Thursday, December 1, 2016

JK KUZUIWA UWANJA WA NDEGE--SERIKALI YALIPA ONYO KALI GAZETI LA MTANZANIA

Jakaya Kikwete

Kufuatia gazeti la Mtanzania la Novemba, 20 na 22 kuandika habari ambazo zinamhusu Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kuwa alizuiliwa kuondoka katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Serikali imetoa taarifa kuhusu ukweli wa taarifa hiyo.
Katika taarifa ambayo imetolewa na Kaimu Msajili wa Magazeti, Patrick Kipangula imesema kuwa taaarifa hiyo haina ukweli na ina nia ya kumdhalilisha Kikwete ambaye aliondoka madarakani mwaka jana 2015 na nafasi yake kuchukuliwa na Rais wa awamu ya tano, Dk. John Magufuli.
Hivyo kutokana na kuchapishwa kwa habari hizo, Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Magazeti imetoa onyo kwa gazeti la Mtanzania na kuvikumbusha vyombo vya habari kuzingatia maadili ya uandishi ya habari.
1e504b16-a8c4-4f31-985f-d3bd4f01e8aa

No comments: