Thursday, June 16, 2016

TIGO YATOA DOLA 12,000 (26.4M/-) KWA C-SEMA KUBORESHA KITUO CHA HUDUMA YA SIMU KWA MTOTO

Meneja wa Huduma za Jamii wa Tigo Woinde Shisael akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya dola za Kimarekani 12,000(26.4m/-) Ofisa Mtendaji Mkuu wa C-Sema Kiiya kwa  ajili ya kuboresha kituo cha kutoa cha kupokelea simu cha Huduma ya Simu kwa Mtoto kilicho mjini Zanzibar, zoezi hili limefanyika leo katika viwanja vya JMK, Dar es Salaam kwa ajili ya kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika.
 
 Kampuni ya Tigo Tanzania imeshiriki katika kumbukumbu ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2016 kwa kuchangia  zaidi ya shilingi 26.4m/-($12,000) kwa asasi isiyo ya kiserikali ya  C-Sema  ambayo inaendesha kituo cha kupokelea simu cha Huduma ya Simu kwa Mtoto (Child Helpline Call Centre)  mjini Zanzibar ambacho kinatoa ushauri na kuwaunganisha watoto kupata huduma sahihi za kijamii  kikishirikiana na serikali.
Tigo na asasi ya C-Sema  watafanya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika  mwaka huu katika Kituo cha Michezo cha JMK Park jijini Dar es Salaam Alhamisi Juni 16. Siku ya Mtoto wa Afrika ni tukio linalofanyika duniani kote  kila Juni 16 ya kila mwaka. 
Akizungumza wakati wa kukabidhi  msaada huo, Meneja wa Huduma za Jamii wa Tigo, Woinde Shisael  alisema  msaada huo ni sehemu ya  mkakati wa kampuni  wa kuwekeza katika  ajenda ya kumlinda mtoto iwe kwa njia ya mtandao  na hata nje ya mtandao.
Akitoa shukrani  kutokana na msaada, huo Ofisa Mtendaji Mkuu wa C-Sema, Kiiya JK aliishukuru kampuni hiyo ya simu kwa  kutoa mchango sahihi katika  kuwekeza rasilimali zake  ili kuhakikisha kwamba watoto na wazazi wanakuwa na uhakika wa kupata jukwaa ambalo wanaweza kutoa taarifa  kuhusu aina yoyote ya ukatili dhidi yao.
“Ninaishukuru  Tigo kwa msaada huu wakati leo tunasherehekea watoto wa Afrika kwa kuzisikiliza sauti zao wakati wakitueleza  kile wanachokifikiria kuhusu masuala mbalimbali yanayowasibu na nini kitu gani kifanyike  kutokomeza  matendo mabaya ambayo yanaweza   kukwamisha maendeleo yao.”
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tukio la mwaka huu la Siku ya Mtoto wa Afrika.
Kituo cha taifa cha kupokelea simu za huduma ya simu kwa mtoto (Child Helpline call centre) kilianzishwa rasmi Juni 15, 2013  kikiwa na kituo cha Dar es Salaam na Zanzibar.

No comments: