Friday, September 30, 2016

SERENGETI BOYS SIO WA MCHEZO MCHEZO--TIZAMA MAZOEZI YAO WAKIJIANDAA KUIANGAMIZA CONGO


Huyo ndiye Muhsin Malima Makame au unaweza ukamwita ‘Super Sub’ wa Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 - Serengeti Boys, akikokota mpira kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Alphonse Massamba-Débat - Rais wa zamani wa Congo kuonyesha uwezo wake uwanjani pindi anapoingia kipindi cha pili kuokoa jahazi. Akikosa kufunga huwa ni kama bahati mbaya.

Beki wa kushoto wa Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 - Serengeti Boys, Nickson Kibabage akimdhibiti Kelvin Nashon wakati wa mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika leo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Alphonse Massamba-Débat - Rais wa zamani wa Congo kabla ya mchezo wa Jumapili. 

Mashindano ya Tigo Igombe Marathon kulindima jumapili hii



Meneja  Mauzo wa Tigo mkoani Tabora, Bright Kisanga(kushoto) akiongea na wanahabari jana wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Igombe marathon yatayofanyika jumapili mkoani Tabora. Wengine ni Amon Mkoga Mratibu wa mashindano na katibu wa chama cha riadhaa mkoani Tabora, SalumTaradadi. Kampuni ya Tigo ndio mdhamini mkuu wa mashindano hayo.
Mratibu wa mashindano ya Igombe Marathon, Amon Mkoga(katikati) akionesha kombe na medali kwa washindi wa Igombe marathon kwa wanahabari wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo jana,Wengine pichani kushoto Meneja Mauzo wa Tigo mkoani Tabora, Bright Kisanga na katibu wa chama cha riadha  mkoani humo Salum Taradadi.
Mratibu wa mashindano ya Igombe Marathon, Amon Mkoga(katikati) akiongea na wanahabari wakati wa uzinduzi wa mashindano hayo jana,Wengine pichani kushoto Meneja Mauzo wa Tigo mkoani Tabora, Bright Kisanga na katibu wa chama cha riadha  mkoani humo Salum Taradadi.
Msanii akicheza na Nyoka wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Igombe marathon
28 Septemba 2016 Tabora, Kampuni ya simu za mkononi Tigo Tanzania  ikishirikiana na kampuni ya Chief promotions imetangaza rasmi kwamba  tarehe 02/10/216  kampuni ya Chief Promotions imendaa mbio za kila mwaka kwa jina la Tigo Igombe Marathon.

LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA WIKIENDI HII


Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) inaendelea leo Septemba 30, 2016 kwa mchezo mmoja tu, unaozikutanisha timu za Toto Africans na Ndanda ya Mtwara katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

BENKI KUU YA TANZANIA YASEMA PATO LA TAIFA LIMEONGEZEKA KWA ASILIMIA 7.9

 Kaimu Meneja Kitengo cha Mahusiano kwa Umma wa BoT, Victoria Msima, akimkaribisha  Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu (wa pili kushoto), kuzungumza na wanahabari kuhusu ukuaji wa pato la taifa kwa robo na nusu mwaka 2015 Dar es Salaam leo.
 Taswira ya meza kuu katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Kaimu Meneja Kitengo cha Mahusiano kwa Umma, Victoria Msima,Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mabenki,  Kenedy Nyoni, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Beno Ndulu na Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti wa Sera za Kiuchumi, David Kwimbere.
 Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandshi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa taarifa ya ukuaji wa pato la taifa kwa robo na nusu ya mwaka 2016. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mabenki,  Kenedy Nyoni.
 Wapiga picha wakiwa kazini.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mwanahabari Samuel kutoka kituo cha Televisheni ya ESTV akiuza swali

TIZAMA LIPUMBA ALIVYOTINGA CUF SAA MBILI ASUBUHI KUMSUBIRI MAALIM SEIF,HAJATOKEA


 Hali ilivyokuwa katika makao makuu ya chama cha wananchi Cuf majira ya asubuhi ya saa mbili leo ambapo Mwenyekiti wa chama hicho anayedaiwa kutimuliwa uawanachama akiwasili ofisini kwake baada ya kuwepo Taarifa za ugeni kutoka zanzibar ukiongozwa na Katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad ambapo alitarajiwa kuwasili katika ofisi hizo baada ya kutoka katika kikao cha baraza kuu walioamua kumtuimua Lipumba juzi.

Akizngumza na wanahabari mapema asubuhi hiyo amewaeleza wanahabari kuwa Hana Taarifa zozote za kuwa na ugeni huo lakini Ndani ya makao makuu hayo kuna Ofisi za katibu mkuu wa chama hivyo haonijambo la ajabu kama anakuja ofisini kwake na anamsubiri kwa hamu ili ampe mikakati na mipango ya chama inavyokwenda kwa ajili yab kukuza chama chao.

Ameasema kuwa yeye na maalim Seif hawana ugomvi kama inavyoelezwa katika vyombo vya Habari bali kinachowachanganya watu ni yeye kufwata katiba ya chama ambayo imemtruhusu kurudi madarakani baada ya kujiulzuli mwaka jana.

Amesema kuwa anashangwazwa kusikia kuwa Ktibu mkuu wake anaenda kuomba Ulinzi kwa polisi kwa ajili ya kuja ofisini kwake wakati yeye ana walinzi wa serikali,ana walinzi wa chama na hakina mtu anayeweza kuleta fujo kwa kuwa chama hipo chini ya ulinzi mkali wa walinzi wa chama hicho

Hadi tunaondoka eneo la tukio Maalim Seif hakuwa amefika katika ofisi hizo na hali ilikuwa swari

Breaking Nwezz---UKUTA WAFUTWA RASMI HAUPO TENA,HIZI NI MBINU MPYA ZA UKAWA WALIZOZITAJA MUDA HUU

 Chama cha democrasia na maendeleo chaema hatimaye leo kimatangaza kufuta rasmi maandamano na mikutano ya hadhara iliyokuwa imepewa jina la UKUTA na abadala yake wameamua kutumia mbinu nyingine walizozitaja kuwa bira zaidi za kufikisha ujumbe waliokusudia kufikisha kwa serikali.

Akizngumza na wanahabari mapema leo Mwenyekiti wa chama Taifa Mh Freman Mbowe amesema kuwa Baada ya kuspgeza mbele maandamano hayo na kuwapa nafasi viongozi wa Dini kulifanyia kazi swala hilo hatimaye wamegundua kuwa hakuna chochote kilichofanyika ambapo ni haki yao kuendeleaza Fikra za UKUTA kwa kuwa wametumia kila mbinu kulimaliza lakini imeshindikana.

Amesema kuwa Swala la kudai Haki za msingi sio swala la siku moja hivyo Fikra za kudai haki na operation UKUTA zinendelea kudumu na kutumia mbinu nyingine mpya kwa ajili ya kudai haki ya kidemocrasia ambayo imeminywa nchini.

Akieleza mbinu hizo mpya amesema kuwa chama sasa kimeanza ziara za kwenda katika mataifa ya ulaya na jumuiya za ulaya kuwaeleza nkile abacho kinaendelea nchini Tanzania na kufanya ikutano mbalimbali kuonyesha hali halisi ambapo kwa kuanza na hili kundi la kwanza la viongozi wakuu wametoka Ujerumani kufanya hivyo na ziara Hizo zitakuwa nyingi Zaidi.

Njia nyingine amesema kuwa wameamua kufungua kesi mbalimbali na nyingi katika mahakama za ndani na nje kwa ajili ya bkupinga yale abayo hayaendi sawa katika taifa kwa sasa ikiwemo kuminywa kwa Democrasia ya nchi.
NUKUU
Kuhusu ukuta tulikubaliana kuwapa muda viongozi wa dini kufanyia kazi hilo.
Jana tulikutana tena kupata mrejesho wa swala hilo.
Taarifa ambazo kamati maalum ya kamati kuu imepewa taarifa kuwa vingozi wa dini hawakufanya lolote hatuna taarifa.
Sisi kama chama cha siasa tuliwsheshimu na tutaendelea kuwaheshimu sana ila ni wajibu wetu sasa kuendelea na haraksti zetu
Baada ya kuona mambo kadhaa yalitopo tumeona kusitisha maandamano ya October moja na kupisha mbinu nyingine mpya
Tukio la kudai haki sio tukio la Siku moja kama wengi wanavyodhani.
Kwa umuhimu wa hali hiyo chama kilituma Ujumbe maalum Ulaya kuielezea Jamii ya kimataifa ugandamizaji unaoendelea nchini.
Bado misafara mingine ya chama itaendelea kwenda nchi nyingi zaidi kufanya mikutano na kuzitaka jumuiya nzima za kimaraifa waelewa kuwa tanzania ile Amani haipo tena
Tunaendelea na maandalizi ya kufungua kesi mbalimbali kuhusu yanayoendelea nchini.
TAKE NOTE....UKUTA  WA OCTOBER MOJA UMEFUTWA RASMI WAMETANGAZA KUFANYA MBINU NYINGINE.
Kuhusu sakata la Lipumba na Cuf Mbowe anasema ----.....Lipumba ni political relevant amepoteza kisiasa.ni wakala wa wasaliti wenzake.tunampuuza maana kuendelea kumjadili ni kumpa nafasi ambayo alikuwa nayo zamani.sisi tutaendelea kushirikiana na Cuf na kuheshimu vikao vyake halali.

Kuhusu Report ya Twaweza anasema kuwa nao wamejitwishwa uwendawazimu.ni mtanzania mwendawazimu pekee anayeweza kuiamini report yao.eti serikali inakubalika kwa asilimia 95 ni uwendawazimu Mkubwa sana.Twaweza wanaandaliwa report na serikali.wanalipwa na serikali.hawawezi kuja na fact

Thursday, September 29, 2016

GHAFLA--MAPOKEZI YA MAALIM SEIF DAR ES SALAAM YAMEFUTWA


Kwa mujibu wa Taarifa ambayo mtandao huu imeinasa kwenye ukurasa wa Mwenyekiti wa Muda wa chama hicho JULIUS MTATIRO imeleeza kuwa mapokezi hayo yameahirishwa kwa  muda.

MAALIM SEIF APANGA KUANZIA KWA IGP MANGU KUMSHTAKI LIPUMBA KESHO KABLA YA KUTINGA BUGURUNI

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, atatua ofisini kwa kiongozi mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu, ili kumueleza mkakati wake wa kutua ofisini kwake, Buguruni jijini Dar es Salaam

Maalim anakwenda kwa IGP Mangu kumueleza adhima yake ya kufika ofisi kuu ya chama chake kesho Ijumaa, majira ya saa mbili asubuhi.

Hatua ya Maalim kutinga ofisini kwa IGP imetokana na kitendo cha jeshi la polisi kumsindikiza Prof. Lipumba kurejea ofisini; kusaidia uharibifu wa mali na kushambulia wanachama na wafuasi wa chama hicho.

ZIMWI LA TEGETA ESCROW LAMTISHA PROFESA TIBAIJUKA, AKATAA KUPOKEA DOLA 300,000 BAADA YA KUPEWA TUZO YA KIMATAIFA

 Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka akionesha tuzo ya kimataifa (UN) ya Maendeleo Endelevu ya Mwana Mfalme Khalifa Bin Salman Al Khalifa aliyotunukiwa hivi karibuni New York Marekani wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo.
 Profesa Anna Tibaijuka akionesha cheti alichokabidhiwa sanjari na tuzo hiyo.
 Profesa Tibaijuka akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari. Kulia ni Mratibu wa mkutano huo, Mussa Ally.
 wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

HATMA YA OPERATION UKUTA KUJULIKANA KESHO


Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari leo wametutafuta wakitaka kujua au kupata taarifa kutoka CHADEMA juu ya mambo mawili.

1. Evergreen story na updates (rasmi) kuhusu Operesheni UKUTA na hatima siku ya maandamano na mikutano nchi nzima iliyotangazwa na chama.
2. Maoni au mtizamo wa CHADEMA kuhusu Ripoti ya Utafiti wa Taasisi ya Twaweza iliyotolewa leo juu ya maoni ya watu kuhusu UKUTA;

TAIFA STARS WATAKAOIVAA ETHIOPIA HAWA HAPA


Kocha Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), Charles Boniface Mkwasa ametaja majina ya nyota 24 watakaounda kikosi ambacho kitasafiri mwishoni mwa wiki ijayo kwenda Addis Ababa, Ethiopia kucheza na wenyeji wetu kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaofanyika Oktoba 8, mwaka huu.

MRADI WA URASIMISHAJI ARDHI UBUNGO WAINGIA MIZENGWE WATENDAJI WATISHIA KOGOMA KWA KUKOSA POSHO

Waziri wa Ardhi, William Lukuvi



Na Dotto Mwaibale

WATENDAJI na vibarua wanaofanya kazi ya kupima ardhi katika mradi wa urasimishaji wa ardhi katika maeneo yaliyojengwa kiholela katika Kata ya Kimara 

wilayani Ubungo umeingia mdudu baada ya kutishia kugoma kutokana na kutolipwa fedha za posho ya kazi hiyo kwa zaidi ya miezi mitatu.

Hatua hiyo imefikiwa baana ya kuona baadhi ya vongozi wanaosimamia mradi huo wa kuanza kujinufaisha wenyewe na kuwanyonya watendaji wakiwemo vibarua 

hao.


Wafanyakazi wa upimaji wa ardhi kutoka wizarani na vibarua hao wakiongea kwa nyakati tofauti na gazeti hili kwa masharti ya kuto andikwa majina yao gazetini 

wamesema  viongozi hao kupitia mradi huo wamejenga mazingira ya  kujinufaisha kupitia fedha zilizotoka Benki ya Dunia kufanya mradi huo.


"Tunachangamoto kubwa ya kupata fedha za malipo kwa kazi tunayoifanya tumefanya kazi miezi minne lakini tumelipwa mwezi mmoja tu na si sisi peke yetu na hata 

watendaji wa wizara wanaofanya kazi hii nao hawajalipwa wakati fedha zipo " alisema mmoja wa vibarua hao.


Kibarua huyo alisema kuwa kuna mmoja wa kiongozi wa wizara hiyo anayesimamia mradi huo ndiye kikwazo kikubwa cha mradi huo na jitihada za makusudi 

zisipochukuliwa mradi huo hautafikia malengo yake.


“Binafsi acha niseme ukweli mradi huu ulianza vizuri lakini sasa utakwama kwani viongozi waliopo pale wizarani wameanza kutumia fedha vibaya na hawataki kutupa

licha ya fedha za mradi kuwepo na tunapowadai wanasema eti Rais John Magufuli hajaidhinisha fedha hizo wakati sio kweli" alisema mtendaji mwingine wa 
mradi huo kutoka wizarani.


Mtendaji huyo alisema changamoto hiyo yakutopewa fedha zao imewapunguzia mori wa kazi hivyo kuingia mashaka kama mradi huo utakwisha.




“Kiukweli ndugu mwandishi hapa watu wanaishi kama ndege wafanyakazi kila kukicha ila hawajalipwa mwezi wa tatu, ukiangalia kwa sasa wanasema eti hela zao 

zimetoka ila wanalipwa siku 20 wakati mwezi unasiku 30 sasa hizo hela zinazobaki za siku 10 viongozi wanazipeleka wapi? kama si wizi wa macho macho" alihoji 
mtendaji huyo.


Mtendaji huyo aliongeza kuwa jambo hilo limekuwa ni janga kwani watendaji wa mradi huo wapo zaidi ya 50 sasa anapokatwa siku 10 kila mmoja anapata 

shilingi ngapi hanazikosa na fedha hizo zinapelekwa wapi.


Akizungumzia changamoto hiyo Diwani wa Kata ya Kimara ambapo mradi huo upo, Pascal Manota alikiri kwa watendaji hao kutolipwa fedha hizo na tayari amekwisha 

mjulisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi juu ya changamoto hiyo.


"Changamoto kubwa ipo kwa viongozi wa wizara waliopewa kufanyakazi hiyo fedha zipo lakini hawawalipi watendaji hali inayozoofisha mradi huo tunamuomba 

waziri aliangalie suala hilo kwa karibu kabla ya mambo kuharibika" alisema Manota.


Manota alisema watendaji hao wa serikali hivi sasa wapo tu ofisini wakisoma magazeti hawana ari ya kazi hali hii imechangiwa na viongozi hao wasiokwenda na kasi ya Rais wetu Dk. John Magufuli ya hapa kazi tu.



Jitihada za gazeti hili za kumpata mratibu wa urasimishaji wa ardhi wa wizara hiyo ambaye anasimamia mradi huo, Lydia Bagenda zilishindikana baada ya kwenda 

ofisini kwake na kuambiwa alikuwa nje ya ofisi kikazi na hata halipopigiwa simu mara kadhaa simu yake ilikuwa imefungwa.

TIGO YAWAKUMBUKA WAHANGA WA TETEMEKO MKOANI KWA KUTOA SARUJI MIFUKO 2424


Mkurugenzi wa Mtandao wa Tigo kanda ya ziwa Ali Mswanya(kulia) akizungumza mkoani Kagera alipomkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu(kushoto)sehemu ya mifuko ya saruji 2424 yenye thamani ya Sh 40 Milioni ,kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu(kushoto) akipokea sehemu ya mifuko ya saruji 2424 yenye thamani ya Sh 40 Milioni kutoka kwa Mkurugenzi wa Mtandao wa Tigo kanda ya ziwa Ali Mswanya,kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Kijuu(kulia) akipeana mkono na Mkurugenzi wa Mtandao wa Tigo kanda ya ziwa Ali Mswanya alipomkabidhi sehemu ya mifuko ya saruji 2424 yenye thamani ya Sh 40 Milioni ,kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera,wa pili kulia ni Meneja wa Tigo Mkoani humo Sadock Phares.

MPYA KUTOKA SIMBA NA MO WAO ASUBUHI HII KUELEKEA JUMAMOSI



Klabu ya Simba inayo furaha kubwa ya kutangaza kumshukuru mlezi wake bwana Mohammed Dewji kwa kuanza kutekeleza ahadi zake kwa vitendo.
Dewji maarufu kama MO tayari ameshaanza kulipia mishahara ya wachezaji,benchi la ufundi na Sekretarieti ya klabu na atafanya hivyo katika kipindi chote cha mpito kuelekea mabadiliko ya kimuundo ya klabu.
Mbali ya hayo mfanyabiashara huyo mkubwa barani Afrika atalipia kodi za nyasi bandia na gharama nyingine za uendeshaji wa klabu.

ALIYEIMBA WIMBO WA DIKTETA UCHWARA MBARONI

1
Mwanamuziki wa Bongo Fleva Fulgency Mapunda maarufu Mwana Cotide amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kwa tuhuma za kuimba na kusambaza wimbo wenye maudhui ya kichochezi.
Mwana Cotide ameiamba wimbo wenye jina “Dikteta Uchwara” ambao aliusambaza kupitia mtandao wa YouTube kitu ambacho kinavunja sheria ya makosa ya mitandao.
Akisoma mashtaka hayo, mwanasheria Derrick Mukabatunzi alisema kuwa Mwana Cotide na mtayarishaji wa muziki huo, Mussa Kibakwe walitenda kosa hilo mwezi Agosti 2016 eneo la Manzese Dar es Salaam.
Watuhumiwa wote wawili walikataa mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana. Kesi hiyo imetajwa kusikilizwa tena Oktoba 12.

CELINA PATEL BINTI WA MIAKA 11, AIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA KIMATAIFA YA AFRICA LIGHTING GOLDEN GOLF TOURNAMENT MKOANI ARUSHA.


Mtanzania Celina Patel binti wa miaka saba ameibuka kidedea katika mashindano ya Africa Lighting Golden Jubilee Golf Tournament yaliyofanyika mkoani arusha.

Mashindano hayo ambayo yaliwakutanisha washiriki kutoka kutoka nchi mbalimbali duniani pamoja na nchi wanachama wa jumuhiya ya afrika mashariki  ambapo mtanzania Celina Patel aliibika kuwa mshindi wa kwanza.

Kufatia Ushindi huo  Celina Patel ambye kwa kipindi kifupi ameweza kushinda medani nyingi umeleta heshima kubwa  kwa watanzania na Taifa kwa ujumla hasa katika mchezo wa golf. 

Pia Ushindi huo utakuwa chachu katika kulitangaza taifa hususani  kwa wapenzi wa mchezo huo dunia, jambo ambalo litasaidia pia kuitangaza nchi katika medani ya kimataifa hasa kupitia michezo. 

Aidha Celina Patel Ameibuka mshindi katika category mbalimbali kama Ladie Winner at Africa Lighting Golden Jubilee Golf Tournament Arusha, Junior Prize winner at Muthaiga junior Open Golf Tournament Kenya pamoja na Winner of Bronze Division at Mombasa Ladies open Golf Tournament.

Pia ni mshindi katika category ya  Junior Winner at Tanzania Open at kili golf, Winner of Women’s category in kilimanjaro Spurs Golf Tournament.
Tangu Mheshimiwa Rais ameingia madarakani,  watanzania wengi wamekuwa wakifanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya ndani na nje ya nchi

Kufatia ushindi huo ni wazi kuwa Tanzania imechukua ubingwa huo wa dunia hivyo pongezi kwa jitihada zake na kuliletea taifa ushindi huo , pia kumtakia kila la kheri katika michezo na taaluma kwa ujumla, pamoja na kukutakia Afya njema ili uzidi kuwakilisha Taifa.

SERENGETI BOYS HAWATAKI UJINGA UJINGA--TIZAMA WALIVYOWASILI CONGO KUMALIZA KAZI

Baadhi ya wachezaji wa Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 - Serengeti Boys, wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Maya Maya mara baada ya kutua leo wakitokea Kigali nchini Rwanda walikopiga kambi kabla ya kuwavaa vijana wenzao wa Congo, Jumapili ya Oktoba 2, 2016 kwenye dimba la Massamba Sebat, Brazzaville.  Timu hiyo imefikia Hoteli ya Michael’s iliyopo Barabara ya Nelson Mandela jijini hapa. Kikosi hicho kimetua salama salmin kujindaa kuifumua Congo Jumapili. (Picha na Alfred Lucas wa TFF). 

Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla afanya ziara Wilaya za Buhigwe na Uvinza Mkoani Kigoma


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya za Uvinza na ile ya Buhigwe na kutembelea Hospitali na vituo vya Afya ndani ya Mkoa huo wa Kigoma.
Akiwa katika kituo cha Afya cha Uvinza,  Naibu Waziri  ameweza kubaini mapungufu mbalimbali huku na kutoa maagizo kwa wasimamizi wake kuhakikisha wanafanyia marekebisho kasoro hizo kwa muda unaotakiwa kabla ya kuchukuliwa  wahusika.
Miongoni mwa kasoro  alizobaini ni pamoja na kuwa kituo hicho licha ya kuhudumia wananchi kama Hospitali ya Wilaya ya Uvinza, hadi sasa  hakina sifa hiyo kwani  hakina Chumba cha upasuaji, Maabara hisiyofuata utaratibu pia kutokuwa na maji kwa kituo hicho maji ambayo wanategemea kutoka kwa wagonjwa.

“Kituo cha Afya Uvinza, kinahudumia eneo lenye watu zaidi ya 59,000. Walipaswa kuwa 10,000 tu. Hakina maji, umeme Kwa sababu zisizo za kawaida. Hakuna Chumba cha upasuaji (Theatre), maabara ya kusuasua na dawa si za kutosha.
 Nimewaagiza ndani ya miezi mitatu wawe wamekarabati eneo nusu la wodi ya wanaume kiasi cha kuweka  Chumba cha Upasuaji.  Pia wavute maji na kuweka matenki juu ili kuepukana na tabia ya kuagiza wajawazito kuja na ndoo za maji kituoni!.  Nimewapa mwezi mmoja ili wavute umeme na kuanza kutumia Vifaa vyao Vya maabara.” Amesema Dk.Kigwangalla wakati wa kutoa maagizo yake hayo kwa viongozi wa Serikali na wa Hospitali hiyo.
Aidha, kwa upande wa ziara yake katika Wilaya ya Buhigwe, Dk. Kigwangalla alipongeza juhudi za wabia binafsi kwa kuweza kushirikiana na Serikali kwenye jambo la maendeleo huku akiwahakikishia uongozi wa Hospital ya Wasabato ya Heri Mission  iliyopo eneo la Manyovu  kuwa juhudi zao wanazitambua na suala la kuifanya Hospitali hiyo kuwa Hospitali teule ya Wilaaya zinashughulikuwa huku akiwataka kuzingatia sheria mbalimbali na mambo madogomadogo.
Dk. Kigwangalla ameutaka uongozi wa Wilaya hiyo kuhakikisha wanafanyia marekebisho ya barabara inayoingia Hospitalini humo pamoja na kuhakikisha wanajenga vituo zaidi vya  Afya ili kuwafikia wananchi wake.
Dk. Kigwangalla yupo Mkoani hapa  kwa ziara ya siku ambapo pia atatembelea Hospitali na vituo vya  Afya vya Kigoma Mjini.
mwisho.

Wednesday, September 28, 2016

TAARIFA YA KATIBU MKUU JUU YA UPATIKANAJI WA DAWA


SSRA YAWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII NCHINI

 Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole (kushoto), akitoa ufafanuzi mbalimbali kwenye semina ya siku moja ya wanahabari kuhusu mifuko ya jamii Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji, SSRA, Sarah Kibonde.
 Mkurugenzi wa Tafiti, Sera na Tathmini wa SSRA, Ansgar Mushi akitoa mada katika warsha hiyo.
 Waandishi wa habari wakiwa katika semina hiyo.
 Waandishi wakiwa kwenye semina hiyo
 Semina ikiendelea.
 Waandishi wa habari wakichukua mambo kadhaa kwenye semina hiyo.
 Wanahabari wakiwa makini katika semina hiyo.
 Maswali yakiulizwa.
 Taswira meza kuu katika semina hiyo.

Picha ya pamoja waandishi wa habari na maofisa wa SSRA.