Wednesday, August 10, 2016

MASAUNI AONGOZA HARAMBEE YA UJENZI WA KITUO CHA POLISI SEGEREA

 Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wa pili kulia), akishirikiana na viongozi wengine akiwemo Mbunge wa Jimbo la Segerea,Mheshimiwa Bonnah Kaluwa(wa kwanza kushoto),kuzindua   ujenzi wa kituo cha polisi kinachojengwa katika Jimbo la Segerea ikiwa ni mkakati wa kupambana na uhalifu katika jimbo hilo.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akishiriki ujenzi wa awali wa kituo cha polisi kinachojengwa katika Jimbo la Segerea ikiwa ni mkakati wa Mbunge wa jimbo hilo  kupambana na vitendo ya uhalifu katika jimbo hilo.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(suti nyeusi), akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya Ujenzi wa Kituo cha Polisi .Naibu Waziri huyo pia aliongoza Harambee ya Ujenzi wa kituo hicho ikiwa ni mkakati wa  Mbunge wa Jimbo hilo Bonnah Kaluwa, kupambana  na matukio ya uhalifu.Naibu Waziri huyo aliongoza
 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati wa Harambee ya Ujenzi wa Kituo cha Polisi .Wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea,Mheshimiwa  Bonnah Kaluwa. Ujenzi wa kituo hicho ni mkakati wa kupambana na matukio ya uhalifu yanayotokea katika jimbo hilo.
 Mbunge wa Jimbo la Segerea la Segerea, Bonnah Kaluwa, akimuongoza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(suti nyeusi) na viongozi wengine kwenda kutembelea eneo ambapo ujenzi  wa kituo cha polisi katika jimbo hilo umeanza ikiwa ni mkakati wa kupambana na matukio ya uhalifu jimboni hapo.
Wananchi wa Jimbo la Segerea, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani), wakati wa Harambee ya  Ujenzi wa Kituo cha Polisi ikiwa ni mkakati wa Mbunge wa Jimbo hilo, Bonnah Kaluwa, kupambana na matukio ya uhalifu katika jimbo hilo.(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA         MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments: