Monday, August 1, 2016

ALI KIBA KUPAMBA SHAMRASHAMRA ZA TAMASHA LA CHANELI YA STARTIMES KISWAHILI

TIM1Mkurugenzi Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Kushoto ni msanii Ali Kiba ambaye atakuwepo kutumbuiza na kutoka kulia ni Msanii Madee pamoja na Meneja Mauzo wa Huawei, Bw. Zhang Heng, ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL.
TIM2Msanii wa muziki wa bongo flava Ali Kiba (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Wakimsikiliza kwa makini kulia ni Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li na kushoto ni Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian. Huawei ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL.
TIM5Msanii wa bongo flava kutoka kundi la TipTop Connenction lenye maskani yake Manzese, Madee akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Huawei ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL.
TIM6Msanii wa kizazi kipya Bi. Snura alimaarufu ‘Mama Majanga’ akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Msanii Madee wa kundi la Tip Top Connection.

TIM7Msanii wa muziki wa singeli Eskide akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian. Huawei ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL.
TIM8Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Huawei ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL. Kulia ni Msanii Ali Kiba.
TIM11Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Huawei, Bw. Zhang Heng, ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha la StarTimes Kiswahili linalokwenda kwa jina la SEREBUKA MUSIC FESTIVAL, Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li, Msanii wa muziki wa bongo flava Ali Kiba na Meneja wa chaneli ya StarTimes Swahili, Bi. Wang Qian wakikata keki kuashiria uzinduzi wa tamasha la kusherehekea miaka miwili ya chaneli ya Kiswahili ya StarTimes litakalofanyika siku ya Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Wasanii wakubwa nchini kulishambulia jukwaa, wakiwemo Ali Kiba, Lady Jaydee, Yamoto Band, Madee, Juma Nature, Snura, Stamina, Eskide (msanii wa muziki wa singeli) na bila ya kusahau wakali wa bongo movie pia watakuwepo.
…………………………………………………………………………………………………..
Wasanii wa muziki wa Bongo Flava Ali Kiba na Lady Jaydee wanatarajiwa kutumbuiza katika tamasha la kusherehekea miaka miwili tangu kuanzishwa kwa chaneli ya StarTimes Kiswahili siku ya Jumamosi ya Agosti 13, 2016 katika viwanja vya Posta, Kijitonyama.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo Mkurugenzi Msaidizi wa Masoko na Maudhui wa StarTimes Tanzania, Bw. Damien Li amesema kuwa tamasha hilo linadhamiria kusherehekea kwa pamoja na wateja wao mafanikio yaliyofikiwa na chaneli ya StarTimes Kiswahili katika kuonyesha vipindi vyenye maudhui ya Kiswahili nchini Tanzania na Kenya.
“Chaneli hii mwaka huu mwezi wa Agosti inatimiza miaka miwili tangu kuanzishwa kwake mnamo Agosti mosi mwaka 2014. Chaneli ya StarTimes Kiswahili inaonekana katika nchi mbili za Tanzania na Kenya na hivyo kutoa wigo mpana kwa wasanii na watayarishaji wa vipindi hapa nchini kupata fursa ya kuonekana maeneo hayo. Vipindi vingi katika chaneli hii huangazia masuala ya filamu, muziki, burudani, vyakula, mitindo ya maisha na mavazi pamoja na tamaduni za watu wa Afrika ya Mashariki hususani kwa nchi hizo mbili ambavyo huwasilishwa kwa lugha ya Kiswahili.” Alisema Bw. Li
“Tamasha hili litahusisha shughuli mbalimbali hususani kuangazia maudhui yanayopatikana kwenye chaneli ya StarTimes Kiswahili lakini pia litapambwa na burudani kadhaa kutoka kwa wasanii watakaoalikwa. Siku hiyo watanzania watawashuhudia wasanii wakubwa wa muziki wa bongo flava jukwaani kama vile Ali Kiba, Lady Jaydee, Juma Nature, Madee, Yamoto Band, Snura na Stamina. Pia kutakuwepo na wasanii mashuhuri kutoka katika tasnia ya bongo movie ambao filamu zao zinaonekana kupitia chaneli hii kama vile Wema Sepetu, JB, Steve Nyerere na Ray Kigosi.” Aliongezea Bw. Li
Chaneli ya StarTimes Kiswahili inapatikana katika visimbuzi vyote viwili vya StarTimes yaani cha antenna kuazia kifurushi cha NYOTA kwa shilingi 6000/- na cha dishi kuanzia kifurushi cha NYOTA PLUS kwa shilingi 8000/- kama malipo ya mwezi. Kampuni hiyo inajivunia kuwa ya kipekee nchini Tanzania kwa kutoa matangazo bora ya dijitali kwa gharama nafuu ambayo kila mtu anaweza kuimudu.
“Ningependa kutoa wito kwa wateja wa StarTimes na watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika tamasha hili litakalofanyika siku ya Jumamosi ya Agosti 13 mwaka huu pale viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Tiketi zitapatikana kwa bei ya kawaida kabisa ya kuanzia shilingi 5000/- na kupatikana katika vituo vitakavyoanza kutangazwa kwa njia mbalimbali. Tamasha hili ni maalumu kwa ajili ya kuwashukuru watanzania kwa kuipokea vizuri chaneli hii na kuifanya kuwa chaguo lao kubwa pindi watazamapo luninga, hivyo naomba wajitokeze kwa wingi.” Alimalizia Bw. Li
Naye kwa upande wake msanii wa bongo flava Ali Kiba akizungumza mbele ya waandishi wa habari amewaahidi makubwa wateja wa StarTimes na watanzania watakaohudhuria siku hiyo kuwa watapata burudani ya aina yake.
“Kwanza kabisa ningependa kutoa pongezi za dhati kwa kampuni ya StarTimes kwa kutambua mchango wa lugha ya Kiswahili na kuikuza miongoni mwa nchi wanazofanya biashara. Hii ni fursa ya kipekee kwa wasanii na watayarishaji wa kitanzania kuweza kupanua wigo wa kazi zao na kuweza kuonekana sehemu zingine. Kusema ukweli hapo awali wakati matangazo ya dijitali yanaingia nchini sikuweza kuiona fursa hii lakini sasa ninaona kazi za wasanii wetu zinaonekana na kutambulika kimataifa.” Alisema Ali Kiba
“Ningependa kutoa wito kwa StarTimes kupanua wigo zaidi wa chaneli hii ifike katika nchi zingine za jirani kama vile Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Kongo hata Afrika ya Kusini kwani kuna watanzania kule na waafrika ambao wanapenda kufahamu lugha ya Kiswahili na tamaduni za waswahili wenyewe. Na mwisho kabisa ningependa kuwaalika watanzania wote siku hiyo waweze kuhudhuria kwa wingi kwani tamasha hili ni lao, nawaomba waje kwa wingi kusherehekea kwa pamoja maudhui mazuri na ya kusisimua yanayopatikana ndani yake.” Alihitimisha Ali Kiba au King Kiba kama anavyojulikana miongoni mwa mashabiki wake

No comments: