Thursday, July 28, 2016

RAIS WA SIMBA SPORTS CLUB EVANS AVEVA AZINDUA WIKI YA SIMBA NA SIMBA DAY 2016.


Rais wa Simba Sport Club  Evans Aveva akizungumza na Vyombo vya Habari leo wakati wa Uzinduzi wa Simba Week Akiwa Sambamba Katibu Mkuu wa Simba Patrik Kahemela (Kulia) na Afisa Masoko na Mawasiliano Kutoka Eaggroup Richard Ryaganda( kushoto) .
Simba inasherehekea wiki maalum iliyo Batizwa Jina la Simba Week ambayoImezinduliwa Leo na Rais wa Simba Sport Club Ndugu Evans Aveva na  hufikia kilele chake Tarehe 8 Mwezi Agosti. Mwaka huu siku hii ya Simba week itakuwa na uzito wa kipekee kwani Klabu ya Simba itakuwa inaanza Sherehe za kuadhimisha Miaka 80 ya klabu Hiyo. Sherehe za Wiki ya Simba zinaenda sambamba na dhima yetu ya kuendeleza Mabadiliko chanya ndani ya Simba bado inaendelea kushika kasi, Katika kipindi cha mwaka mzima.  
Katika Kipindi Hiki Simba  Sport Club imekuwa na utaratibu wa kuwa na siku maalum kwaajili ya kufurahi, kuwatambulisha Rasmi wachezaji,Jezi za timu na kujiandaa kwa Msimu Mpya, siku hii imekuwa Maarufu kama Simba Day. Tangu  Ianzishwe imekua ikiboreka Siku hadi siku, mwaka huu Imeona ni Muhimu kuiboresha zaidi na hususani kuangalia Mchango wa timu Hiyo kwa Jamii inayoizunguka. 
 Simba iliamua kuanzisha Simba Week ambayo lengo lake kuu ni kuwa wiki ya Simba Sports Club kufanya kazi za Jamii, kukuza vipaji vya soka vya vijana, kutembelea  Wadau wa Maendeleo na pia Shughuli Nyingine Zenye Tija kwa Timu..Siku ya Simba Day, Simba Sports Club itacheza Mechi naInter Clube ya Angola kwenye Mechi hii Wachezaji Wapya wataonekana Rasmi baada ya Maandalizi. 

No comments: