Friday, October 21, 2016

KOROSHO GHAFI YAZIDI KUPANDA BEI MTWARA

Mbunge wa jimbo la Ndanda, Cecil Mwambe akizungumza na baadhi ya wakulima wa korosho  waliohudhuria mnada wa wazi katika ghala la Denyecha halmashauri ya mji Nanyamba wilaya ya Mtwara.Mbunge alikwenda kuwakilisha wakulima wa wilaya ya Masasi. (Picha na Haika Kimaro)
Baadhi ya wakulima wa zao la korosho waliohudhuria mnada wa wazi uliofanyika leo katika ghala la Denyecha halmashauri ya mji Nanyamba wilayani Mtwara.(Picha na Haika Kimaro)
 Na Mwandishi wetu,Habari24 Blog
Wakulima wa zao la korosho mkoani Mtwara leo wameendelea kushirikishwa katika mnada wa wazi na kupata fursa ya kuchagua bei juu kuliko zote jambo ambalo halikuwa likifanyika hapo awali.

Wakizungumza na Mtandao huu wakulima waliohudhuria mnada wa nne uliofanyika katika halmashauri ya mji Nanyamba wilaya ya Mtwata walisema kitendo cha minada kuwa wazi kitawawezesha kuboresha maisha yao ambapo kilo moja ya korosho ghafi imeuzwa kati ya Sh 3,762 hadi 3,805 ambapo ni sawa na tani 5,933 zimeuzwa.

Akizungumza mkulima Alhaji Mohamed alisema korosho kuwa na bei nzuri kutawasaidia kuinua uchumi wao na kuboresha maisha.
"Zamani tulikuwa hatushirikishwi kwenye mnada lakini sasa hivi tunakuwashirikishwa na bei imekuwa nzuri tunapata matumaini ya kuboresha maisha yetu kwasababu haijawahi tokea tangu nizaliwe,"alisema Mohamed

Naye Zuhura Hamis aliiomba serikali kuhakikisha wanawajengea viwanda vya kubangua korosho ili kuongeza ajira kwa vijana.
"Sasa bei ni nzuri kwasababu wakulima wenyewe tunashirikishwa moja kwa moja lakini tunaiomba serikali itujengee viwanda vya kubangua korosho zetu zikiwa hapa nyumbani ili kuongeza ajira pia, "alisema Hamis

Akizungumza Mbunge wa jimbo la Ndanda,Cecil Mwambe aliwataka wakulima kuvumilia wakati wakisubiri malipo yao badala ya kuuza korosho nje ya mfumo na kuibiwa.
Aidha aliwataka waendelee kushiriki katika minada  kuona yanayofanyika ili kuondokana na malalamiko yaliyokuwa yakitokea siku za nyuma.

Wakulima niendelee kuwasihi sana kuuza korosho zenu kwa mfumo wa stakabadhi ghalani msikubali kurubuniwa na watu wanaonunu kangomba kwasababu watakupa Sh 1,500 kwa kilo lakini pia kipimo chake sio halisi na yale malalamiko ya kupanga bei hayatakuwepo, "alisema Mwambe

No comments: