Wednesday, May 11, 2016

ULISIKIA SAKATA LA WAMACHINGA KUTAKIWA KUHAMA KARIAKOO,SASA LEO WAMEIBUKA NA KUPINGA,IPO HAPA

Siku moja imepita tangu Baraza la Madiwani kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Isaya Mnguruni kutoa tamko kuwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga wanatakiwa waondoke maeneo ya Kariakoo mpaka kufikia siku ya jumamosi na kwenda maeneo waliyo pangiwa kwa madai ya kuwa sehemu hizo zimekidhi vigezo vya wao kufanya biashara.

Tamko hilo limepokelewa tofauti na Machinga ambapo Mwenyekiti wa wafanyabiashara ndogondogo katika Halmashauri ya Ilala Steven Lusinde ameeleza kuwa baada ya kupokea taarifa hiyo waliamua kutembelea maeneo hayo ambayo ni Ukonga,Tabata Muslim,Kigogo Fresh,Kivule na kukuta hayapo katika miundombinu stahiki, yakikabiliwa na changamoto mbalimbali.

Akizitaja baadhi ya changamoto hizo Lusinde amesema wamekuta maeneo yamevamiwa na watu wanaojiita wazawa hivyo wakienda huko wanahofu ya kutokea uvunjifu wa amani, huku mengine yakiwa hayana vizimba, huduma ya choo na maji.

Lusinde ameongeza kuwa hawapingani na serikali kuhusu wao kuondoka ila ni vyema serikali ikajipanga kwa kuboresha mazingira  na kutatua migogoro iliyopo, kwani bila kufanya hivyo watakuwa hawawatendei haki.

No comments: