Monday, October 31, 2016

Serikali Kuhakiki Vyeti vya Ndoa,Magufuli afichua siri Kenya,Kifo cha Bondia Mashali Utata Mtupu,Soma Magazeti ya leo Nov 1,2016

LOWASSA,SUMAYE WAWEKA KAMBI DODOMA KUTETA NA WABUNGE WA UKAWA KUNUSURU WAANDISHI WA HABARI TANZANIA


Mawaziri Wakuu wa zamani ambao ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa na Frederick Sumaye wameweka kambi mjini Dodoma ili kuteta na wabunge wa Ukawa. 

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema kuwa wanasiasa hao wako mjini humo kwa ajili ya kufanya vikao na wabunge wa Ukawa ili kuweka mkakati na msimamo dhidi ya hoja mbalimbali zinazotarajiwa kuibuliwa katika vikao vya Bunge vinavyoanza kesho. 

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEJI WAKE RAIS UHURU KENYATTA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakiongozana kwenye Ikulu ya Nairobi Oktoba 31, 2016. Rais yuko nchini Kenya kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. (PICHA NA IKULU)

POLISI WAZUIA MKUTANO WA MAALIM SEIF ULIOKUA UFANYIKE TANGA,........WAMLINDA PROFESA LIPUMBA

Wakati polisi ikizuia mkutano mkuu maalumu wa CUF uliopangwa kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad mjini Tanga jana, mwenyekiti anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba alifanya usafi soko la Buguruni, huku akilindwa na jeshi hilo. 

Lipumba alifanya kazi hiyo akitekeleza agizo la Rais John Magufuli la kufanya usafi Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi. Msemaji wa CUF, Abdul Kambaya alisema haoni kama ni jambo la ajabu kwa Lipumba kufanya usafi wakati akilindwa.

“Sioni mantiki ya swali hilo, suala la kulindwa Lipumba siyo wa kwanza,” alisema 

RAIS DKT MAGUFULI AWASILI NCHINI KENYA,APOKELEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS UHURU KENYATTA

key1
Rais Dkt John Pombe Magufuli, akilakiwa na Mwenyeji wake, Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta alipokaribishwa Ikulu, Nairobi nchini Kenya leo. Rais Magufuli yupo nchini Kenya kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

key3
Rais Dkt John Pombe Magufuli akikagua gwaride la Jeshi la Kenya, alipowasili Ikulu jijini Nairobi leo.
key6
Rais Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Naibu Rais wa Kenya, Mh. Willam Ruto.
key5
Rais Dkt John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mwenyeji wake, Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta, alipowasili Ikulu ya Kenya, Jijini Nairobi leo.
key4
key2
Rais Dkt John Pombe Magufuli (kulia) akiwa na Mwenyeji wake, Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta wakipokea salamu za kijeshi, katika viwanja vya Ikulu ya Kenya, Jijini Nairobi leo.

HAYATOU AMTEUA MALINZI KAMATI YA MAGEUZI CAF

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika, Issa Hayatou ameteua Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kuwa miongoni mwa wajumbe 11 wa Kamati maalumu ya mageuzi ya muundo wa CAF itakayokuwa na jukumu la kufanya mabadiliko mapya ya shirikisho, imefahamika.

LIGI YA TAIFA WANAWAKE KUANZA RASMI KESHO

Ligi ya Taifa ya Wanawake inatarajiwa kuanza kesho Jumanne Novemba 1, 2016 kwa viwanja sita kuchezwa mechi za ufunguzi ingawa hafla ya uzinduzi wa ligi hiyo utafanyika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma katika mchezo ambao Baobao ya hapo itakapocheza na Victoria Queens ya Kagera.

Ligi hiyo ya kwanza kufanyika nchini Tanzania, lakini pia kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati imetokea kuvutia wadau kadhaa wakiwamo Azam Tv ambao wamedhamini kwa kuonyesha mubashara (live), michezo hiyo 30 itakayofanyika viwanja mbalimbali hapa nchini.

Viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwamo mawaziri na wabunge ambao kwa sasa wako kwenye vikao mjini Dodoma kwa pamoja wanatarajiwa kuwa katika hafla hiyo ambayo pilikapilika zake zinatarajiwa kuanza saa 8.00 mchana kabla ya mchezo kuanza saa 10.00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Holland Based Duo M.A.E MUSIC RELEASE NEW SONG FEAT BARAKA DA PRINCE

When it comes to songs about love in Bongo, you might say the topic is hugely saturated with each and every singer trying to showcase their singing talent.

Now M.A.E Music a group of two ladies, Martha Yoseph and Amy Elisabeth who are based in Holland have defied geographical distances and of course their passion for bongo fleva to release a brand new audio featuring Baraka Da Prince. Now we don't know about you but this one is definitely worth the listen. Be the first to listen here. 

In January M.A.E Music released Kitopokolo a video in which they featured the one and only Prince Dully Sykes who also doubles up as their Producer.

The Group which comprises of Martha Elina Joseph a Tanzanian/Dutch Singer & songwriter plus Amy Elisabeth a Dutch National, is currently on a two week holiday in Dar es salaam, Tanzania.
links za nyimbo zao on youtube
MAE Music ft. Barakah da Prince - I love you: http://youtu.be/aLOI174FymY
MAE Music ft Dully Sykes - Kitopokolo: http://youtu.be/HTiHmLhPPZ8

Haya ndiyo yaliyojiri kwenye soko la hisa wiki hii kuisha Ijumaa tarehe 31 Oktoba 2016.

http://tanzaniainvest.com/wp-content/uploads/2015/12/dse-dar-es-salaam-stock-exchange-tanzania.jpg
                       Mauzo ya Soko
Idadi ya mauzo imeongezeka kwa asilimia 39% na kufikia TZS 5.3 Bilioni kutoka TZS 3.8 Bilioni wiki iliyopita.
Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imeshuka kwa asilimia 91% hadi 869,453 kutoka 9.8 Milioni wiki iliyopita.
Kampuni tatu zinazoongoza kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa ni zifwatazo:
1.     CRDB kwa asilimia 51.8%
2.     TBL kwa asilimia 44.44%
3.     DCB kwa asilimia 1.22%

Ukubwa wa Mtaji wa Soko
Ukubwa wa mtaji wa soko umepanda kwa asilimia 1% na kufika Trilioni 21.8 kutoka Trilioni 21.6 wiki iliyopita.
Ukubwa wa mtaji wa makampuni ya ndani pia umepanda kwa asilimia 0.4% hadi Trilioni 8.19 kutoka Trilioni 8.16 wiki iliyopita.

Viashiria (Indexes)
Sekta ya viwanda imejitokeza wiki hii kuongezeka Zaidi ya pointi 26 baada ya bei ya hisa za TBL kuongezeka kwa asilimia 0.76%:

Bei za hisa za makampuni mengine ya ndani ziliendelea kubaki kwenye kiwango kile kile na kupelekea viashiria vya sekta za huduma za kibenki na za kibiashara kubakia kwenye kiwango kile kile wiki hadi wiki.
. by Exaud Msaka Habari on Scribd

Taarifa za Kifo cha Bondia wa Tanzania Thomas Mashali

Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali amefariki dunia usiku wa kuamkia leo October 31 2016 maeneo ya Kimara DSM, Taarifa zinadai kuwa alishambuliwa na wananchi baada ya madai ya kuitiwa mwizi.
Taarifa kutoka kwa Promota wake, Siraji Kaike amesema watu aliokuwa anagombana nao walimwitia mwizi na wakawa wamemshambulia na baadaye wakawa wamemtupa na bodaboda waliokuwa wanamjua Thomas Mashali walimuokota na kumpeleka hospitali ambapo baadaye zilitolewa taarifa kuwa amefariki.
SOURCE AYYO.COM

Sunday, October 30, 2016

Lowasa,Mbowe,Sumaye waumizwa,Biashara zao zataifishwa,Piki[iki za UVCCM zatoweka,Yanga Yaranda mbao soma MAGAZETI YA LEO TZ NA NJE .OKTOBA 31

Tigo yapanua huduma ya 4G LTE hadi Lindi na Mtwara

Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Pwani, Goodluck Charles
Wateja wa Tigo katika mikoa ya Lindi na Mtwara hivi sasa wanaweza kufurahia kuunganishwa na  intaneti ya kasi kufuatia  kampuni hiyo kupanua huduma yake ya 4G LTE  katika miji hiyo ya kusini mwa Tanzania. Teknolojia ya 4G LTE ni ya kasi takribani mara tano zaidi ya  teknolojia  ya 3G  iliyopo katika soko kwa hivi sasa.

Saturday, October 29, 2016

MAGAZETI YA LEO TZ NA NJE,OCT 30

Rais Magufuli Afanya Ziara Ya Kushtukiza Wizara Ya Maliasili Na Utalii Na Kushuhudia Pembe Za Ndovu 50 Zilizokamatwa

Rais Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri Katibu Mkuu wa  Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi baada ya kukagua pembe za ndovu 50 zilizokamatwa katika operesheni maalum ya kusaka majangili alipofanya ziara ya kushtukiza makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii (MPINGO HOUSE) jijini Dar es salaam leo Oktoba 29, 2016.


Advertisement

CHADEMA Waijibu CCM.......Wadai Lowassa ni Tishio Ndo Maana Wanamwandama, Waitaka CCM Ijiandae Kuachia Madaraka 2020


Baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia msemaji wake Christopher Ole Sendeka kusema kuwa aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Edward Lowassa, kuwa si tishio kwa CCM.

Jumamosi ya Oktoba, 29 Chadema imejibu kuwa Lowassa pamoja na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) utaendelea kuwa tishio kwa chama hicho na kwamba CCM ijiandae kuachia madaraka mwaka 2020 kwa kuwa imejipanga kuchukua dola.

KAULI YA ACT WAZALENDO KWA OLE SENDEKA NA CCM


TAARIFA KWA UMMA

CHAMA  cha ACT Wazalendo kimeshtushwa na tuhuma, kashfa, porojo na matusi mbalimbali yaliyotolewa jana na msemaji wa chama cha Mapinduzi(CCM), Ndugu Christopher Ole Sendeka dhidi ya Kiongozi wa chama chetu, ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto.
 Kutokana na hayo chama kina masuala yafuatayo ya kusema kwa wanachama wetu na umma wa Watanzania kwa ujumla:

• Chama chetu kinakaribisha uchunguzi juu ya mali na madeni ya Kiongozi wetu, ndugu Zitto. Tutafurahi uchunguzi huo ukihusisha akaunti zake za benki pamoja na mfumo wa maisha yake binafsi (Life Style). 
Tunavitaka vyombo vya uchunguzi vianze kazi hiyo mara moja kwani tunaamini kuwa  Kama kuna Kiongozi ambaye Mali, Madeni, Maslahi na Akaunti zake viko wazi basi ni ndugu Zitto. 

RC -PAUL MAKONDA AONGOZA MAHAFALI YA KIDATO CHA NNE SHULE YA SEKONDARY JITEGEMEE JKT MGULANI JIJINI DAR ES SALAAM

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati), akizungumza na wanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT Mgulani katika mahafali ya 32 yaliyofanyika jana. Makonda alikuwa mgeni rasmi. Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo, Luteni Kanali Robert Kessy na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi wa Shule hiyo, Brigedia Generali Laurance Magere.
RC Makonda akimkabidhi cheti Mwalimu Bora wa Shule hiyo, Grace Eliyatosha Moshi.
RC Makonda akimkabidhi zawadi Mwanafunzi Bora,  Samuel Ndebeto.
RC Makonda akipeana mkono na mhitimu wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT, Samina Rajab baada ya kumkabidhi cheti  katika mahafali ya 32 kwa ushiriki wake wa masuala ya Skauti shuleni hapo. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi wa Shule hiyo, Brigedia Generali Laurance Magere.
Huyu ndiye ni Mwanafunzi Bora wa Shule hiyo,  Samuel Ndebeto.
Mkuu wa Mkoa Paul Makonda (katikati), akiwa meza kuu na viongozi mbalimbali. Kutoka kulia ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Kigamboni, Luteni Kanali, Laurent Mgongolwa, Mkurugenzi wa Mipango ya Huduma Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Kanali Festus Mang'wela, Mkuu wa Shule ya Sekondari Jitegemee, Luteni Kanali, Robert Kessy, Mwenyekiti wa Bodi wa shule hiyo, Brigedia Generali mstaafu, Laurence Magere, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Wilaya ya Temeke, Hashim Komba na Mjumbe wa Bodi wa Shule hiyo, Sebastian Enosh.
Mgeni rasm Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na walimu na wafanyakazi wa shule hiyo.
Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo.
Mhitimu wa kidato cha nne akisakata rhumba kwenye mahafali hayo.
Walimu na wanafunzi wakicheza kwaito.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jitegemee JKT wakitoa burudani kwenye mahafali hayo.
Wahitimu ndani ya ukumbi.
Mgeni rasmi Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali waliokuwa jukwaa kuu.
RC Makonda akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu hao.
RC Makonda akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu hao.
Vijana wa Skauti wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Kwaya ya shule hiyo.

Friday, October 28, 2016

Lowasa na Zitto waitesa CCM,Sasa kuchunguzwa,Yanga wampigia magoti Kocha wao,Soma Magazeti ya Leo Jumamosi Oct 29 hapa

BENKI KUU YA TANZANIA (BoT) YACHUKUA USIMAMIZI WA BENKI YA TWIGA BAADA YA KUFILISIKA

 Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jioni hii kuhusu kuchukuliwa kwa benki hiyo ambayo ilikuwa ikimilikiwa na serikali kwa asilimia 100.
 Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mabenki, Kenedy Nyoni (kushoto), akichangia jambo kwenye mkutano huo. Kulia ni Gavana wa Benki Kuu, Profesa Beno Ndulu.
 Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki wa BoT, Victoria  Msina (kulia), akimkaribisha Gavana Beno Ndulu kuzungumza na wanahabari. Wa pili kutoka kulia ni Kaimu Katibu wa Benki, Mustafa Ismail.
 Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.
 Wapiga picha wakiwa kazini.
Taswira ya ukumbi huo wakati wa mkutano.