Tuesday, July 5, 2016

Mchezo wa Utangulizi Kombe la Ramadhani Masauni na Jazeera Cup Kati ya Meveterani wa Kikwajuni na Timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Uliofanyika Uwanja wa Mnazi Mmoja Timu ya Baraza Imeshinda Bao 1--0.

Waziri wa Habari Michezo Mhe Nape Moses Nnauye akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya TAYI Tanzania Ndh Abdalla Othman Miraji wakati akihudhuria fainali za Kombe la Masauni and Jazeera lililofanyika jana usiku katika viwanja vya Mnazi Mmoja kati ya Kilimani na Kisimamanjongoo, kabla ya mchezo huo kulikuwa na mchezo wa utangulizi kati ya Maveterani wa Kikwajuni na Timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, katika mchezo huo timu ya Baraza imeshinda bao 1--0. 
Timu za Baraza na Maveterani zikiingia uwanjani tayari kwa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika wakati wa fainali hiyo Timu ya Maveterani wa Kikwajuni wakiongozwa na Mhe. Mbunge wa Kikwajuni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Eng Hamad Yussuf Masauni kulia na Timu ya Baraza ikiongozwa na Mwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni Mhe Nassor Salum Jazeera.
Waziri wa Habari Michezo Mhe Nape akisalimiana na wachezaji  wa timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kabla ya kuaza kwa mchezo wao na maveterani wa kikwajuni Zanzibar.

Waziri wa Habari Michezo Mhe Nape akisalimiana na wachezaji  wa timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kabla ya kuaza kwa mchezo wao na maveterani wa kikwajuni Zanzibar.
Mhe Waziri wa Michezo Mhe Nape akisalimiana na Nahodha wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Hamad Masauni wakiwa na bashasha wakati wakisalimiana. 
Waziri Nape akisalimiana na wachezaji wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni kabla ya mchezo wao wa kirafiki na Timu ya Baraza la Wawakilishi ukiwa ni mchezo wa utangulizi wa Fainali ya Kombe la Ramadhani Masauni and Jazeera. mchezo uliofanyika uwanja wa mnazi mmoja jana usiku.
Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe Rashid Ali Juma akizungumza wakati wa mchezo huo wa ufunguzi wa Fainali ya Kombe la Ramadhani Masauni and Jazeera Cup na kumkaribisha Waziri mwezake wa Michezo Mhe Nape Mnauye, akiwa kulia kwa waziri.
Waziri wa Michezo Tanzania Mhe Nape Mnauye akitowa nasaha zake kabla ya kuaza kwa mchezo wa kirafiki wa utangulizi wakati wa fainali ya Kombe la Ramadhani Masauni and Jazeera Cup zilizofanyika uwanja wa mnazi mmoja jana usiku
Wachezaji wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni wakimsikiliza Waziri wa Michezo Mhe Nape Mnauye akitowa nasaha zake kwa Wanamichezo waliohudhuria fainali hiyo na kuupongeza Uongozi wa Kamati ya Mashindano hayo Jimbo la Kikwajuni Zanzibar.
Wachezaji wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni wakimsikiliza Waziri wa Michezo Mhe Nape Mnauye akitowa nasaha zake kwa Wanamichezo waliohudhuria fainali hiyo na kuupongeza Uongozi wa Kamati ya Mashindano hayo Jimbo la Kikwajuni Zanzibar.
Nahodha wa Timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Nassor Salim Jazeera akiongoza wachezaji wake kusalimiana na Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar. 
Kikosi cha Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni. kilichotowa upinzani kwa Timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar na kulazimishwa kufungwa bao moja.   
Kikosi cha Timu ya Baraza la Wawakilishi kilichotoa kipigo cha bao moja dhidi ya Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar.
Mchezaji wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar akimpita mchezaji wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar wakati wa mchezo wao wa kirafiki wa utangulizi wa ufunguzi wa mchezo wa Fainali kati ya Timu ya Kisimamanjongoo na Kilimani. 
Mchezaji wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar akimiliki mpira wakati wa mchezo wao wa kirafiki wa utangulizi wa ufunguzi wa mchezo wa Fainali kati ya Timu ya Kisimamanjongoo na Kilimani.
Mchezaji wa Timu ya Maveterani wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar akimpita mchezaji wa Timu ya Baraza la Wawakilishi, wakati wa mchezo wao wa kirafiki wa utangulizi wa ufunguzi wa mchezo wa Fainali kati ya Timu ya Kisimamanjongoo na Kilimani.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe. Hamad Masauni akimiliki mpira akijiandaa kumpita mchezaji wa Timu ya Baraza la Wawakilishi wakati wa mchezo wao wa kirafiki.
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe. Hamad Masauni akimiliki mpira akijiandaa kumpita mchezaji wa Timu ya Baraza la Wawakilishi wakati wa mchezo wao wa kirafiki.

Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Mhe. Hamad Masauni akimiliki mpira akijiandaa kumpita mchezaji wa Timu ya Baraza la Wawakilishi wakati wa mchezo wao wa kirafiki.
Imetayarishwa na OthmanMapara 
Zanzinews.Blgospot.com.
Email othmanmaulid@gmail.com.

No comments: