Thursday, September 8, 2016

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said Azindua Baraza la Vijana wa Shehia Tatu za Unguja Ukuu.

Shekh Mohammed Suleiman akisoma Quran kabla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana kwa Shehia Tatu za Unguja Ukuu Kaebona, Unguja Ukuu Kaepwani na Unguja Ukuu Tindini uliofanyika katika viwanja vya mpira Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja. 
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akisalimiana na Sheikh Mohammed Suleiman baada ya kusoma quran wakati wa uzinduzi wa Baraza la Vijana Unguja Ukuu Zanzibar.
Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu Kaepwani, Unguja Ukuu Kaebona na Unguja Ukuu Tindini wakifuatilia Uzinduzi huo wa Mabaraza yao.
Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu wakisoma Utenzi wa Uzinduzi wa Mabaraza yao ya Vijana katika Jimbo la Tunguu Zanzibar.
Mhe Simai Mohammed Said, Mkuu wa Wilaya ya Kati Unguja Mhe Mashavu Sukwa wakisikiliza utenzi wakati wa uzinduzi huo. 
Msanii wa Gogoti Mussa akionesha umahiri wao wakati wa uzinduzi huo.

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed SDaid akionesha dhana ya ushupavu na moyo wa ujasiri wa kucheza na chatu wakati wa Uzinduzi wa Mabaraza la Vijana wa Jimbo la Tunguu Shehia za Unguja Ukuu Kaepwani, Unguja Ukuu Kaebona na Unguja Ukuu Tindini uliofanyika katika viwanja vya Idumu Unguka Ukuu leo jioni..
Vijana wa Jimbo la Tunguu wakimpiga picha Mwakilishi wao wakati akicheza na Chatu katika hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana leo jioni katika viwanja vya Idumu Unguja Ukuu Zanzibar Wilaya ya Kati.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akimsalimia Msanii Mussa Nyoka baada ya kutowa burudani wakati wa hafla hiyo ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana la Jimbo hilo. 
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said, akiwa na simu wakati Mhe Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Anayeshughulikia Muungano Mhe. Januhuri Makamba akiongea na Wananchi akiwa Mjini Dodoma alikuwa ahudhuria uzinduzi huo wa Mabaraza la Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu Zanzibar na kutoa ahadi ya kuchangia shilingi milioni tatu kwa Shehia hizo Tatu za Unguja Ukuu Kaepwani. Unguja Ukuu Kaebona na Unguja Ukuu Tindini.
Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu wakimsikiliza Mhe Januari Makamba akizungumza na Wananchi wa Shehia hizo kupitia simu ya mkononi akiwa Mjini Dodoma akihudhuria Kikao cha Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kiongozi wa Mabaraza ya Vijana wa Unguja Ukuu akisoma risala ya Vijana wa Mabaraza ya Unguja Ukuu wakati wa uzinduzi huo. uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akihutubia Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu Zanzibar wakati wa Uzinduzi wa Mabaraza hayo uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja leo jioni.

Wazee wa Unguja Ukuu wakimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akizindua Mabaraza ya Vijana wa Jimbo lake uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya mpira vya Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu akihutubia wakati wa Uzinduzi huo wa Baraza la Vijana Unguja Ukuu Zanzibar.
Vijana wa Shehia za Ungujav Ukuu Wilaya ya Kati Unguja wakimsikiliza Mwakilishi wao Mhe. Simai Mohammed Said akiwahutubia. 
Mkuu wa Wilaya ya Kati Unguja Mhe Mashavu Sukwa akizungumza wakati wa hafla hiyo ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana Shehia za Unguja Ukuu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kati Unguja na Diwani wa Wadi ya Bungi Mhe Saidi Mtaji Askari, akizungumza wakati wa uzinduzi huo wa Baraza la Vijana wa Unguja Kuu Wilaya ya Kati Unguja. 
Mwenyekiti wa Vijana wa UVCCM Wilaya ya Kati Unguja Ndg Khamis Hamza Chilo, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo wa Baraza la Vijana Shehia ya Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Vijana wa Shehia ya Unguja Kuu wakimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akihutubia wakati uzinduzi huo.
Msanii wa Ngogoti akionesha umahiri wake wakati wa uzinduzi huo. akicheza na nyoka aina ya chatu
Wasanii wa Kikundi cha Sarakasi cha Bungi wakinesha umahiri wao.





Kikundi cha Wasanii wa Dance wa Bungi wakionesha umahiri wa kudance wakati wa hafla ya uzinduzi huo.

Sheikh Mohammed Suleiman akisoma dua baada ya kumalizika hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana Jimbo la Tunguu Wilaya ya Kati Unguja.

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar akizungumza nma Viongozi wa Mabaraza ya Vijana ya Shehia za Unguja Ukuu wakati wa kumalizika kwa hafla hiyo ya Uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya mpira vya Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
 Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.com
Zanzinews.com.

No comments: