Thursday, June 23, 2016

HARAMBEE YA OKOA MAISHA YA WANAHABARI KUFANYIKA MJINI DODOMA JUMAMOSI

Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya kampeni ya Okoa Maisha ya Waandishi wa Habari, Peter Nyanje (wa pili kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kuhusu harambee maalum ya kuosha magari, ijulikanayo kama ‘Media Car Wash for Health’, yenye lengo la kukusanya fedha zitakazotumika kuwakatia Bima ya Afya Waandishi wa habari takribani 1000, itakayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kesho Jumamosi. Kushoto ni Mjumbe wa Kamati hiyo, Grace Nacksso, Mwakilishi wa Media Assistant waratibu, Dickson Matikila (kulia) na Msanii wa Bongo Fleva, Haruna Kahena ‘Inspector Haroun’.
Msanii wa Bongo Fleva, Haruna Kahena ‘Inspector Haroun’ (wa pili kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kuhusu ushiriki wake katika harambee maalum ya kuosha magari, ijulikanayo kama ‘Media Car Wash for Health’, iliyoandaliwa na Kamati ya Maandalizi ya kampeni ya Okoa Maisha ya Waandishi wa Habari, yenye lengo la kukusanya fedha zitakazotumika kuwakatia Bima ya Afya, waandishi takribani 1000, itakayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kesho Jumamosi. Kushoto ni Mjumbe wa Kamati hiyo, Grace Nacksso, Mwakilishi wa Media Assistant waratibu, Dickson Matikila (kulia) na (wa pili kushoto) ni Mjumbe wa kamati, Peter Nyanje.

No comments: