Lilian Liundi Mkurugenzi wa mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP LILIAN LIUNDI akizungumza na wanahabari mapema leo |
EASSI ni asasi ya kuhamasisha mpango wa maendeleo ya wanawake katika ukanda wa afrika
mashariki (EASSI) yenye miaka 20 sasa ni asasi ya kirahia ya kikanda
iliyoanzishwa mwaka 1996.
EASSI ina dhamira ya kuwezesha ufuatiliaji wa utekelezaji wa makubaliano ya jukwaa la utendaji wa
Beijing (Beijing platforms for action{ BPFAS}) Ambacho ni chombo cha mkutano
wa nne wa wanawake uliofanyika nchini Beijing nchini china mwaka 1995 na
mkutano wa nne wa wanawake afrika uliofanyika Dakar Senegal asasi hii ambayo
imesajiliwa nchini Uganda kama asasi isiyo ya kibiashra, inafanyakazi na asasi
nyingine za kitaifa katika nchi nne zikiwamo Burundi,
Eritrea,Ethiopia,Kenya,Rwanda,Somalia Tanzania na Uganda
Kuanzia
mwaka 2008 EASS kwa kushirikiana na
mashirika yanayotetea haki za wanawake ikiwemo TGNP Mtandao na nchi tano
wanachama ilikuwa ikifanya kampeni kuweza kuleta itifaki ya usawa wa kijinsia na
itifaki hii iliweza kubadilishwa na kuwa mswaada binafsi na kuwasilishwa katika
bunge la afrika mashariki na kuwa tayari kusikilizwa na umma katika nchi tano
wanachama na lengo la mswaada huo nikukuza mahusiano ya kijamii kiuchumi na
kisiasa na utamaduni kwa manufaa ya wanawake na wanaume ili kuweza kufuatwa kwa
haki za binaadamu katika nchi hizo zimeridhia matamko mbalimbali kwa mfano azimio
la Beijing, SEDO itifaki ya mkataba afrika kuhusu haki za binadamu malengo endelevu ya kidunia la kwanza
umasikini na la tano kuhusu usawa wa kijinsia kampeni hii ilichangizwa nchi za
kusini mwa afrika SADC iliyofanywa na
wanawake kusini mwa afrika iliyowahimiza kuwepo kwa tamko au mkataba wa kijinsia ambao baadae ilibadilika na kuwa
itifaki ya kijinsia.
Mwenyekiti
wa TGNP Mtandao Lilian Liundi amesema kuwa afrika mashariki
inahitaji mswaada wa sheria kijinsia na maendeleo kwa kuwa jumuiya ya afrika
mashariki imesaini mikataba mingi ya kitaifa na kikanda na pia ukiukwaji wa
haki za wanawake umeendelea kushamili ndani ya jumuiya hiyo kwa mfano vitendo
vya ukeketaji bado vinaendelea na kwamba kwa Tanzania ni28.4- 31.7 Kenya 27% sudan 88% Uganda 1%
Lakini
pia amisema kuwa hata katika maswala ya uzazi vifo vimezidi kuongezeka kwa
kiwango kikubwa sana na ametoa idadi katika wazazi laki moja wanafariki hadi 740
kwa burundi Kenya 400 Rwanda 320 Tanzania 410 Uganda 360 na pia anasema hili si
la kulifumbia macho kwa kuwa ni kinyume na makubaliano ya Abuja ambayo nchi
hizi ziliweza kukubali kwa kusema asilimia 15 itengwe kwaajili ya sector ya
afya na akiongezea kwa kusema hii ni baadhi tu ya mifano lakini ipo mingi sana
inayomkandamiza mwanamke.
Ameongezea
kuwa mswaada huo itakapopitishwa itasaidia sana wanawake wengi ambao
wanakandamizwa na pia itaoanisha sheria za kikanda na kimataifa kwa afrika mashariki na kuondoa unyanyasaji
wa kijinsia na kuleta usawa kwa jinsia zote katika Nyanja mbalimbali kwenye
maamuzi , uongozi na biashara. Pia sheria hii itawawezesha wanawake kwa wanaume
kuweza kukua katika biashara na ubaguzi wa kijinsia utakuwa umetokomezwa.
Pia
alisema kuwa sio tu wanasukumwa kupitisha sheria hiyo ila wanania thabiti ya
kupima selikali za nchi zote wanachama kweye kutekeleza majukumu yao ya kuweka
usawa wa kijinsia kwa mara ya kwanza wame
amua kuanzisha kipimo cha mlengwa wa kijinsia na pia iko kipimo litatoka na
chapisho lakini pia katika hilo chapisho litakuwa na takwimu maalumu kuhusu
kipimo katika nchi zote wanachama na chapisho la kwanza litatoka mwezi oktoba,
lakini pia hilo chapisho halitalenga selikali pekee mfano tukisema umasikini
umeshuka wataweza kutembelea wananchi nakuweza kuongea nao na kujua ni kweli
kama takwimu zinavyosema au kuna udanganyifu umetendeka.
No comments:
Post a Comment