Friday, October 14, 2016

ANATAFUTWA MBUNIFU JEZI MPYA ZA TIMU YA TAIFA


Shirikisho Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linaalika umma kuwania zabuni ya kubuni mwonekano mpya wa jezi mpya za timu ya taifa zitakazotumika kwa msimu wa 2017/18 na msimu wa 2018/19.


Kwa taarifa hii, TFF imefungua milango kwa umma ambako mtu mmoja mmoja anaweza kuwasilisha ubunifu wa mwonekano wa jezi hizo katika ofisi zake zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume ulioko kwenye makutano ya barabara za Uhuru na Shaurimoyo, Ilala jijini Dar es Salaam.

Wakati mwisho wa kupokea zabuni hizo ni Novemba 30, 2016, sharti kwa mbunifu ni kutoiga ubunifu kutoka makampuni makubwa ya vifaa vya michezo. Na Mbunifu Bora au Mshindi wa jezi ambazo zitakuwa lazima ziwe na nembo ya TFF na Bendera ya Taifa, atazawadiwa shilingi milioni mbili (Sh milioni 2).
Jezi za sasa za Timu ya Taifa ni rangi ya bluu kwa michezo nyumbani na nyeupe mechi za ugenini.

No comments: