Saturday, December 31, 2016

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MWANDISHI WA HABARI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA AGIZO LA DC KAHAMA

TAARIFA KWA UMMA

UONGOZI wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Shinyanga (SPC),na baadhi ya waandishi wa habari wilayani Kahama,wamekutana na mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu ili kupata muafaka wa tatizo la kukamatwa na kufikishwa mahakamani mwandishi wa habari wa kujitegemea Paul Kayanda.

Kikao hicho cha usuluhishi kilichofanyika leo Jumamosi Desemba 31,2016 katika ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo,kimehudhuriwa pia na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya Kahama. 

MUST READ: AN OPEN LETTER TO 2016


Image may contain: 1 person, smilingAs we are left with only few hours before the year comes to an end, 2016 has been a journey that I can’t even begin to explain ESP on this platform, but I promise you my dear readers you will eventually read this…(keeping the juicy insights for my upcoming book).

This year has taught me a lot, it has made me the the most courageous woman than I have ever thought I was. (Did I just say woman 😁)
I have learnt that most people use words as mere “words”.
Through my long untold journey I have discovered so many secrets that made me finally open up to the world and especially to women.
Seriously, 2016, has been (throughout its existence) the epitome of blerg.

Friday, December 30, 2016

Bei ya umeme yapanda maradufu,Dr Mpango asema uchumi upo safi,Simba na ndoto za Ubingwa,soma magazeti ya mwisho kwa mwaka huu dec 31,2016,Jumamosi

Magazetini leo Jumamosi Desemba 31,2016

MAPUNDA: ITC TAYARI TUMEIPATA

img_0122

Baada ya kususua kwa takribani majuma mawili sasa  hatimaye  hati ya uhamisho ya kiungo Mrisho Khalfan Ngassa imetua  kwenye klabu ya Mbeya City fc  asubuhi ya leo .

VIONGOZI WA CHADEMA WASHIKILIWA NA POLISI ARUSHA


JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha linawashikilia watu 12, wakiwemo viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Arusha.



Viongozi hao walikamatwa kwa amri ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo wakituhumiwa kuhusika kuchoma moto mashine za kuvuta maji kutoka kwenye chanzo cha Kangdet wilayani Karatu kwa madai kwamba wanatekeleza agizo la Serikali, hatua ambayo imeelezwa kuwa haikufuata utaratibu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Arusha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, aliwataja waliokamatwa kuwa ni pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Karatu, Moshi Darabe ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Barai, anayedaiwa kuhamasisha wananchi kuchoma moto mashine hizo zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 16.

PHIRI:FITI DHIDI YA MBAO,NGASSA KUANZIA BENCHI

img_0983

ZIKIWA zimesalia  saa kadhaa kabla ya kuchezwa kwa mchezo wa ligi  kuu ya Vodacom Tanzania  bara  kati  Mbeya City fc na Mbao Fc kutoka jijini Mwanza uliopangwa  kuchezwa  kesho  jumamosi kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine  jijini hapa, kocha Kinnah Phiri amesema  maandalizi  kwa timu yake kuelekea mchezo huo yamekamilika  kinachosubiriwa ni dakika 90 huru za ndani ya uwanja.

MWANDISHI WA HABARI PAUL KAYANDA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA AGIZO LA DC KAHAMA

Paul Kayanda akipanda kwenye gari la polisi leo Ijumaa Desemba 30,2016
Mwandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Paul Kayanda amefikishwa mahakamani kwa agizo la Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkulu kwa madai kuwa mwandishi huyo wa habari anamchafua kwa njia ya email.

Mwandishi huyo anadaiwa kuandika habari kuhusu mkuu huyo wa wilaya kuibiwa laptop mbili nyumbani kwake kisha kuwaweka ndani/polisi kwa muda wa siku saba watu watatu akiwemo kijana anayeishi naye nyumbani bila kuwafikisha mahakamani.

Mwandishi huyo alikamatwa leo asubuhi kisha kufikishwa katika mahakama ya wilaya kisha kurudishwa tena polisi kutokana na kukosekana kutokuwepo kwa shtaka lolote lililofunguliwa kutoka polisi kwenda mahakamani.

Hata hivyo baada ya kurudishwa polisi,alifikishwa katika wilaya ya Mwanzo  wilayani humo na kusomewa mashtaka ya kumchafua mkuu huyo wa wilaya kisha kuachiwa kwa dhamana na kutakiwa kurudi mahakamani  Januari 02,2017.

Mkuu huyo wa wilaya amesema mwandishi wa habari huyo amefikishwa mahakamani kutokana na kuandika habari za kumchafua kwa kusambaza habari kupitia email na kumtumia sms alizodaiwa siyo za maadili.

Na Edo Kumwembe---Chid Benzi anatushangaa tunavyomshangaa

NI zaidi ya kujikuta juu ya kitanda na msichana unayempenda kuliko wote duniani. Ni zaidi ya kutazama bao la ushindi la timu yako katika dakika za majeruhi katika mechi muhimu. Yote haya hayazidi starehe ya kubwia unga.


Sahau kuhusu bia, sigara, Sahau kuhusu kila starehe. Inatajwa kuwa hakuna starehe kama unga. Na sasa Watanzania wanaendelea kumshangaa mtu anayeitwa Chid Benz. Mwanamuziki hodari wa kizazi hiki katika zile staili za vijana za muziki wa kufokafoka.
Chid anateketea. Mwili wake kwa sasa ni kama mahindi ya shambani yaliyoliwa na nzige. Mwili wake ni kama kama gari lililoungua likaisha. Amebaki mifupa tu. Unaweza kupishana naye bila ya kumfahamu kama bado kichwani unatembea na taswira ya yule Chid Benzino mwenye mashavu manene, miwani usoni, na taulo shingoni.
Wasichofahamu watu wengi ni ukweli kwamba wakati sisi tukiendelea kumshangaa Chid, kumbe yeye ndiye anatushangaa zaidi sisi. Anatushangaa kwanini hatuungani naye katika starehe yake tamu. Anatushangaa kwanini hatupo katika safari yake ya kubembea.
Kwanini anatushangaa? Ninesema hapo juu hakuna starehe tamu zaidi ya unga. Kitu cha muhimu hili ni kutoonja starehe yenyewe. Ukionja hautabaki. Hata Chid si ajabu zamani alikuwa analaani wala unga. Kosa kubwa alilifanya katika kuonja tu. Ukionja ni vigumu kutoka katika mtego.
Ni hapo ndipo lilipo tatizo la Chid na watumiaji wengine. Kikubwa wanachotakiwa kukifanya kuachana na unga hawawezi kukifanya. Kitu cha kwanza kabisa ni kuukana utamu wake. Kuukana utamu wake ni kama kuikana nafsi yako. Hapa ndipo ilipo vita kubwa ya kuacha.
Kwanza inabidi uone mapungufu makubwa ya unga lakini kama ukilegeza moyo kamwe hauwezi. Kwa mfano, leo Chid hajioni mchafu, hajioni amekonda, hajioni amepoteza nuru. Utamu wa unga umezidi akili ya kujitafakari (self assessment). Ikifika hapo kazi inakuwa nzito zaidi.
Kumpeleka Chid katika vituo vya matibabu (rehabilitation centres) ni kupoteza muda mpaka pale moyo wake utakapoanza kujifanyia self assessment kuwa amepotea, anahitaji msaada na anachukia unga. Akifika hapo atashinda vita.
Chukulia kwamba familia yako imekuomba mtoke out na uwape muda wa kuwa na wewe. Wanaweza na tabia yako ya kupenda mpira kuliko wewe. Unawakubalia walichokuomba. Lakini wanakupeleka katika hoteli ambayo watu wanatazama mpira. Lazima moyo wako utakuwa unafuatilia kwa karibu matokeo huku mwili wako ukiwa mezani na familia.
Kitu cha aina hiki kinaitwa addiction. Ndipo alipofika Chid. Kama ambavyo wewe unashangaa kwanini mtu hapendi mpira au muziki, basi na ndivyo Chid anavyotushangaa kwanini na sisi wengine hatupendi unga. Alipofikia yeye na sisi wengine wote tumefika ingawa sisi tuna starehe tofauti na yeye.
Kabla ya matibabu kitu cha msingi kwa Chid ni kukutana na mwanasaikolojia wa kumshawishi aelewe kwamba kitu anachokiona kitamu kumbe sio kitamu. Nani anaiweza kazi hii? Ni kazi ngumu. Ndio maana washkaji zake walipompeleka Bagamoyo alitoroka na kuendelea na starehe yake kwa sababu hakuwa tayari kuona utamu wake unaitwa uchungu.
Mwisho wa Chid? Sitaki kuingilia kazi ya Mwenyezi Mungu lakini mwisho wake unatabirika kiurahisi zaidi pengine kuliko mwisho wa watu wengi tunaomshangaa. Sisi tuna siku zetu za ahadi na tunaweza kuondoka mapema hapa duniani kuliko yeye, hata hivyo tutaondoka kwa vifo visivyotabirika.


Chid anaweza kufuata njia za akina Whitney Houston tu. Watu wengi wa aina yake huwa inatokea tunawaokota mtaroni au chumbani wakiwa wametangulia Mbele ya haki. Inatokea huwa wanajidunga kupitiliza, au kuliko miili yao inavyoweza kuhimili uzito wa dawa aliyotumia siku hiyo. Kwa kiingereza cha matumizi ya unga wanaita overdosing.
Hili sio la kuombea lakini maisha ya kufichana yamepita zamani jamani. Kama tunahitaji lisitokee basi ni kwa Chid mwenyewe kumjua adui yake na kupambana naye. Adui wa Chid sio unga. Adui wa Chid ni akili yake mwenyewe. Unga upo tu, lakini mbona wengi hatutumii?


Ana bahati mbaya ameangukia katika starehe ambayo inammaliza. Sisi wengine tuna matatizo kama yake ya kuendekeza starehe lakini bahati nzuri huwa hazitumalizi. Starehe ya kubishana nani zaidi ya Lionel Messi na Ronaldo haiwezi kutumaliza kwa urahisi.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA MCHAMBUZI EDO KUMWEMBE 

ACT WAZALENDO KUZINDUA KAMPENI ZAKE KESHO..NI UCHAGUZI MDOGO

TAARIFA KWA UMMA

KESHO Disemba 31/2016 Chama cha  ACT Wazalendo, tutazindua rasmi kampeni  za kuwania Ubunge na nafasi za udiwani katika kata ambazo tumesimamisha wagombea
Kutokana na uzinduzi huo awamu ya kwanza ya viongozi  wa kitaifa watagawanyika katika timu mbili tofauti  kwa ajili ya kushiriki kampeni hizo.

Timu ya kwanza itaongozwa na mwenyekiti wa Chama Mama Anna Mghwira na makamu Mwenyekiti wa Chama Tanzania Bara, Mzee Shaban Mambo ambapo ziara yao itaanzia mkoani Geita katika kata ya Nkome(Disemba 31) Kahama katika kata ya Isagenhe(Januari Mosi),Dodoma katika kata ya Ihumwa(Januari 2),Morogoro, katika kata ya kiwanja cha ndege(Januari 3),Dar esSalaam katika kata ya Kijichi(Januari 4) na Zanzibar katika jimbo la Dimani (Januari 5)

MAONI YA WATEJA NI MUHIMU KWA UKUAJI WA BIASHARA YAKO

Na Jumia Travel Tanzania

KUJA kwa maendeleo ya sayansi na teknolojia hususani mtandao wa intaneti kumebadilisha kwa kiasi kikubwa mienendo ya matangazo ya utoaji wa huduma mbalimbali duniani na hii ni kutokana na uwezo wake wa kuwaruhusu wateja kutoa ushuhuda, kukosoa au kutoa maoni juu ya walichohudumiwa na kujionea.

Tofauti na kipindi cha nyuma kidogo ambapo wataalamu wa masoko walikuwa wanatumia zaidi njia za luninga na redio kuwafikia wateja wao, siku hizi mfumo wa intaneti unapewa kipaumbele zaidi kutokana na namna unavyofikia watu wengi zaidi ndani ya muda mfupi, kwa haraka na gharama kidogo.

Matangazo ya luninga na redio yanaweza kuwa hayana ushawishi mkubwa ukilinganisha na mtandao wa intaneti kwani hivi sasa makampuni yanaweza kuwasilisha bidhaa na huduma zao na kupokea majibu kujua kwamba zinakubalika au la. Hali hiyo ni dhahiri kutokana na makampuni mengi kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika teknolojia na rasilimali watu katika kusimamia tovuti na kurasa zao rasmi za mitandao ya kijamii kama vile facebook, twitter, instagram na mingineyo.

Kupitia tovuti na kurasa hizo za mitandao ya kijamii biashara na huduma nyingi zinafanya vizuri kutokana na ushawishi wao kwenye mitandao kutokana na namna ambavyo zinazungumziwa vizuri na watu wengi. Lakini pia husaidia kampuni hizo husika kuwasiliana moja kwa moja na wateja wao kwa sababu wateja huwasilisha maoni yao moja kwa moja mtandaoni tofauti na luninga au redio ambazo hutoa fursa ya kuona au kusikiliza tu matangazo.

Vivyo hivyo hali hii inaweza kusaidia sana ukuaji wa sekta ya utalii na ukarimu kama vile huduma za hoteli na malazi ambazo hujitangaza zaidi kupitia namna wateja wanavyozizungumzia.

Jumia Travel (www.travel.jumia.com) kampuni unaongoza kwa huduma za hoteli mtandaoni barani Afrika umezitunuku vyeti hoteli kadhaa ambazo zilizopendekezwa na kutembelewa ndani ya wateja wengi kipindi cha mwaka mzima wa 2016.

Akizungumzia juu ya umuhimu wa vyeti hivyo Meneja Mkazi wa Jumia Travel Tanzania, Bi. Fatema Dharsee amesema kuwa, “Vyeti hivi vina umuhimu mkubwa kwani ni viashiria vikubwa vya namna hoteli yako inatathminiwa vipi na wateja pindi wanapoitembelea. Siku zote wateja huambizana huduma wanazozipata sehemu za biashara wanazotembelea na kutokana na ushuhuda huo ndio na wengine hushawishika kutembelea pia. Kupitia mtandao wetu wateja wanayofursa ya kutoa maoni juu ya hoteli walizozitembelea, huduma walizopatiwa, mapungufu waliyoyaona na maboresho ambayo wangependa yafanyiwe kazi.”

“Imefikia mahala sasa ni lazima wataalamu wa masoko watambue mchango na ushawishi walionao wateja kwenye kukua kwa biashara zao kwani nguvu yao ni kubwa zaidi ya matangazo wanayoyalipia kupitia luninga na redio au njia nyinginezo. Maneno au ushuhuda unaotolewa na wateja unatosha kwa kiasi kikubwa mtu kutumia bidhaa au huduma yako kwani ni halisi kutokana na mtu kuitumia au kupatiwa huduma hiyo husika. Hivyo ningependa kutumia fursa hii kuwataka mameneja wa hoteli waliokabidhiwa vyeti hivi kuichukulia hali hii kama ni changamoto kwao kwa kufuatilia maoni ya wateja yanayoachwa kwa njia ya mtandao na kuyafanyia kazi.” Alihitimisha Bi. Dharsee.

Hoteli ambazo zimepatiwa vyeti hivyo ni pamoja na Jafferji House & Spa Hotel na Garden Lodge za visiwani Zanzibar, Golden Tulip Hotel, Peacock Hotel na Butterfly Hotel zote za jijini Dar es Salaam.

Thursday, December 29, 2016

Mbowe amtupia neno JPM,adai amejaa Hofu,kiama cha wakwepa kodi ardhi wiki ijayo,waliomuua Dr Mvungi waanza kuachiwa Huru,Simba Sc kama Ulaya vile yamaliza mwaka kwa shangwe.Magazeti ya leo dec 30 ijumaa 2016 yapo hapa soma


Kubenea aivuruga CHADEMA,baada ya kudai Ben saanane Yupo mtaani,Makada wataka akamatwe asaidie Polisi

Tangu kutokea sintofahamu juu ya wapi alipo kada maarufu wa chadema Ben saanane kumekuwa na minongono mingi juu yake huku mengine yakihusishwa na kile kinachoitwa kutekwa na wapinzani wake kisiasa,huku wengine wakiamini kuwa Kada Huyo amejihifadhi mahali ili kitengeneza jina lake kisiasa.

Gazeti la mwanahalisi ambalo linaongozwa na Mbunge wa chadema Ubungo na mwandishi nguli wa uchunguzi Said Kubenea wiki hii limebadilisha upepo wa sakata hilo baada ya kudai kuwa Kada huyo hajapotea na yupo mtaani anaonekana akipata kahawa na rafiki zake.

SOMA BAADHI YA SENTENS ZA MAKALA HIYO HAPA

UTATA kuhusu kutoonekana kwa Bernard Saanane, msaidizi wa masuala ya siasa wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe sasa unazidi kuongezeka. Wanaandika Waandishi Wetu …. (endelea).

Taarifa zinasema Saanane ambaye haonekani nyumbani wala kazini, anaonekana kwa marafiki zake mitaani. Mjumbe mmoja wa Kamati Kuu (CC) ya Chadema amesema, “Nina wasiwasi kama siyo mkakati binafsi wa kisiasa. 

Kijana Saanane amekuwa akionesha kutaka kukwea madarakani haraka hata nje ya taratibu. ”

Baada ya makala hiyo makada mbalimbali wa chadema akiwemo huyo maarufu kama Malisa ameamua kuandika hitaji lake la kutaka polisi kumkamata mara moja kada mwenzao Said Kubenea kwa ajili ya kueleza ukweli juu ya kuonekana kwa Ben Saanane.
SOMA ALICHOKIANDIKA
Taarifa za Mhe.Kubenea kwamba Ben yupo mtaani anarandaranda na kujificha kwa rafiki zake, ni
taarifa zinazopaswa kufanyiwa kazi na Jeshi la Polisi na uongozi wa Chadema. Takribani mwezi mmoja sasa polisi na Uongozi wa Chadema umetoa taarifa rasmi za kumtafuta Ben. Leo Kubenea anasema Ben yupo mtaani, anaonekana kwenye vijiwe vya kahawa.

Ni vizuri Polisi wakamkamata Kubenea aeleze ni mitaa ipi Ben alionekana, na ni vijiwe vipi vya kahawa alivyokutwa. Je alikua na nani? ni siku gani? aliyemuona ni nani? na kwanini alipomuona hakutoa taarifa polisi? Na kwa kuwa Kubenea anajua polisi wanamtafuta kwanini alipojua Ben yupo mtaani hakwenda kuripoti polisi ili awasaidie ktk kufanya uchunguzi? Kwanini Kubenea anawaacha Polisi watumie rasilimali kubwa kumtafuta Ben wakati anajua Ben amejificha ili kujipatia umaarufu wa kisiasa?

Kubenea anasema Ben anatafuta umaarufu, je ni umaarufu gani wa kujipoteza? Ili iweje? Kwa faida ya nani? Kwamba Ben akijipoteza ndo anakua maarufu? Halafu huo umaarufu unamsaidiaje? Kugombea nafasi ya uongozi kwenye chama? Ni nafasi gani ambayo mtu huchaguliwa kwa kujipoteza? Na ni akina nani watakua wajinga wa kumpa mtu kura kwa sababu tu alijipoteza? Hivi kujipoteza kwa Ben kunamuongezea kura au kunampunguzia?

Kama kweli Ben yupo mtaani, je Kubenea haoni kuweka taarifa gazetini ni kumfanya azidi kujificha? Kwanini asingewaarifu polisi kwanza wamkamate then ndo aweke gazetini? Na hao marafiki zake Ben waliomficha huko mtaani ni mahiri wa ujasusi kiasi gani? Je wamewazidi akili polisi, usalama wa taifa na intelijensia ya Chadema? Je Kubenea kuandika habari bila kujibu maswali muhimu (5Ws +H) haoni kunaifanya habari hiyo kukosa uhalali wa kuaminika mbele ya jamii?

Na kwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema Mhe.Freeman Mbowe alitamka hadharani kuwa kuna uwezekano Ben ametekwa, je Kubenea kusema Ben kajificha haoni anamfanya Mbowe kuonekana ameshiriki kumficha Ben? Kwa kuwa Kubenea ameshindwa kutaja vyanzo vyake vya habari haoni habari hiyo inaweza kuonekana ni ya kutunga maana haina credible source? Je ikija kubainika kuwa Ben ametekwa au amekufa, je Kubenea haoni kwamba atakua amewakosea sana watanzania, kuikosea familia ya Ben, na hata nafsi yake mwenyewe?

Sisemi kuwa Ben hawezi jificha, as a human being anaweza kufanya hivyo na ikibainika kajificha nashauri achukuliwe hatua kali za kisheria. Lakini ukweli ni kuwa habari ya Kubenea imeacha maswali mengi kuliko majibu.
Nahofia Kubenea asije kuwa ameandika habari hiyo kwa chuki binafsi dhidi ya Ben halafu baadae akaja kujuta. Nafahamu ugomvi binafsi kati ya Ben na Kubenea uliosababishwa na tofauti za kisiasa. Kuna mengi yalitokea ambayo siwezi kuyasema yote hapa lakini Ben na Kubenea wamewahi kunyukana kwa nyakati tofauti kwa sababu mbalimbali (ushahidi wa maandishi yao wakinyukana upo).

Sasa isije kuwa Kubenea anaendeleza mnyukano kati yake na Ben akasahau suala la uhai wa mtu ni muhimu kuliko tofauti zao za kisiasa. Ikibainika Ben amejificha Kubenea atakua shujaa kwenye hili, lakini ikija kubainika kuwa Ben amekufa, kuuawa au kutekwa, dhamiri ya Kubenea itamhukumu maisha yake yote. Ni vizuri kuwa na akiba ya maneno.!

AMUUA RAFIKI YAKE KWA PANGA,ATAFUNA UBONGO KISHA KULA SEHEMU ZAKE ZA SIRI


JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya,linamshikilia mchimba dhahabu, Shija Salum (38), mkazi wa Kahama mkoani Shinyanga kwa tuhuma za kumuua rafiki yake na kula ubongo wake.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba pamoja na mtuhumiwa huyo kula ubongo wa rafiki yake huyo aliyetambuliwa kwa jina moja la Shija, pia alitafuna sehemu zake za siri baada ya kuzikata.

Viongozi 22 wa kitaifa CHADEMA kuzindua kampeni kanda ya Kaskazini


Viongozi 22 wa kitaifa wa Chadema wanatarajia kushiriki uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata nne za mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro kuanzia leo.


Kampeni hizo zitazinduliwa kwenye Kata ya Duni, mjini Babati ambako chama hicho kimemteua Ally Muhidini kugombea udiwani.

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa amesema watazindua kampeni kwa kila kata ikiongozwa na viongozi wa kitaifa na wabunge.

Golugwa amesema wabunge 22 wa Chadema Kanda ya Kaskazini wamepangwa kusimamia kata hizo na kwamba wanne watakuwa katika kata moja. Pia, madiwani 352 wa chama hicho katika kanda hiyo watashiriki kwenye kampeni.

“Tumejipanga kushinda kata zote, katika uchaguzi uliopita tulishinda kata moja tu kati ya hizi nne,” amesema.

Golugwa amesema uzinduzi wa kampeni kwenye kata nyingine tatu utatangazwa baadaye. Hata hivyo, amesema wameshaanza kampeni za nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha Januari 22 wanashinda viti hivyo.

Wednesday, December 28, 2016

LEMA SIKIO LA KUFA RUFAA YAKE YAGONGA MWAMBA,ARUDISHWA RUMANDE

Mbunge Godbless Lema amerejeshwa tena rumande leo baada ya rufaa yake ya kupinga kunyimwa dhamana kushindikana kusikilizwa kama ilivyokuwa imepangwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo.

INASHANGAZA--SODA YAUA MTU MKOANI ARUSHA


JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha linamshikilia mkazi wa Olasiti, jijini Arusha, Hamisi Amani (17), kwa tuhuma za kumuua mwenzake wakati wakigombea soda.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, tukio hilo lilitokea Desemba 25, mwaka huu, saa mbili usiku katika eneo la Kwa Morombo.

MAAMBUKIZO YA VVU NA UKIMWI YASHUKA KWA ASILIMIA 20 NCHINI

 Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) Dk.Leonard Maboko (katikati), akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, wakati akitoa taarifa kuhusu mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi katika mkutano wa kujitambulisha kwao tangu ateuliwe na Rais Dk.John Magufuli kushika nafasi hiyo Julai 7 mwaka huu. Kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Muitikio ya Kitaifa, Dk.Hafidhi Amri, Mkuu wa Kitengo cha Sheria Tacaids, Elizabeth Kaganda na Mkurugenzi wa Habari na Ulaghibishi, Jumanne Issango.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) Dk.Leonard Maboko (kushoto), akisisitiza jambo kwenye mkutano huo. Kulia ni Mkurugenzi wa Habari na Ulaghibishi, Jumanne Issango.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Wapiga picha wakichukua taarifa hiyo.

Tuesday, December 27, 2016

Lema,Lissu wanaongoza kukamatwa 2016,Bei ya Umeme yapaa,Ridhiwani ainyooshea Kidole serikali ya JPM,Chadema hawataki Ujinga ukuaji wake watisha.Soma magazeti ya leo december 28,2016 hapa

ei ya

MWALIMU ASHUSHIWA KIPIGO KWA KUMCHARANGA MAPANGA MWANAFUNZI WAKE SIKU YA KRISMASI

Kijana Limbe akipata matibabu
Mwalimu Pendo akipata matibabu
*****

MWANA HABARI MPOKI BUKUKU AZIKWA MKOANI DODOMA,ANGALIA PICHA


Alice Mama wa Marehemu Mpoki Bukuku akisaidiwa kuweka shada la maua katika kaburi la mwanaye Mpoki Bukuku wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika Msalato nje kidogo ya mji wa Dodoma Marehemu Mpoki alifariki wiki iliyopita jijini Dar es salaam kwa kugongwa na gari maeneo ya Mwenge.
Watoto wa Marehemu Mpoki Bukuku Junior akiongozana na wadogo zake wakiweka shada la maua katika kaburi la baba yao wakati wa mazishi yaliyofanyika Msalato nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Junior akiwa ameshikilia msalaba kwa majonzi wakati wa mazishi ya baba yake.

Benki Kuu (BoT) yatolea ufafanuzi taarifa za kutotumika tena noti ya shilingi 500



Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuwafahamisha wananchi wote kuwa habari inayoenea katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba noti ya shilingi mia tano haitatumika tena baada ya Disemba 31, 2016 sio taarifa ya kweli na ni uvumi unaopaswa kupuuzwa.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma za kibenki BoT, Marcian Kobello ambapo alifafanua kuwa noti ya shilingi 500 itaendelea kuwepo katika mzunguko sambamba na ile sarafu ya shilingi 500 hadi pale noti hiyo itakapotoweka mikononi mwa wananchi.

ACT WAZALENDO NA UCHAGUZI WA MARUDIO

Tunapenda kuwafahamisha wanachama wa ACT Wazalendo na umma wa watanzania kwa ujumla, kuwa kampeni  kwa ajili ya chama cha ACT Wazalendo katika jimbo la Dimani visiwani Zanzibar na kata mbali mbali kwa Tanzania bara ambazo chama kimesimamisha wagombea zitafunguliwa rasmi disemba 31/2016

SABODO AMSHAURI RAIS MAGUFULI AZIDI KUPUNGUZA BARAZA LA MAWAZIRI


 Mfanyabiashara maarufu nchini, Jaffar Sabodo akizungumza nyumbani kwake Upanga Dar es Salaam  mwishoni mwa wiki, ambapo alimtaka Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Rais John Magufuli azidi kupunguza Baraza la Mawaziri kufikia 15 na Kamati Kuu 15 pamoja na Halmashauri Kuu wajumbe 55. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Monday, December 26, 2016

TFF WAMLILIA MPOKI BUKUKU MPIGA PICHA ALIYEAGWA LEO DAR

Wakati mwili wa Mwanahabari, Mpoki Bukuku ukiagwa leo jijini Dar es Salaam, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Theophil Makunga kutokana na kifo hicho.

NAPE,MBOWE WAONGOZA KUUAGA MWILI WA MPOKI BUKUKU DAR

 Wanahabari wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mwandamizi wa The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku baada ya kutolewa heshima za mwisho katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Tabata, Dar es Salaam, tayari kulisafirishwa kwenda kwao Msalato Dodoma kwa mazishi. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akiwaongoza waombolezaji kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mwandamizi wa The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Tabata, Dar es Salaam. Mwili wa Mpoki ulisafirishwa kwenda kwao Msalato Dodoma kwa mazishi.
 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman  akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa mpendwa wetu Mpoki Bukuku

Sunday, December 25, 2016

MCHUNGAJI LUSEKELO 'MZEE WA UPAKO' AFUKUZA WAANDISHI WA HABARI KANISANI


MCHUNGAJI wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako, aliwagomea waandishi wa habari kusikiliza hotuba yake ya ibada na kutuma wasaidizi wake wawaondoe waandishi hao.


“Samahani tunaomba muondoke kwani Mchungaji amesema hataki kumuona mwandishi hivyo tunaomba muende kwenye makanisa mengine,” alisema msaidizi huyo na kuhakikisha waandishi wote wanaondoka eneo hilo majira ya saa sita kasoro mchana.

Saturday, December 24, 2016

WAKRISTO WALIVYOSHIRIKI IBADA YA MKESHA WA KRISMASI JIJINI DAR ES SALAAM

 Askofu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, akisalimiana na muumini wa kanisa hilo Usahrika wa Azania Front, Violet Muro baada ya kumpatia zawadi ya ibada mkesha wa Krismasi iliyofanyika jana usiku jijini Dar es Salaam.
 Kwaya ya Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Akbano ikitumbuiza katika ibada iliyofanyika katika kanisa hilo jijini Dar es Salaam.
 Waumini wa Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano wakiwa kwenye ibada ya mkesha wa krismasi.
 Vijana wa Kanisa la KKKT la Azania Front wakiigiza igizo la kumbukumbu ya kuzaliwa Yesu Kristo.
 Kwaya ya Vijana ya KKKT usharika wa Azania Front ikitoa burudani.
 Kwaya ya vijana ya KKKT Usharika wa Azania Front ikiendelea kutoa burudani.
 Watoto wakishiriki ibada katika Kanisa la KKKT la Azania Front
 Askofu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa akimsalimia muumini wa kanisa hilo, Violet Njau aliyekuwa ameongoza na familia yake.
 waumini wakiwa nje ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri usharika wa Azania Front baada ya ibada hiyo.

Kwaya ya Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph ikitoa burudani