Thursday, January 19, 2017

NAIBU WAZIRI MASAUNI AKUTANA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA JIJINI MBEYA

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akijibu maswali yaliyoulizwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakati wa ziara ya kikazi iliyofanyika leo jijini Mbeya.Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Kanali Mstaafu Masoud Ally.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi) 
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kapteni Mstaafu Goerge Mkuchika, akizungumza wakati wa kipindi cha kuuliza maswali yaliyoelekezwa kwa Idara zilizopo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.Kamati hiyo imekutana  jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Juliana Shonza (katikati) akizungumza wakati wa kipindi cha kuuliza maswali yaliyoelekezwa kwa Idara zilizopo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi .Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo.Kamati hiyo ya Bunge  iko jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Rehema Madusa akizungumza wakati wa mkutano na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama,iliyokutana jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Mkuu wa Idara ya Uhamiaji mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi , Asumsio Achachaa, akijibu maswali yaliyoelekezwa kwenye Idara yake na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama(hawapo pichani), wakati wa mkutano na kamati hiyo iliyokutana Jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)


No comments: