Wednesday, January 4, 2017

AKAMATWA NA POLISI AKIFUKUA KABURI LA ALBINO


Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia mtu mmoja kwa tuhuma za kufukua kaburi la marehemu ambaye likuwa ni mlemavu wa ngozi (Albino) aliyefariki mwaka 2010 kwa lengo la kuchukua viungo vyake.



Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa na Kamanda a Polisi Mkoani Mbeya DCP Dhahiri Kidavashari inasema kuwa mnamo tarehe 03.01.2017 majira ya saa 01:00 usiku katika Kijiji cha Mumba kilichopo Kata ya Ilembo, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JONAS JOHN mkazi wa Chapakazi alikamatwa na askari Polisi akiwa na wenzake wawili wakifukua kaburi la marehemu SISTER OSISARA aliyekuwa mlemavu wa ngozi (ALBINO)

Inadaiwa kuwa marehemu alifariki dunia mwaka 2010 kwa ugonjwa wa homa na kuzikwa katika makaburi ya Kijiji cha Mumba.

Mtuhumiwa alikutwa na majembe na makoleo ambayo walikuwa wakiyatumia kufukuria kaburi hilo. Baada ya mahojiano mtuhumwa huyo aliwataja washirika wenzake wawili ambao walikimbia baada ya kuwaona askari.

Jeshi hilo linaendelea na msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa .

Katika tukio lingine Mnamo tarehe 03.01.2017 majira ya saa 3:30 usiku katika kata ya Makongolosi wilayani Chunya, mkoa wa Mbeya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la KELVIN KUBANDA mkazi wa Kahama alikamatwa akiwa na bhangi kete 10 sawa na uzito wa gramu 55.

Mtuhumiwa alikamatwa akiwa katika kijiwe cha kuvutia Bhangi. Upelelezi unaendelea.

No comments: