Ikiwa sekeseke ndani ya chama cha wananchi CUF likianza
kufukuta juu ya kurudi au kutorudi kwa aliyekuwa mwenyekiti wao Profesa IBRAHIM
LIPUMBA Wanachama wa chama hicho mkoani
Mtwara wamewataka wajumbe wa mkutano mkuu wa CUF wanaokutana mnamo tarehe 21
mwezi Agust mwaka huu kumkubalia kiongozi huyo arejee kwenye nafasi yake ili
kukiimarisha chama hicho..
Kauli hiyo inayoendelea kuleta sintofahamu juu ya sakata hilo
imekuja wakati wa ufunguzi wa shina la chama cha wananchi CUF hapo jana katika
mtaa wa Chipuputa manispaa ya Mtwara mikindani ambapo walisema kuwa
tangu Prof. Lipumba atoke kwenye nafasi hiyo chama kimekuwa kikiyumba na
kwamba hakuna wa kuyasimamia na kuyakemea mambo mabaya yanayotokea ndani ya
chama.
Aidha Akizungumza katibu wa CUF mkoa wa Mtwara Said Kulaga
alisema katika tafiti waliyoufanya kwa kipindi kifupi ndani ya mkoa wa Mtwara
wamebaini kuwa wanachama wengi wanamtaka Pro. Lipumba arejee kwenye nafasi yake
ili kukiimarisha chama hicho.
“Kwa niaba ya chama na utafiti nilioufanya kwa kushirikiana
na viongozi wangu inaonekana watu wengi wanachama wanaunga mkono na wanaona
umuhimu wa Prof Lipumba kurudi kwenye nafasi ya uongozi,kwahiyo kama mratibu wa
chama mkoa natoa tamko hili kwa niaba ya mkoa wa Mtwara na viongozi wenzangu wa
mkoa wa Mtwara ambao litakuja kupewa Baraka na mwenyekiti wa chama wa wilaya ya
Mtwara mjini kwa niaba ya wenyeviti wa mkoa ambao wameniagiza hapa,”alisema
Kulaga
Aidha alisema kuwa tamko hilo linasema CuF ni taasisi huru ya
kisiasa inayoongozwa kwa mujibu wa miongozo yake kwa maana ya katiba
hivyo misingi ya katiba kama imekiukwa inapswa kufuatwa ili kumaliza changamoto
zilizopo na si migogoro ili kuleta umoja.
Akizungumza mbunge wa jimbo la Mtwara mjini ,Maftah Nachuma
alisema anaungana na wananchama wake waliompa ridhaa ya ubunge hivyo anaheshimu
maamuzi yao kwani chama sio mtu mmoja.
“Kimsingi chama ni wanachama,chama si mtu mmoja wala si
mbunge,mambo yote nayofanya nmeagizwa na chama kwenda kuyafanya nje na ndani ya
bunge kwahiyo kama tamko limetolewa na wanachama ni maamuzi ya wanachama na
ndio maamuzi ya wengi na wanachama ndio walioniweka mimi hivyo siwezi kwenda
tofauti nao,suala la tamko I suala la wanachama wenyewe na wefanya vikao
sio kwamba wametoa hayo matamko bila sababu ukipita huko mitaani kila mtu
anamzungumzia Prof Lipumba,”alisema Nachuma
Mwanachama Fatuma Chande alisema wanamuhitaji Prof Lipumba
kutokana na kuwaeleza juu ya haki zao za msingi juu ya rasilimali gesi
iliyogundulika Mtwara kwani aliweza kuwaeleza haki zao na sasa wananufaika.
“Lengo letu sisi tunawatuma viongozi wa wilaya mkamrudishe Pr
Lipumba kwasababu ni mpambanaji wa kusini bila kujali anatokea wapi
,tusingeweza kujua juu ya haki zetu kama za gesi kama sio Lipumba kwani alikuja
hapa akatupa tasfiri ya gesi na sisi wanamtwara tukajua haki zetu na mpaka sasa
tunafaidika,”alisema Chande
Naye Radhid Abdallah alisema “Sisi tumeumbwa na Mungu makundi
mawili yakipigana yapatanisheni haraka,kundi lingiine likiwaonea lipigeni,sasa
Pr Lipumba amejirudi na sisi tunatakiwa tukatae ugomvi,anayesema hafai huyo ni
mgomvi..kukosekana kwake katika nafasi hiyo pigo kwa chama ,”alisema
Abdallah
No comments:
Post a Comment