Wednesday, June 22, 2016

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI MJINI DODOMA

J1Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa  akimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,Utumishi na Utawala Bora,  George Simbachawene (wapili kulia)  na Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge, Kazi,Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama   watatu kulia) bungeni mjini Dodoma Juni 22, 2016.  Wengine kutoka kushoto ni Mbunge wa Babati Vijijini  Jitu Vrajlal Son, , Mbunge wa Bukoba Vijijini Jasson Rweikiza,Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde, Mbunge wa Korogwe Stephen Ngonya na Mbunge wa Kilolo Venance Mwamoto.
J2Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akiwa katika picha ya pamoja na Wananchi kutoka jimbo la Ukongwa waliotembeklea  bunge  kwa mwaliko wa Mbunge  (wapili kulia)  Juni 22, 2016.
J3 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Utumishi, na Utawala Bora , George Simbachawene  (kulia) na Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei  Massay (kushoto) kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Juni 22, 2016. Wapili kushoto ni Mosses Kirway  na wapili  kulia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu yaTaifa ya  CCM, Thomas Lulu, wote  wakiwa ni wageni waliotembelea Bunge wakitoka Mbulu.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: