Friday, January 20, 2017

NAIBU WAZIRI MASAUNI AIONGOZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KUTEMBELEA GEREZA LA KILIMO SONGWE

Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimpokea Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kanali Mstaafu Masoud Ally (wapili kushoto), wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na Gereza la Kilimo Songwe, wilayani Mbalizi, mkoani  Mbeya. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kanali Mstaafu Masoud Ally, akiwaongoza wajumbe wengine wa kamati hiyo kusalimiana na Maafisa wa Jeshi la Magereza wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na Gereza la Kilimo Songwe, wilayani Mbalizi, Jijini Mbeya. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wapili kulia), akiongozana na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kanali Mstaafu Masoud Ally (wakwanza kulia), kuingia ndani ya Gereza la Kilimo la Songwe,lililopo wilayani Mbalizi, jijini Mbeya,  ambapo wajumbe wa kamati walipata fursa ya kusikiliza maoni kupitia  risala iliyoandaliwa na wafungwa wa gereza hilo.Wengine ni viongozi wa gereza hilo. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

CAP PIX 4
Afisa wa Jeshi la Magereza  akijibu maswali yaliyoulizwa na wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama walipotembelea shamba la mahindi linalomilikiwa na Gereza la Kilimo la Songwe, lililopo wilayani Mbalizi, mkoani Mbeya.Wa kwanza kulia ni Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akijibu maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari baada ya kumaliza ziara ya kutembelea shamba la Mahindi linalomilikiwa na Gereza la Kilimo Songwe, lililopo wilayani Mbalizi, jijini  Mbeya.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

No comments: