Monday, June 6, 2016

KELEKEA MFUNGO WA RAMADHAN-SHEIKH JALALA ALAANI VIKALI MAUAJI YANAYOENDELEA NCHINI SASA


Na Exaud Mtei
WAKATI nchi ya Tanzania ikiwa katika sintofahamau kubwa kutokana na matukio ya mauaji ambayo yameitikisa nchi kwa kipindi kifupi na kuacha watanzania wakiwa katika wasiwasi mkubwa naye kiongozi mkuu wa waislam wa dhahebu la shia nchini Tanzania Seikh HEMED JALALA ameibuka na kulaani vikali  mauaji ambayo ameyaita ya kiigaidi yaliyotokea katika mikoa mbalimbali nchini huku akisema kuwa vitendo hivyo vinakwenda kinyume na Imani ya dini yoyote nchini na vinastahili kupingwa na kila mtanzania.

Akizungumza na wanahabari mapema leo jijini Dar es salaam wakati akitoa salamu za pongezi kwa waislam wote kwa kuuanza mwezi wa mfungo wa ramadhani Sheikh JALALA amesema kuwa Tanzania ni nchi iliyotambulika duniani kote kuwa kisiwa  ya Amani na utulivu hivyo vitendo hivyo ni vitendo ambavyo vinaharibu sifa ya nchi duniani kote.
Ameongeza kuwa vitendo vya ugaidi na ukatili pamoja na uvunjifu wa Amani nchini ni vitu vya kuwa makini sana na kuwa na tahadhari sana kwani vinaweza kuzuia hata waumini mbalimbali kuabudu kwa uhuru na Amani hasa kipindi hiku cha mfungo

Aidha amewataka watanzania sasa kuchukua jukumu la kuwa walinzi wa maeneo wanayoishi na kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa haraka pale ambapo wanaona watu au kikundi cha watu ambao hawaeleweki wakiwa katika maeneo yao huku akivitaka vyombo vya usalama kuhakikisha kuwa wanachukua taarifa za wananchi na kuzifanyia kazi mara moja ili kuepuka kutokea kwa matukio ya kigaidi na mauaji kama yaliyotokea mwezi huu.

Tukumbuke kuwa siku za hivi karibuni kumekuwa na mfululizo wa matukio ya mauaji ya kutisha huku wengine wakichinjwa ambayo yaiyokea mkoani mwanza na mengine mkoani tanga matukio ambayo yameacha simanzi kwa watanzania walio wengi.

Katika hatua nytingine Sheikh JALALA akizungumzia mwezi mtukufu wa ramadhani amewataka waislam wote nchini  kuutumia mwezi huo kama mwezi wa kuwa karibu Zaidi na mungu na kuhakikisha kuwa wanautumia kudumisha Amani na umoja uliopo nchini.

No comments: