Tuesday, October 11, 2016

WANAWAKE WA AFRIKA KUKUTANA KILIMANJARO MWEZI HUU KUJADILI CHANGAMOTO ZA MWANAMKE KATIKA SWALA LA ARDHI

Katikati ni Mkurugenzi wa mtandao wa Jinsia nchini Tanzania TGNP akizngumza na wanahabari wakati wakitangaza kufanyika kwa kongamano kubwa mwezi huu la ardhi la wanawake wa africa mlima kilimanjaro kongamano ambalo litafanyika mkoani Kilimanjaro,kulia kwake ni meneja kilimo na haki ya ardhi kutoka shirika la ActionAid ambao ni washirika katika kongamano hilo Bwana Elias Mtinda  na kushoto ni Mkurugenzi wa TAMWA Bi Gladness Munuo.Picha na Exaud Mtei(Msaka Habari)
 Wakati dunia ikiwa katika kipindi cha kuhakikisha kuwa usawa katika jamii kati ya wanawake na wanaume unafikia asilimia 50 kwa 50 nchini Tanzania imeelezwa kuwa ni asilimia 20 tu ya ardhi yote iliyosajiliwa inamilikiwa na wanawake huku wengi wao wakiwa  ni wale wanaoishi mjini jambo ambalo linawainua wanaharakati nchini Tanzania na kuamua kukutana kujadili kwa pamoja changamoto mbalimbali zinazowakumba wanawake katika swala zima la ardhi.
Mkurugenzi wa Miradi kutoka TAWLA ambao pia ni moja kati ya waandaaji na washiriki katika kongamano hilo la ardhi la wanawake Bi Masieku Kisambu akizungumza wakati wa mkutano na wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam wakati wa kutangaza kufanyika kwa kongamano hilo mkoani Kilimanjaro
Katika kuzingatia changamoto hiyo kubwa kwa wanawake ya upatikanaji,utumiaji na umiliki wa ardhi na rasilimali kwa kuzingatia kufanana kwa kiasi kikubwa kwa changamoto hizo katika ukanda wote wa Afrika,mashirika mbalimbali nchini wameandaa kongamano la ardhi kwa wanawake wa Afrika linalojulikana kama wazo la Kilimanjaro (Kilimanjaro initiative) kongamano ambalo limelenga kuleta sauti za wanawake wa Africa kwa pamoja ili kuwakilisha maadhimio ya wanawake wa Africa kuhusu nini wanataka katika kutetea mabadiliko yenye kuchochea maendeleo ya wanawake wa Africa ikiwemo Tanzania.
Meneja kilimo na haki ya ardhi kutoka shirika la Action Aaid ambao ni washirika katika kongamano hilo Bwana Elias Mtinda akisisitiza Jambo wakati wa mkutano huo.
Akizungumza na wanahabari mapema leo Mkurugenzi wa TGNP kwa niaba ya mashirika shiriki wa mkutano huo Bi Lilian Liundi amesema kuwa kongamano la ardhi la wanawake wa Africa Mlima Kilimanjaro litaanza tarehe 13-16 October 2016 ambapo linatarajiwa kuwa na washiriki Takribani 400 ambao ni wawakilishi wa wanawake walioko pembezoni toka katika kanda tano za Africa ambazo ni kanda ya nchi za Africa kusini,Africa ya mashariki,Africa ya kati,Africa ya kaskazini,na Africa mangharibi ambapo 30 miongoni mwao Tayari wamekwishaanza kupanda mlima Kilimanjaro kwa kusidio la kusimika madai yao juu ya ardhi kwenye kilele cha mlima.
 Mkurugenzi wa TAMWA Bi Gladness Munuo akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari Leo

Liundi amesema kuwa pamoja na changamoto nyingi wanazopitia wanawake wa Africa bado wameweza kuwa wazalishaji wakuu na pia kuendeleza vuguvugu la kujikomboa katika mifumo mbalimbali kandamizi ukiwemo mfumo dume hivyo kwa kutambua hilo na kusherekea jithada hizo wanawake hao wamechagua kupanda mlima Kilimanjaro ikiwa ni alama ya changamoto na ushindi pale unapofanikiwa kutika katika kilele cha mlima huo.
Ameongeza kuwa katika mkutano huo maazimio ya wanawake wa Afrika yatawakilishwa na wawakilishi wa wanawake kutoka kanda hizo tano za Africa na kukabidhiwa kwa wawakilishi viongozi wa nchi pamoja na mgeni Rasmi mualikwa toka umoja wa nchi za afrika pamoja na umoja wa mataifa.
Kongamano hilo litakalofanyika mkoani Kilimanjaro limeandaliwa na mashirika ya ActionAid Tanzania (AATZ),TGNP Mtandao kwa kushirikiana na International Land Coalition,Oxfam,Wildaf,na Institute for Poverty,Land and Agrarian studies (PLAAS).

Ros Sarwatt kutoka chama cha wanawake wajane Tanzania TAWIA akizngumza na wanahabari jinsi gani wanawake wajane wanapata matatizo ya ardhi nchini Tanzania.
Aidha katika hatua nyingine katika ngazi ya kitaifa wanawake Takribani mia moja wanakutana Jijiji Dar es salaam Jumatano ya tarehe 12 mwezi huu kesho kukabidhi madai yao kwa serikali ya Tanzania kupita Naibu waziri wa ardhi Mheshimiwa Mama Angelima Mabula ambaye ndiye atakuwa mgeni Rasmi katika tukio Hilo litakalofanyika katika viwanja vya TGNP.
Akizungumzia  Tukio hilo Liundi amesema kuwa madai hayo ya ngazi ya kitaifa yatajenga madai ya wanawake kikanda na hivyo kupeleka  sauti ya wanawake kwa Tanzania katika jukwaa kubwa la Africa.
PICHA ZAIDI CHINI---




No comments: