Wednesday, January 4, 2017

UVCCM WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KUMTUMBUA KIGOGO WA TANESCO

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umesema kuwa umefurahishwa na kitendo cha Rais Magufuli cha kupigania maslahi ya wanyonge na kuzuia kupandisha bei ya umeme nchini.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka wakati wa kikao cha watumishi wa umoja huo wa kutathmini utendaji kazi wa mwaka 2016 na kuweka utendaji wa mwaka huu.

Shaka amesema kitendo cha Rais Magufuli kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), Mhandisi Felchesm Mramba, ameonyesha uzalendo, ujasiri na upendo kwa wananchi ambao walimpa dhamana ya kuongoza nchi.

“UVCCM tunaunga mkono uamuzi wa Rais wa kuzuia kupanda kwa bei ya umeme na ametazama maslahi ya wananchi waliomchagua kuingia madarakani,”amesema Shaka.

Hata hivyo, amesema kuwa Tanesco kupitia kwa Mkurugenzi wake Mramba aliyetumbuliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo waliwaahidi wananchi kutopandisha bei ya umeme.

No comments: