOO, CITY CENTRE, ILALA, UBUNGO MAZIWA, KIGOGO, MBURAHATI, HOSPITALI YA
RUFAA MUHIMBILI, BUGURUNI, CHANGOMBE NA KEKO.
WANANCHI
MNASHAURIWA KUHIFADHI MAJI NA KUYATUMIA KWA MATUMIZI YA LAZIMA.
DAWASCO INAWAOMBA RADHI WANANCHI WA MAENEO HUSIKA
KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA.
Wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja
022-2194800 au 0800110064 (BURE)
IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU

No comments: