Monday, January 9, 2017

TAASISI YA KAREMJEE JIVANJEE FOUNDATION YATOA ZAWADI YA UFADHILI WA MASOMO KWA WANAFUNZI WA TANZANIA

Nadhra Mresa akikabidhiwa zawadi yake kutoka kwa Yusuph Karimjee wakati wa Hafla Fupi ya kukabidhi zawadi kwa washindi hao.
 Taasisi ya Karimjee Jivanjee Foundation imewapatia zawadi Diana sosoka na Nadhra Mresa ambao ni wanafunzi wa shule ya secondary ya wasichana Mtwara kwa kuibuka washindi wa kwanza kwenye mashindano ya wanasayansi chipukizi Young Scientist Tanzania (YST) kwa mwaka 2016.

Akizungumza na wahabari wakati wa Hafla ya kuwaaga washindi hao wanaoelekea katika Jiji la Dublin nchini Ireland kwa niaba ya mwenyekiti wa KJF Yusuph Karimjee amesema kuwa wawili hao watapata ufadhili wa masomo wa elimu ya juu pindi watakapohitimu masomo yao ya kidato cha sita.
Diana sosoka Mshindi wa shindano la wanasayansi chipukizi akikabishiwa zawadi yake kutoka kwa Yusuph Karimjee leo Jijini Dar es salaam.
Wanafunzi hao watasafiri kwenda Dublim nchini Ireland leo kwa ajili ya kushughudia mashindano ya Tafiti mbalimbali ya kisayansi zilizofanywa na wanafunzi wa nchi hiyo,hatua ambayo itawaongeza ujuzi wanafunzi hao wa mtwara wa namna ya kuboresha mradi wao.


Mwenyekiti wa taasisi hiyo ya KJF amesema kuwa wao wanafuraha kubwa kuwa moja kati ya wafanikishaji wa wanafunzi hao kutimiza ndoto zao za kimasomo hasa kiwango chao cha masomo ya sayansi jambo ambalo linapiganiwa na dunia nzima kuwa na wanasayansi wengi.
Wasichana hao walishiriki mashindano ya wanafunzi mbalimbali wanasayansi yaliyoandaliwa na Taasisi ya young scientist Tanzania TYS Ambapo yalishirikisha wanafunzi kutoka shule mbalimbali nchini Tanzania wakionyesha ubunifu mbalimbali wa kisayansi ambao wamebuni.


Wanafunzi hao kutoka Mtwara secondary waliibuka kidedea baada ya kueleza wazo lao la kutaka kuwasaidia kina mama wa mkoa wa mtwara kuondokana na umasikini waliokuwa nao kwa kuwafundisha ufugaji wa kisasa wa kutotolesha kuku ambao wanaweza kuutumia katika kujikwamua na umaskini ulio mkubwa.

Wakizungumza na wanahabari wasichana hao wamesema kuwa masomo ya sayansi yamekuwa yakionekana kama ni magumu sana hasa kwa watoto wa kike jambo ambalo wamesema sio kweli bali kinachihitajika ni juhudi za kweli na nia ndiyo itakayomsaidia msichana mwanafunzi kufikia malengo yake.

No comments: