Monday, October 3, 2016

UMESKIA HII YA MTATIRO KUNASA MBINU ZA LIPUMBA MPYA,KIMO PIA KIKAO CHA LIPUMBA NA MSAJILI

 Ikiwa ni siku kadhaa tangu mwenyekiti wa chama cha wananchi cuf anayetambulika na msajili wa Vyama vya siasa nchini Profesa Ibrahumu Lioumba kufanya maamuzi ya kufukuza baadhi ya wakiurugenzi wa chama hicho hatimaye Menyekiti wa kamati ya uaongozi wa chama hicho Julius Mtatiro ameibuka na kufichua siri ya kufanyika kwa maamuzi hayo huku akimtuhumu Msajili wa vyama vya siasa kuendeleza kile anachokiita kukihujumu chama hicho.

Akizngumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Mtatiro ameeleza kuwa kuna kikao ambacho kiiliwakutanisha msajili wa vyama vya siasa Jaji Fransis ,Mutungi pamoja na Lipumba ambaye wamempachika jina la Bwana yule,kikao ambacho kilempa maelekezo kadhaa Lioumba kwa ajili ya kufanikisha kile wanachodai ni hujuma.
Amesema kuwa kabla ya kikao hicho Aliyekuwa Mbunge wa chama hicho ambaye alisimamishwa na Chama hicho Magdalena Sakaya ambaye yupo upande wa Lipumba alifika ofisini kwa msajili kupata maelekezo kuhusu ni jinsi gani Ruzuku ya chama hicho itaweza kuwafikia wao na sio chama jambo ambalo lilimfanya msajili kuitisha kikao na Lipumba kwa ajili ya kumpoa maelekezo kadhaa.


Akieleza maazimio ya kikao hicho ambacho wamedai kukifwatilia wamesema kuwa msajili alimuelekeza Mh Lipumba kuhakikisha anavunja uongozi wa chama hicho kwa kuanza na kufuta wakurugenzi hao na kuteua wengine wakurugenzi feki na mara baada ya kukamilisha zoezi hilo aitishe Baraza kuu feki lifanye maamuzi feki ya kuvunja Bodi ya wadhamini ambayo imeudwa na baraza kuu la Taifa la chama na mara baada ya hapo hili baraza lake ambalo wanaliita Feki lifanye kazi ya kuwadhibitisha hao wakurugenzi feki walioteuliwa na Mh Lipumba.
Mh Mtatiro ameendelea kuusema kuwa Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa imemhakikishia Profesa Lipumba kuwa kama akipita katika swala hilo la kuunda baraza kuu feki kitakachofwatia ni kazi ya msajili kutambua kila maamuzi yatakayokuwa yanatolewa na Baraza hilo la Mh Lipumba.

Kwa mujibu wa Mtatiro amewaeleza wanahabari kuwa Baraza kuu la chama hicho lipo moja lenye wajumbe 53 ambao ndio waliokutana Zanzibar  na kufanya maamuzi ya kumtimia uanachama mwanachama mwenzao Lipumba na wote waliohukuwa kwenye kikao hicho walisaini wajumbe 43 walioshiriki huku wengine kumi wakitoa udhuru maalum.

Amesema kuwa kwa mujibu wa katiba ya chama hicho Profesa Lipumba hata akitumia huo uenyekiti wake aliopewa hana uwezo wa kuitisha baraza kuu la Cuf kwa kuwa baraza kuu la chama lenye wajumbe 53 ndilo lililofanya maamuzi ya kumtimua uanachama wake ndani ya chama.

No comments: