Monday, June 6, 2016

RAIS MALINZI AWATAKIA MFUNGO MWEMA WAISLAMU


 


Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewatakia kila la kheri Waislamu wote nchini katika kipindi cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaoanza sasa.


Rais Malinzi amewataka Watanzania kuendeleza tunu za amani na utulivu ili kushiriki katika ibada kama inavyostahili. Amesema kufanikiwa wa Waislamu katika ibada hiyo ni chachu ya mafanikio ya kila sekta na hasa soka ambalo hupendwa na mashabiki wengi ndani na nje ya nchi.

No comments: