Friday, December 9, 2016

Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote Lafana Mjini Songea

Msanii Elias Barnaba akiwa kwenye Jukwaa la Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea usiku wa kuamkia jana


Mr Blue akitoa Burudani kwenye Jukwaa la Tigo Fiesta Songea

Kutoka Temeke Chege Chigunda akiwapa burudani mashabiki wa Tigo Fiesta waliojitokeza uwanja wa Majimaji Songea




Luli Diva Jukwaani

Mkali wa Nyimbo ya Kinanda Messen Selecta  akitoa Burudani

Wasanii waliopanda jukwaa la Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote kwenye uwanja wa Majimaji Songea usiku wa kuamkia jana kwa pamoja wakiweka mishumaa juu kumkumbuka Mtayarishaji wa muziki Joshua Magawa a.k.a Pancho Latino aliyefariki hivi karibu kwenye kisiwa cha Mbudya jijini Dar Es Salaam

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe.Pololite Mgema akiongea na wanachi waliojitokeza kwenye Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea usiku wa kuamkia jana. Pembeni ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Christina Mndeme ns Mratibu wa Tamasha hilo Shafii Dauda.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Christina Mndeme akiongea na wananchi waliojitokeza kwenye Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea usiku wa kuamkia jana.


Mkali wa Wowowo Zaiid akitoa Burudani kwenye Tamasha la Tigo Fiesta  Songea.


Likiwa limeingia mkoa wanne Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote limefana na kuacha alama kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani  Ruvuma usiku wa kuamkia jana, Kabla ya kuingia mkoani humo Tamasha hilo lililoanzia Mkoa wa Morogoro limepita  mikoa ya Rukwa, Iringa, Songea na kuelekea Mtwara jumapili hii.

Akifungua Tamasha hilo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Christina Mndeme aliyeongozana na mkuu wa wilaya ya Songea Mjini Mhe. Pololite  Mgema alisema Tunawashukuru Kampuni ya Tigo na Clouds Media kwa kutuletea tamasha hili kubwa mkoani kwetu. “ Hii si kwa burudani pekee bali ni fursa kwa wakaazi wa mkoa huu kwa kuwawezesha kwa kuwaongezea kipato kwa kipindi hiki chote cha wiki nzima”. Niendelee kuwapongeza tena Tigo  na Clouds Media na kuwaomba mwakani msiache kuja tena kwenye mkoa wetu.

Kwa upande wa burudani, ilianza kwa kumpata mshindi wa shindano la kusaka vipaji la Tigo Supa Nyota kwa kumuibua Msanii Single Baba atakayeiwakilisha Ruvuma kwenye fainali zitakazofanyika jijini Dar Es Salaam mwezi ujao.

Shoo rasmi ilianza kwa Msanii Mesen Selekta kufuatiwa na Rubby huyu ni msanii aliyeibuliwa kwenye Supa Nyota miaka kadhaa iliyopita, kwa kweli ni msanii wa aina yake aliweza kuteka hisia za mashabiki kwa kuimba nyimbo tofauti tofauti zikiwemo Niwaze,Ntade, Na Yule,Forever na nyingine.

Jumla ya wasanii kumi na mbili walipanda jukwaani wakiwemo Rostam, Weusi, Ruby, Mr. Blue, Barnaba, Zayd, Fid Q, Masen Selekta,  Lulu Diva,Chege, Foby ambao wasanii hao ndio watapanda kwenye jukwaa jumapili uwanja wa Nangw’anda Mtwara.

Mdhamini mkuu wa msimu huu, kampuni ya Tigo imewakumbusha mashabiki wote wa muziki mjini Sumbawanga kufurahia promosheni zake tatu murwa katika msimu hii wa vibes. ‘Data Kama Lote inawapa wateja hadi mara mbili ya vifurushi vya intaneti watakavyonunua kupitia menu iliyoboreshwa ya *147*0#. Hii itawawezesha wateja wa Tigo kufurahia msimu huu wa vibes kupitia mtandao wa kasi ya juu zaidi wa Tigo 4G+.

Tigo pia inatoa punguzo kubwa la bei kwa tiketi za tamasha la Tigo Fiesta 2018 zitakazonunuliwa kupitia Tigo Pesa Masterpass QR. Kwa Sumbawanga, tiketi zitakazonunuliwa kwa mfumo wa Tigo Pesa Masterpass QR zitagharimu TSH 5,000 pekee badala ya TSH 7,000 kwa watakaonunua kwa pesa taslim, Wateja wanapaswa kupiga *150*01#  na kuchagua 5 (lipia huduma) kisha kuchagua namba 2 (lipa Masterpass QR) na kutuma kiasi husika kwenda namba ya Tigo Fiesta 78888888.

Wateja wa Tigo pia watapata faida zaidi kupitia shindano la Tigo Fiesta 2018 – Chemsha Bongo Trivia linalotoa zawadi za kila siku za TSH 100,000, zawadi za kila wiki za TSH 1 milioni, simu janja za mkononi zenye thamani ya TSH 500,000 kila moja, pamoja na donge nono la TSH milioni 10 kwa mshindi wa jumla. Kushiriki wateja wanapaswa kutuma neno MUZIKI kwenda 15571 au kutembelea tovuti ya  http://tigofiesta.co.tz na kuchagua Trivia.


Huu ni mwaka wa 17 wa tamasha la muziki na kitamaduni la Tigo Fiesta 2018 – Vibe Kama Lote ambapo mwaka huu linashirikisha 100% wasanii wa nyumbani watakaozuru mikoa 15 ya nchi ikiwemo; Morogoro, Sumbawanga, Iringa, Singida, Songea, Mtwara, Moshi, Tanga, Muleba, Kahama, Mwanza, Musoma, Arusha na Dodoma, huku kilele kikifanyika Dar es Salaam.

No comments: