Saturday, August 27, 2016

Mkuu wa wilaya ILALA awataka wananchi wake wasijihusishe na maandamano ya UKUTA

Mkuu wa wilaya ya ILALA,SOPHIA MJEMA,amewataka wafanyabiashara katika soko la kariakoo kutoandamana siku ya tarehe moja mwenzi wa tisa.

Akizungumza na wafanyabiasha hao hii leo jijini Dar-es-salaam katika zoezi la usafishaji mazingira linalofanyika kila jumamosi ya mwisho wa mwenzi,amemewataka wafanyabiashara hao kutojihusisha katika maandamano ya tarehe moja mwenzi wa tisa  yajulikanayo kama UKUTA,
“nawaomba wafanyabiashara msiandamana siku hiyo kwani maandamano hayo hayana matiki wala na hayafuati sheria na katiba ya nchi iliyopo nawaomba siku hiyo mfanye bishara zenu kwa utulive na amani" Kiongozi huyo amesema  .

Pia MJEMA ametembelea hospital ya Amana akiwa na wakuu wa idara mbalimbali katika manispaa hiyo na kushiriki zoezi la usafishaji wa mazingira katika hospitali hiyo amewataka wauguzi na madaktali kuwa na utamaduni wakufanya usafi wa mara kwa mara  
 “ili wagonjwa  wapate matibabu bora na afya njema awanabudi kukaa  kwenye mazingira yaliyo safi hivyo natoa wito kwenu zoezi hili la usafi lisiishie hapa bali lifanyeni kila wakati ilikupunguza magonjwa mbalimbali ya mlipuko nchin"amesema.

Aidha diwani wa kariakoo,MASAMAKI,amewataka wananchi kujijengea utamaduni wakufanya usafi wenyewe bila kushurutishwa,kwan wakifanya ivyo watasidia kuondoa magonjwa mbalimbali ya mlipuko,pia amewaasa kufuata sheria na taratibu za nchi zilizopo   

No comments: