Mkurugenzi mtendaji wa LHRC Bi Hllen Kijo Bisimba akifafanua jambo wakati LHRC walipotoa Taarifa ya haki za binadamu nchini Tanzania kwa miezi sita iliyopita |
Na
Exaud Mtei
Watu
394 wakiwemo vikongwe katika maeneo mbalimbali ya vijijini nchini Tanzania
wameuawa kwa Imani za kishirikina kwa kipindi cha miezi sita kwa mwaka 2016
huku ikitajwa ni ongezeko kubwa la mauaji hayo ukilinganisha na mwaka jana
ambapo ni vifo 57 tu vilivyoripotiwa nchini.
Hali
hiyo imeelezwa leo katika taarifa ya haki za binadamu kwa miezi sita kuanzia
January ya mwaka 2016 iliyotolewa na kituo cha sheria na haki za binadamu
nchini Tanzania lhrc ikiwa ni utaratibu wa kituo hicho kutoa Report kuonyesha
hali ya mwendendo wa haki za binadamu nchini Tanzania kwa kipindi husika.
Akizungumza
wakati wa utoaji wa Taarifa hiyo mbele ya wanahabari Jijini Dar es salaam
mkurugenzi mtendaji wa LHRC Bi Hllen Kijo Bisimba amesema kuwa haki ya kuishi
nchini Tanzania imeendelea kukiukwa kwa kasi huku mauaji ya Imani za
kishirikina yakionekena kuongezeka kwa kasi.
Paul Mikongoti Kutoka LHRC akifafanua baadhi ya mambo ambayo yanapatikana katika Report Hiyo |
Ameeleza
kuwa pamoja na Idadi hiyo ya 394 iliyotajwa na Report hiyo bado kuna uwezekenao
mkubwa kuwa matukio ni mengi Zaidi ya hayo kwa kuwa mauaji ya aina hii mengi
yamekuwa hayatolewi taarifa kwenye vyombo vya dola,huku akiitaja mikoa ya
Mwanza,Simiyu,Geita,Shinyanga,ikiendelea kuwa vinara wa matukio ya mauaji
yanayohusisha Imani za kishirikina.
Aidha
katika Report Hiyo iliyotolewa leo na LHRC imeonyesha maeneo mbalimbali ambayo
bado haki za binadamu zimekuwa zikikiukwa kwa kasi kwa kipindi cha miezi sita
iliyopita huku wakiitaka serikali kuhakikisha wanachukua hatua za haraka ili
kudhibiti hali hiyo ambayo ikiachwa inaweza kuligharimu Taifa.
Paul
Mikongoti ni Mwanasheria na mtafiti kutoka LHRC ambapo akisoma baadhi ya maeneo
hayo ameeleza kuwa mwaswala kama kujichukulia sheria
mikononi kwa wananchi bado ni tatizo nchini Tanzania ambapo watu 135
wameuawa kwa watu kujichukulia sheria mkononi,huku eneo lingine likiwa ni watu kufia mokononi mwa polisi ambapo Kwa mujibu wa
Taarifa Rasmi ya Jeshi la polisi ni taarifa ya mtu mmoja aliyefia mikononi mwa
polisi japo katika LHRC wamekiri kwa wao wanataarifa ya watu wawili Zaidi
waliofia mokononi mwa polisi.
Kaimu Mkurugenzi wa LHRC Imelda Lulu Urio Akifafafanua jambo |
Maeneo
mengine ni uvamizi wa vituo vya polisi,mauaji ya
ukatili kwa watu wenye ualbino,ajali za barabarani,haki ya uwakilishi,haki ya
wanawake na watoto,haki ya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni pamoja na haki ya
kupata habari na uhuru wa vyombo vya habari,haki za kisiasa,haki ya afya,ambapo
kwa pamoja mambo hayo yameonekana kukiukwa sana katika kipindi cha miezi sita
iliyopita jambo ambalo linahitaji kuangaliwa kwa makini Zaidi.
Katika
eneo la haki za kisiasa Report hiyo imeeleza kuwa sakata la Jeshi la polisi
kuzuia shughuli za kisiasa ikiwemo mikutano ya kisiasa hasa ile inayofanywa na
vyama vya upinzani ukiwemo ule wa CHADEMA kahama na ambapo watu walipigwa mabomu pamoja na kongamano
la ACT WAZALENDO kupigwa marufuku ni ushahidi tosha kuwa haki ya kufanya siasa
nchini Tanzania imekiukwa na serikali ya awamu ya tano inahitaji kujitagfakari
upya kwani kazi ya mwanasiasa ni kufanya siasa hivyo anahitaji haki hiyo.
Aidha
sakata la utumbuaji majipu lililoanzishwa na serikali ya awamu ya tano likiwa
na lengo la kurudisha nidhamu katika kazi nakutokomeza Rushwa limetajwa kama
moja kati ya mambo yaliyokiuka haki za binadamu nchini kwa kile kilichoelezwa
kuwa ni kukosekana kwa haki ya wale wanaotuhumiwa kupewa nafasi ya kujieleza
kabla ya hatua kuchukuliwa ambapo kwa mujibu wa katiba ya Tanzania inamtambua
tu kama mtuhumiwa mpaka pale mahakama itakapomkuta na hatia ndipo anaweza
kupewa adhabu stahiki.
No comments:
Post a Comment